Usalama wa Dawa Wakati wa Ujauzito

NaRavindu Gunatilake, MD, Valley Perinatal Services;
Avinash S. Patil, MD, University of Arizona College of Medicine
Imekaguliwa naOluwatosin Goje, MD, MSCR, Cleveland Clinic, Lerner College of Medicine of Case Western Reserve University
Imepitiwa/Imerekebishwa Nov 2023 | Imebadilishwa Jul 2024
v809905_sw

Wakati wa ujauzito, wanawake wanaweza kuhitaji kutumia dawa ili kutibu hali ya kiafya iliyopo au mpya. Pia, vitamini fulani vinapendekezwa wakati wa ujauzito. Kabala ya kutumia dawa yoyote (ikiwa ni pamoja na dawa za kununua dukani) au Virutubisho lishe (ikwia ni pamoja na dawa za mitishamba), mwanamke mjamzito anapaswa kushauriana na daktari. Wanawake ambao sasa wanatumia dawa na wanapanga kuwa wajawazito wanapaswa kushauriana na daktari kabla ya kubeba ujauzito, ikiwa inawezekana, ili kuona endapo dawa hizo zinapaswa kusitishwa au kubadilishwa. (Angalia pia Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa: Dawa na Ujauzito.)

Dawa au dutu nyinginezo zinazotumiwa na mwanamke mjamzito zinaweza kufikia kihusi kwa kupitia kwenye plasenta, njia ileile inayotumiwa na oksjeni na virutubishi, ambavyo vinahitajika kwa ajili ya ukuaji na maendeleo ya kijusi. Hata hivyo, zile ambazo hazipiti kwenye plasenta bado zinaweza kudhuru kijusi kwa kuathiri uterasi na plasenta.

Dawa au dutu nyinginezo ambazo mwanamke mjamzito anatumia wakati wa ujauzito zinaweza kuathiri kijusi kwa njia mbalimbali:

  • Hakuna madhara kwenye kijusi na ukuaji wake

  • Inafikia kijusi moja kwa moja, na kusababisha madhara, ukuaji usio wa kawaida (na kusababisha kasoro za kuzaliwa), au kifo

  • Kubadilisha shughuli za plasenta, kwa kawaida kwa kusababisha mishipa ya damu kuwa miembamba (kunywea) na hivyo kupunguza usambazaji wa oksijeni na virutubishi kutoka kwa mama (wakati mwingine kusababisha mtoto kuwa na uzito wa chini na asikue vizuri)

  • Husababisha misuli ya kijusi kukaza kwa nguvu, na kujeruhi kijusi isivyo moja kwa moja kwa kupunguza mzunguko wake wa damu au kuchochea uchungu wa uzazi kabla ya wakati na kujifungua

  • Huathiri kijusi isivyo moja kwa moja (kwa mfano, dawa ambazo zinashusha shinikizo la damu la mama zinaweza kupunguza mtiririko wa damu kwenye plasenta na hivyo kupunguza usambazaji wa oksijeni na virutubishi kwenye kijusi)

Baadhi ya dawa zinabaki mwilini zinaweza kuwa na madhara baada ya kusistishwa. Kwa mfano, isotretinoin, dawa inayotumika kutibu matatizo ya ngozi inahifadhiwa kwenye mafuta chini ya ngozi na huachiliwa taratibu kwa baada ya wiki kadhaa. Isotretinoin inaweza kusababisha kasoro za kuzaliwa ikiwa mwanamke atakuwa mjamzito ndani ya wiki 2 baada ya kuacha kutumia dawa hizo. Kwa hivyo, wanawake wanashuariwa kusubiri hadi angalau wiki 3 hadi 4 baada ya dawa kuacha kutumika kabla hawajawa wajawazito.

Jinsi Dawa Zinavyopenya Kondo

Baadhi ya mishipa ya damu ya kijusi huwekwa katika mwonekano mdogo kama wa nywele (vili) au placenta ambayo inaenda hadi kwenye ukuta wa mji wa mimba. Damu ya mama inapita kwenye sehemu inayozunguka vili (nafasi ya kati ya vili). Ni utando mwembamba pekee (utando wa plasenta) ndio unaweza kutenganisha damu ya mama na nafasi ya kati ya vili kutoka kwenye damu ya kijusi kwenye vili. Dawa katika damu ya mama inaweza kuvuka utando huu na kuingia kwenye mishipa ya damu kwenye vili na kupita kwenye kitovu hadi kwenye kijusi.

Jinsi dawa inavyoathiri kijusu hutegemea

  • Hatua ya ukuaji wa kijusi

  • Nguvu na dozi ya dawa

  • Hali ya kuweza kupenya kwenye plasenta (ni rahisi kiasi gani vitu vinapita)

  • Sababu za kijeni kwa mwanamke mjamzito, ambayo inaathiri kiasi gani cha dawa ni amilifu na kinapatikana

  • Afya ya mwanamke mjamzito (kwa mfano, kichefuchefu na kutapika kunaweza kupunguza unyonyaji wa dawa zinazotumika kwa mdomo)

Jedwali
Jedwali

Mashirika ya serikali yanayosimamia usalama wa dawa yanaweza kuainisha dawa kulingana na uelewa wa sasa kuhusu usalama wakati wa ujauzito. Nchini Marekani, Mamalaka ya Chakula na Dawa (FDA) hutoa taarifa kuhusu usalama wa dawa kwenye ujauzito (angalia FDA: Dawa na Ujauzito). Uelewa kuhusu usalama wa dawa kwenye ujauzito unatokana na utafiti kuhusu watu na wanyama na kuhusu madhara ambayo yameripotiwa na watu ambao wametumia hiyo dawa. Kwa ujumla, madaktari wanawashauri wanawake wajawazito kuhusu kutumia dawa kulingana na utafiti uliopo, umuhimu wa dawa kwenye afya ya mwanamke mjamzito, na endapo kuna matibabu mengine ambayo yana hatari kidogo kwa mwanamke mjamzito au kijusi. Dawa zinatolewa kwenye ujauzito ikiwa manufaa yanazidi hatari.

Jedwali
Jedwali

Chanjo Wakati wa Ujauzito

Chanjo ni yenye ufanisi sawa kwa wanawake wajawazito kama ilivyo kwa wale wasiokuwa wajawazito. (Angalia pia Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC): Ujauzito na Chanjo.)

Chanjo zilizotengenezwa kwa virusi hai (kama vile chanjo ya rubela na chanjo ya tetekuwangava) hazitolewi kwa wanawake ambao ni wajawazito au wanaweza kuwa wajawazito.

Chanjo nyingine (kama zile za kolera, kipindupindu, homa ya ini A, homa ya ini B, tauni, kichaa cha mbwa, nahoma ya matumbo) hutolewa kwa wanawake wajawazito tu ikiwa wako katika hatari kubwa ya kupata maambukizi hayo na ikiwa hatari ya madhara yanayoweza kutokana na chanjo ni ndogo.

Baadhi ya chanjo ambazo zinachukuliwa kuwa salama kwa wanawake wajawazito na zinapendekezwa wakati wa ujauzito ni pamoja na

Ushahidi unaonyesha kuwa faida za chanjo ya COVID-19 wakati wa ujauzito zinazidi hatari yoyote inayojulikana au inayoweza kutokea. Data hizi zinaonyesha kwamba manufaa ya kupokea chanjo ya Chanjo ya COVID-19 ni makubwa kuliko hatari zozote zinazojulikana au zinazoweza kutokea za kuchanja wakati wa ujauzito. (Angalia pia CDC: Chanjo za COVID-19 Ukiwa Mjamzito au Unanyonyesha.)

Mnamo Agosti 2023, Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Marekani (FDA) iliridhia matumizi ya chanjo ya virusi vya mapafu (RSV) liidhinisha matumizi ya chanjo ya virusi vya mapafu (RSV) kwa wanawake wajawazito walioko kati ya wiki 32 hadi 36 za ujauzito, ikiwa na onyo la kuepuka matumizi kabla ya wiki 32. (angalia FDA Imeidhinisha Chanjo ya Kwanza kwa Wanawake Wajawazito ili Kuzuia RSV kwa Watoto Wachanga).

Dawa Zilizotumiwa Kutibu Matatizo ya Moyo na Mshipa wa Damu Wakati wa Ujauzito

Dawa za kupunguza shinikizo la damu (antihypertensives) zinaweza kuhitajika kwa wanawake wajawazito ambao walikuwa na shinikizo la juu la damu kabla ya ujauzito au ambao wanapata shinikizo hilo wakati wa ujauzito. Aina yoyote ya shinikizo la juu la damu huongeza hatari ya matatizo kwa mwanamke huyo (kama vile shinikizo la damu la juu wakati wa ujauzito) na kwa kijusi (angalia Shinikizo la Juu la Damu Wakati wa Ujauzito). Hata hivyo, dawa ya kupunguza shinikizo la damu inaweza kupunguza mtiririko wa damu kwenye plaseta ikiwa zinapunguza shinikizo la damu kwa haraka sana kwa wanawake wajawazito. Wanawake wajawazito ambao wanapaswa kutumia dawa hizi wanafuatiliwa kwa ukaribu.

Aina kadhaa za dawa ya kupunguza shinikizo la damu, kama vile vizuizi vya enzaimu ya kugeuza angiotensin na dawa za thiazide za kudhibiti ongezeko la mkojo, kwa kawaida hawapewi wanawake wajawazito. Dawa hizi zinaweza kusababisha matatizo makubwa kwenye kijusi, kama vile kuharibu figo, ukuaji usitosheleza kabla ya kuzaliwa (kizuizi cha ukuaji), na kasoro za kuzaliwa. Spironolactone pia haitolewi kwa wanawake wajawazito.. Dawa hii inaweza kusababisha kuonekana kwa sifa za kike (feminization) katika kijusi wa kiume.

Digoxin, inatumika kutibu moyo kushindwa kufanya kazi na baadhi ya mapigo ya mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida, inapita kwa urahisi kuvuka plasenta. Lakini kwa dozi za kawaida, digoxin kwa kawaida ina athari ndogo kwa mtoto kabla au baada ya kuzaliwa.

Dawa za Kuzuia Mfadhaiko Wakati wa Ujauzito

Unyogovu wa kitabibu ni wa kawaida wakati wa ujauzito; kwa hivyo, dawa za kupunguza unyogovu (antidepressants), hasa baadhi ya vizuizi maalum vya urejeleaji wa serotonin (SSRI) kama sertraline, hutumika mara kwa mara wakati wa ujauzito. Kwa wanawake wajawazito, manufaa ya kutibu unyongovu kwa kawaida yanazidi hatari.

Paroxetine inaonekana kuongeza hatari ya kasoro za kuzaliwa. Kwa hivyo, ikiwa mwanamke mjamzito anatumia paroxetine, ekokadiografia inapaswa kufanywa ili kuinua moyo wa kijusi. Hata hivyo, SSRI zingine haziongezi hatari hii.

Ikiwa mwanamke mjamzito anatumia dawa za kuzuia unyongovu, mtoto mchanga anaweza kuwa na dalili za kuacha matumizi (kama vile harara na kutetemeka) baada ya kujifungua. Ili kuzuia dalili hizi, madaktari wanaweza kupunguza kipimo cha dawa ya kupunguza unyogovu kwa taratibu wakati wa kipindi cha tatu na kusitisha dawa kabla ya mtoto kuzaliwa. Hata hivyo, ikiwa mwanamke ana dalili kubwa za unyogovu au dalili zinaongezeka wakati kipimo kinapopunguzwa, dawa za kupunguza unyogovu zinapaswa kuendelea kutumika. Unyogovu wakati wa ujauzito unaweza kusababisha unyogovu baada ya kujifungua, unaohusisha mabadiliko makubwa ya hisia na unahitaji matibabu.

Dawa za Kuua Virusi Wakati wa Ujauzito

Baadhi ya dawa za kuzuia virusi, kama zidovudine na ritonavir kwa maambukizi ya VVU, zimetumika kwa usalama kwa wanawake wajawazito kwa miaka mingi. Hata hivyo, dawa fulani za kuzuia virusi zinaweza kusababisha matatizo kwa kijusi. Kwa mfano, uchunguzi fulani unaonyesha kuwa baadhi ya mchanganyiko wa dawa za VVU zinazotolewa katika kipindi cha kwanza zinaweza kuongeza hatari ya mdomo na kaakaa zilizopasuka.

Kwa mwanamke mjamzito mwenye COVID-19 ya mapema yenye dalili hafifu hadi za wastani, timu yake ya matibabu inaweza kujadili hatari na faida na kuamua ikiwa nirmatrelvir-ritonavir au remdesivir inafaa. Kwa wagonjwa wajawazito waliolazwa hospitalini kwa COVID-19, matumizi ya baricitinib au tocilizumab pia yanaweza kuzingatiwa. Kwa ujumla, wataalamu wanapendekeza kuwa wasiwasi wa dhana kuhusu usalama wa dawa za kuzuia virusi wakati wa ujauzito haupaswi kuzuia matumizi yao kwa wanawake wajawazito.

Iwapo mwanamke mjamzito atapata mafua (influenza), anapaswa kutafuta matibabu haraka iwezekanavyo, kwa sababu kutibu mafua ndani ya saa 48 tangu dalili kuanza kuna ufanisi zaidi. Hata hivyo, matibabu wakati wowote wa maambukizi huweza kupunguza hatari ya matatizo makubwa. Hakuna utafiti uliandaliwa vizuri kwa ajilili ya wanawake wajawazito kuhusu zanamivir na oseltamivir. Hata hivyo, tafiti nyingi zinazotegemea uchunguzi zinaonyesha kuwa kutibu wanawake wajawazito kwa zanamivir au oseltamivir hakuongezi hatari ya madhara. Kuna taarifa chache au hakuna kabisa kuhusu matumizi ya dawa nyingine za mafua wakati wa ujauzito.

Acyclovir, ikichukuliwa kwa mdomo au kutumika kwenye ngozi, kawaida kutumika kutibu virusi vya herpes simplex, inaonekana kuwa salama wakati wa ujauzito.

Dawa Zilizotumiwa Wakati wa Uchungu wa Uzazi na Kuzaa

Dawa zinazotumika kupunguza maumivu wakati wa ujauzito (kama vile nusukaputi ya sehemu maalumu na dawa za afyuni) kawaida husafiri kupitia kondo la nyuma (plasenta) na zinaweza kuathiri mtoto mchanga. Kwa mfano, zinaweza kupunguza haja ya mtoto mchanga ya kupumua. Kwa hivyo, ikiwa dawa hizi zinahitajika wakati wa kujifungua, hutolewa kwa dozi ndogo zaidi inayofaa.