Muhtasari wa Bakteria

NaLarry M. Bush, MD, FACP, Charles E. Schmidt College of Medicine, Florida Atlantic University;
Maria T. Vazquez-Pertejo, MD, FACP, Wellington Regional Medical Center
Imekaguliwa naBrenda L. Tesini, MD, University of Rochester School of Medicine and Dentistry
Imepitiwa/Imerekebishwa Imebadilishwa Feb 2025
v782369_sw

Bakteria ni viumbe wadogo sana, wenye seli moja. Ni miongoni mwa viumbe hai wa kwanza kabisa kujulikana duniani. Kuna mamilioni ya aina tofauti za bakteria, na wanaishi katika kila mazingira yanayoweza kufikirika kote duniani. Wanaishi kwenye udongo, maji ya bahari na ndani kabisa ya gamba la dunia. Baadhi ya bakteria wameripotiwa hata kuishi katika taka nururishi. Bakteria wengi huishi na kuingia katika miili ya watu na wanyama—kwenye ngozi na njia za hewa, mdomoni, na njia za kumeng'enya chakula, za uzazi na za mkojo, bila kusababisha madhara yoyote. Bakteria kama hao huitwa flora wakaazi. Kuna angalau idadi ya bakteria katika flora wetu wakaazi inayolingana na ya seli za mwilini. Flora wengi wakaazi wanaoishi husaidia watu—kwa mfano, kwa kuwasaidia kusaga chakula au kwa kuzuia ukuaji wa vijidudu wengine hatari zaidi.

Ni aina chache tu za bakteria kwa kawaida huhusishwa na ugonjwa halisi na hujulikana kama pathojeni. Wakati mwingine, chini ya hali fulani, flora wakaazi wa bakteria wanaweza kutenda kama pathojeni na kusababisha magonjwa halisi. Bakteria wanaweza kusababisha magonjwa kwa kuzalisha dutu zenye madhara (sumu), kuvamia tishu au kufanya yote mawili. Baadhi ya bakteria wanaweza kusababisha uvimbe ambao unaweza kuathiri vibaya moyo, mapafu, mfumo wa neva, figo au njia ya utumbo. Baadhi ya bakteria (kama vile Helicobacter pylori) huongeza hatari ya saratani.

Bakteria fulani wana uwezo wa kutumika kama silaha za kibiolojia. Bakteria hawa ni pamoja na wale wanaosababisha kimeta, ubotuli, tauni, na tularemia.

Uainishaji wa Bakteria

Bakteria wanaweza kuainishwa kwa njia kadhaa:

  • Majina ya kisayansi: Bakteria, kama viumbe hai wengine, wanaainishwa kulingana na jenasi (kulingana na kuwa na sifa moja au kadhaa zinazofanana) na ndani ya jenasi, kulingana na spishi. Jina lao la kisayansi ni jenasi ikifuatiwa na spishi (kwa mfano, Clostridium botulinum). Ndani ya spishi, kunaweza kuwa na aina tofauti, zinazoitwa uzao. Uzao hutofautiana katika muundo wa kijenetiki na vijenzi vya kemikali. Wakati mwingine dawa na chanjo fulani zinafanya kazi dhidi ya uzao fulani pekee.

  • Kutia Rangi: Bakteria wanaweza kuainishwa kulingana na rangi wanayobadilika kuwa baada ya kupakwa kemikali fulani (madoa) ili kuwaandaa kuchunguzwa na kutambuliwa kwa hadubini. Kupaka rangi kwa gramu ni mchakato unaotumika sana wa kupaka rangi. Baadhi ya bakteria hubadilika rangi na kuwa wa bluu. Wanaitwa bakteria wa gram-chanya. Wengine huwa na rangi nyekundu. Wanaitwa bakteria hasi wa gramu. Bakteria wa gram-chanya na gram-hasi hubadilika rangi kwa njia tofauti kwa sababu kuta za seli zao ni tofauti. Pia husababisha aina tofauti za maambukizi, na aina tofauti za dawa za kuua bakteria hupata ufanisi dhidi yake. Kuna alama nyingine nyingi za rangi kando na alama ya Gramu.

  • Maumbo: Bakteria wote wanaweza kuainishwa kama wa mojawapo ya maumbo matatu ya msingi: tufe (cocci), fimbo (bacilli), na wa mzunguko au mzingo (spiroketi).

  • Hitaji la oksijeni: Bakteria pia huainishwa kulingana na kama wanahitaji oksijeni ili kuishi na kukua. Wale wanaohitaji oksijeni huitwa aerobi. Wale ambao hawahitaji oksijeni na wanaopata shida kuishi au kukua oksijeni inapokuwepo wanaitwa anaerobi. Baadhi ya bakteria, wanaoitwa bakteria wa kifakti, wanaweza kuishi na kukua oksijeni inapokuwepo au kutokuwepo.

  • Muundo wa kijenetiki: Vipimo maalum vinaweza kubaini tofauti katika muundo wa kijenetiki (aina ya jeni) wa bakteria.

Jinsi Bakteria Anavyojibadilisha

Kwa kawaida mwili huwa na spishi mia kadhaa tofauti za bakteria lakini trilioni nyingi za bakteria binafsi.

Wengi wa bakteria hawa huishi (inayoitwa kutwaa) katika sehemu zifuatazo:

  • Kwenye ngozi na meno

  • Katika nafasi kati ya meno na fizi

  • Katika utando wa kamasi unaozunguka pua na njia za pua, koo, utumbo na uke

Spishi hutofautiana katika kila eneo, hivyo kuonyesha mazingira tofauti katika kila eneo.

Wengi wao ni anaerobi—yaani, hawahitaji oksijeni ili kuishi na kukua.

Kwa kawaida, anaerobi hawa hawasababishi magonjwa. Wengi wana kazi muhimu, kama vile kusaidia kusaga chakula kwenye utumbo.

Hata hivyo, bakteria wa anaerobi anaweza kusababisha magonjwa ikiwa utando wa kamasi umeharibika. Hilo linapotokea, bakteria wanaweza kuingia kwenye tishu ambazo kwa kawaida hawafai kuwepo na ambazo hazina kinga dhidi yao. Bakteria hao wanaweza kuambukiza sehemu zilizo karibu (kama vile sinasi, sikio la kati, mapafu, ubongo, tumbo, fupanyonga na ngozi) au kuingia kwenye mtiririko wa damu na kuenea.

Maambukizi ya Bakteria

Madaktari huainisha maambukizi ya bakteria kulingana na njia mbalimbali wanazotumia kuainisha bakteria. Kwa mfano, maambukizi yanaweza kuainishwa kama yanayosababishwa na bakteria wa gram-hasi au wa gram-chanya. Tofauti hii ni muhimu kwa sababu matibabu ya aina hizo mbili yanaweza kuhitaji aina tofauti za dawa za kuua bakteria.

Maambukizi hasi ya gramu ni pamoja na yafuatayo:

Maambukizi ya gram-chanya yanajumuisha yafuatayo:

Baadhi ya maambukizi huainishwa kulingana na umbo la bakteria. Kwa mfano, maambukizi yanayosababishwa na spiroketi (bakteria wenye umbo la mzunguko) huainishwa kama maambukizi ya spiroketi.

Maambukizi ya Spiroketi yanajumuisha yafuatayo:

Maambukizi mengine yanaweza kuainishwa kulingana na iwapo bakteria wanaoyasababisha wanahitaji oksijeni au wanastawi katika mazingira yasiyo na oksijeni. Bakteria wanaohitaji oksijeni kuishi na kukua huitwa aerobi. Bakteria ambao hawahitaji oksijeni kuishi na kukua huitwa anaerobie.

Maambukizi ya anaerobi ni pamoja na yafuatayo:

Kuna aina nyingi ya dawa za kuua bakteria kwa ajili ya kutibu maambukizi ya bakteria. Hata hivyo, uwezo wa bakteria kustahimili dawa za kuua bakteria unaongezeka na ni jambo linalotia wasiwasi mkubwa.

Ulinzi wa Bakteria

Bakteria wana njia nyingi za kujilinda.

Uliombo wa Kinga

Baadhi ya bakteria hutoa dutu inayowasaidia kujiambatisha kwenye bakteria, seli au vitu vingine. Dutu hii huchanganyika na bakteria na kuunda safu inayonata inayoitwa uliombo wa kinga. Kwa mfano, bakteria fulani huunda uliombo wa kinga kwenye meno (unaoitwa utando wa meno). Uliombo wa kinga hunasa chembe za chakula, ambazo bakteria husindika na kutumia, na katika mchakato huu, yamkini husababisha kuoza jino. Biofilamu pia husaidia kulinda bakteria dhidi ya dawa za kuua bakteria kwa kuwafanya kuwa wagumu kuuawa, kama vile bakteria wanaosababisha maambukizi kwenye viungo bandia na vali za moyo.

Kapsuli

Baadhi ya bakteria huzungushiwa na kukaa ndani ya kapsuli ya kinga. Kapsuli hii husaidia kuzuia seli nyeupe za damu, ambazo hupigana na maambukizi, kumeza bakteria. Bakteria hao wanafafanuliwa kama waliofunikwa kwa kapsuli.

Utando wa nje

Chini ya kipsuli, bakteria wa gram-hasi wana utando wa nje ambao huwalinda dhidi ya dawa fulani za kuua bakteria. Utando huu unapovurugika, huachilia dutu zenye sumu zinazoitwa endotoksini. Uwepo wa endotoxin huchangia ukali wa dalili wakati wa maambukizi ya bakteria hasi wa gramu.

Vijibofu

Baadhi ya bakteria hutoa vijibofu, ambavyo ni aina isiyofanya kazi (iliyolala) ya bakteria. Vijibofu vinaweza kuwezesha bakteria kuishi wakati hali za mazingira ni ngumu (kama vile kuwa kavu sana au ukosefu wa virutubisho). Wakati hali ni nzuri, kila kijibofu huota na kuwa bakteria hai.

Flajella

Flajella ni nyuzi ndefu na nyembamba zinazotoka kwenye uso wa seli wa bakteria na kuwezesha bakteria kusonga. Bakteria wasio na flajella hawawezi kujisogeza wenyewe.

Kustahamili dawa za kuua bakteria

Kwa asili baadhi ya bakteria hawaathiriwi na dawa fulani za kuua baakteria.

Bakteria wengine hukuza uwezo wa kustahimili dawa kwa sababu hupata jeni kutoka kwa bakteria ambao wamekuwa na uwezo wa kustahimili dawa au kwa sababu jeni zao hubadilika. Kwa mfano, pindi tu baada ya dawa ya penicillin kuanza kutumika katikati ya miaka ya 1940, bakteria wachache wa Staphylococcus aureus walipata jeni zilizofanya penicillin isiweze kufanya kazi dhidi yao. Aina zilizokuwa na jeni hizi maalum zilikuwa na uwezo wa kuishi wakati penicillin ilitumika kwa kawaida kutibu maambukizi. Aina za Staphylococcus aureus ambazo hazikuwa na jeni hizi mpya ziliuliwa na penicillin, na kuruhusu bakteria waliobaki wanaostahimili penicillin kuzaana na baada ya muda kuwa wa kawaida zaidi.

Kisha wanakemia walibadilisha molekuli ya penicillin, na kutengeneza dawa tofauti lakini inayofanana, methicillin, ambayo inaweza kuua bakteria wanaostahimili penicillin. Muda mfupi baada ya methicillin kuanza kutumika, aina za Staphylococcus aureus zilitengeneza jeni zilizozifanya kuweza kustahimili methicillin na dawa zinazohusiana. Aina hizi huitwa Staphylococcus aureus zinazostahimili methicillin (MRSA).

Jeni zinazosababisha uwezo wa kustahimili dawa zinaweza kupitishwa kwa vizazi vinavyofuata vya bakteria au wakati mwingine hata kwa spishi nyingine za bakteria.

Jinsi dawa za kuua bakteria zinapotumika kila mara, ndivyo uwezekano wa bakteria sugu unavyoongezeka. Kwa hivyo, wataalamu wanapendekeza kwamba madaktari waagize matumizi ya dawa za kuua baktera pale tu inapobidi na kwa muda mfupi iwezekanavyo. Hasa, madaktari wanapaswa kuagiza matumizi ya dawa za bakteria kwa maambukizi yanayoendelea yaliyosababishwa na bakteria pekee, na si kutibu kutwaliwa. Dawa za kuua bakteria pia hazipaswi kuagizwa ili kutibu maambukizi yanayosababishwa na virusi, kama vile mafua au homa. Kuwapa dawa za kuua bakteria watu ambao yamkini hawana maambukizi ya bakteria, kama vile walio na dalili za kikohozi na mafua, hakufanyi watu kupata nafuu ila husaidia kuunda bakteria wanaostahimili dawa na kuhatarisha kutokea kwa madhara kama vile athari za mzio na kuhara. Kwa sababu dawa za kuua bakteria zimetumika sana (na kutumika vibaya), bakteria wengi wamekuwa na uwezo wa kustahimili dawa mbalimbali za kuua bakteria, huku dawa chache mpya za kuua bakteria zikipatikana.

Bakteria sugu wanaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine. Kwa sababu usafiri wa kimataifa ni wa kawaida sana, bakteria wanaostahimili dawa wanaweza kuenea kwenda sehemu nyingi za ulimwengu ndani ya muda mfupi. Kuenea kwa bakteria hawa hospitalini ni jambo linalotia wasiwasi sana. Bakteria wanaostahimili dawa ni wa kawaida mahospitalini kwa sababu dawa za kuua bakteria huhitajika mara nyingi na kwa sababu wafanyakazi wa hospitali na wageni wanaweza kueneza bakteria ikiwa hawafuati kabisa taratibu zinazofaa za usafi. Pia, wagonjwa wengi wanaolazwa hospitalini wana mfumo dhaifu wa kinga, na hivyo kuwafanya wawe katika hatari zaidi ya kuambukizwa.

Bakteria wanaostahimili dawa pia wanaweza kuenea kwa watu kutoka kwa wanyama. Bakteria wanaostahimili dawa ni wa kawaida miongoni mwa wanyama wa shambani kwa sababu mara nyingi dawa za kuua bakteria hutolewa mara kwa mara kwa wanyama wenye afya njema ili kuzuia maambukizi ambayo yanaweza kuathiri ukuaji au kusababisha magonjwa. Nchi nyingi zimepiga marufuku matumizi ya dawa za kuua bakteria kwa wanyama ili kupunguza hatari ya yafuatayo:

  • Kula bakteria wanaostahimili dawa katika bidhaa za chakula za wanyama

  • Kuambukizwa bakteria wanaostahimili dawa kwa kugusana na wanyama

  • Kuathiriwa na dawa za kuua bakteria zilizo katika bidhaa za chakula za wanyama