Klebsiella, Enterobacter, na Serratia ni bakteria hasi kwa gramu zinazohusiana kwa karibu ambazo wakati mwingine huambukiza njia ya mkojo au njia ya upumuaji ya watu hospitalini au katika vituo vya utunzaji wa muda mrefu.
Bakteria hizi zinaweza kuambukiza njia ya mkojo au njia ya upumuaji, katheta za ndani ya mshipa zinazotumika kutoa dawa au majimaji, majeraha ya kuungua, majeraha yanayotokana na upasuaji, au mzunguko wa damu.
Kutambua bakteria katika sampuli iliyochukuliwa kutoka kwenye damu au kutoka kwa tishu zilizoambukizwa huthibitisha utambuzi wa ugonjwa.
Maambukizi yanayosababishwa na bakteria zote tatu hutibiwa kwa antibayotiki ziinazotolewa kupitia mshipa (ndani ya mshipa).
(Angalia pia Muhtasari wa Bakteria.)
Klebsiella, Enterobacter, na Serratia bakteria huishi kwenye utumbo wa watu wengi wenye afya njema na mara chache husababisha maambukizi kwao. Maambukizi yanayosababishwa na bakteria hawa mara nyingi huambukizwa katika hospitali na vituo vya utunzaji wa muda mrefu. Kwa kawaida hutokea kwa watu ambao upinzani wao dhidi ya maambukizi umedhoofika na/au ambao wana kifaa cha matibabu (kama vile katheta, mifereji ya maji, na mirija ya hewa) mwilini mwao.
Bakteria hizi zinaweza kuambukiza sehemu mbalimbali za mwili:
Njia ya mkojo au njia ya upumuaji (inayosababisha nimonia, maambukizi ya kibofu cha mkojo, au maambukizi ya figo)
Katheta zinazoingizwa kwenye mshipa (katheta ya intravenasi), hutumika kuingiza dawa au vimiminika
Majeraha yaliyosababishwa wakati wa upasuaji
Mkondo wa damu (unaosababisha bakteremia au sepsis)
Mara chache, bakteria za Klebsiella husababisha nimonia kwa watu wanaoishi nje ya kituo cha huduma ya afya (katika jamii), kwa kawaida kwa watu wenye tatizo la matumizi ya pombe, wazee, watu wenye kisukari, au watu wenye mfumo dhaifu wa kinga mwilini. Kwa kawaida, maambukizi haya makali husababisha kikohozi kinachotoa makohozi yanayonata yenye rangi ya kahawia iliyokolea au nyekundu iliyokolea, na mikusanyiko ya usaha (majipu) kwenye mapafu au kwenye utando kati ya mapafu na ukuta wa kifua (empyema).
Aina moja ya Klebsiella hutoa sumu ambayo inaweza kusababisha kuvimba kwa utumbo mpana na kutokwa na damu (kolitisi ya kutokwa na damu [hemorrhagic colitis]) baada ya kutumia antibayotiki. Ugonjwa huu huitwa koliti inayohusiana na antibayotiki. Antibayotiki huua bakteria ambazo kwa kawaida hukaa ndani ya utumbo. Kisha Klebsiella bakteria zinaweza kuongezeka na kuzalisha sumu hiyo. Hata hivyo, ugonjwa wa kolitis unaohusishwa na antibayotiki kwa kawaida husababishwa na sumu zinazozalishwa na Clostridioides difficile.
Utambuzi wa Maambukizi ya Klebsiella, Enterobacter, na Serratia
Uchunguzi na ukuzaji wa sampuli ya tishu iliyoambukizwa
Madaktari wanashuku mojawapo ya maambukizi haya kwa watu walio katika hatari kubwa ya kuambukizwa, kama vile watu wanaoishi katika kituo cha utunzaji wa muda mrefu au mahali ambako kuna au kulikuwa na mlipuko.
Ili kuthibitisha utambuzi, madaktari huchukua sampuli ya makohozi, ute wa mapafu (unaopatikana kupitia bronkoskopu), damu, mkojo, au tishu zilizoambukizwa. Sampuli imetiwa doa la Gram, imepandwa, na kuchunguzwa chini ya darubini. Bakteria hizi zinaweza kutambuliwa kwa urahisi.
Vipimo vingine hutegemea aina ya maambukizi. Huenda zikajumuisha vipimo vya upigaji picha, kama vile vipimo vya ultrasound, eksirei, na skani za tomografia ya kompyuta (CT).
Bakteria zinazotambuliwa katika sampuli hupimwa ili kubaini ni antibayotiki vipi vinavyoweza kuwa na ufanisi (mchakato unaoitwa upimaji wa usikivu).
Matibabu ya Maambukizi ya Klebsiella, Enterobacter, na Serratia
Antibayotiki zinazotolewa kwa njia ya mshipa (kupitia mishipa)
Maambukizi yanayosababishwa na bakteria yoyote kati ya hizi 3 hutibiwa kwa antibayotiki vinavyotolewa kwa njia ya mishipa.
Antibayotiki zinajumuisha cephalosporins, cefepime, carbapenems, fluoroquinolones, piperacillin/tazobactam, au aminoglycosides. Hata hivyo, wakati mwingine bakteria hzi huwa sugu kwa antibayotiki nyingi, kwa hivyo madaktari hufanya vipimo vya usikivu wa antibayotiki.
Ikiwa maambukizi ya bakteria yoyote kati ya hizi 3 yakipatikana katika kituo cha huduma ya afya, maambukizi yanaweza kuwa magumu kutibu kwa sababu bakteria zinazopatikana katika vituo hivyo kwa kawaida huwa sugu kwa antibayotiki nyingi.