Vipimo na Taratibu za Magonjwa ya Uzazi ya Wanawake

NaShubhangi Kesavan, MD, Cleveland Clinic Learner College of Medicine, Case Western Reserve University
Imekaguliwa naOluwatosin Goje, MD, MSCR, Cleveland Clinic, Lerner College of Medicine of Case Western Reserve University
Imepitiwa/Imerekebishwa Apr 2024 | Imebadilishwa Sept 2025
v1157291_sw

Wakati mwingine madaktari hupendekeza vipimo vya uchunguzi kama sehemu ya njia ya kuzuia, ambavyo ni vipimo vinavyofanywa ili kubaini matatizo kwa watu ambao hawana dalili. Ikiwa wanawake wana dalili zinazohusiana na mfumo wa uzazi (dalili za ugonjwa wa wanawake), vipimo vya kutambua tatizo linalosababisha (taratibu za uchunguzi) vinaweza kuhitajika kufanywa.

Vipimo muhimu vya uchunguzi kwa wanawake ni pamoja na

Upimaji wa Mimba

Wanawake walio katika umri wa kuzaa na wanajaribu kupata mimba, wana wasiwasi kuhusu ujauzito usiotarajiwa au wenye dalili za ugonjwa wa wanawake wanaweza kuomba kupimwa ujauzito au daktari anaweza kupendekeza kipimo cha ujauzito. Madaktari huchukua sampuli ya mkojo au wakati mwingine damu na kuipima ili kubaini iwapo mwanamke ni mjamzito.

Usahihi wa vipimo vya ujauzito vya mkojo nyumbani unaweza kutofautiana kulingana na kifaa maalum cha kupima, mbinu na tafsiri. Kwa hivyo, kipimo chochote cha ujauzito nyumbani kinapaswa kuthibitishwa kwa kutumia mkojo kwenye maabara au kipimo cha damu.

Vipimo Vingine vya Maabara

Madaktari wanaweza kufanya vipimo vingine vya damu ili kutathmini matatizo au ugonjwa wa wanawake, ikiwa ni pamoja na

Zaidi ya hayo, wakati mwingine sampuli ya mkojo huchukuliwa ili kupima maambukizi ya njia ya mkojo, maambukizi ya zinaa au matatizo kwenye kibofu au figo.

Upimaji wa Maambukizi ya Magonjwa ya Uzazi ya Wanawake

Upimaji wa ugonjwa wa uke

Kwa wanawake wanaotokwa na uchafu ukeni kwa hali isiyo ya kawaida, madaktari wanaweza kuchukua sampuli ya uchafu huo ili kupima matatizo ya uke kuwa chungu, ambayo inaweza kusababishwa na bacterial vaginosis, maambukizi ya chachu au maambukizi ya trikomonasi. Baadhi ya matokeo ya vipimo yanapatikana papo hapo na mengine huchukua siku chache.

Upimaji wa maambukizi ya zinaa

Wanawake walio katika hatari ya maambukizo ya zinaa (STI) wanapaswa kuchunguzwa ugonjwa huu, hata ikiwa hawana dalili.

Wanawake wanapaswa kupimwa ugonjwa wa zinaa (STI) mara kwa mara, kulingana na hatari. Kipimo kinapaswa kufanywa kila mwaka kwa kisonono na klamidia kwa wanawake ambao

  • Wanashiriki ngono na wana umri wa miaka 25 au chini

  • Wanashiriki ngono na wana umri wa zaidi ya miaka 25 ikiwa kuna hatari kubwa (kama vile mwenzi mpya au wengi wa ngono, mwanamke au mwenzi wake ana zaidi ya mpenzi mmoja au amewahi kupata ugonjwa wa zinaa (STI))

  • Ujauzito

Kupima angalau mara moja katika maisha ya mwanamke kwa virusi vya UKIMWI na homa ya ini C (au mara nyingi zaidi ikiwa mwanamke yuko katika hatari kubwa) pia kunapendekezwa.

Wanawake wajawazito wanapaswa kupimwa VVU, homa ya ini B na kaswende.

Wanawake walio katika hatari kubwa, wenye dalili au wanaoomba kupimwa wanapaswa pia kupimwa ugonjwa wa zinaa (STI). Kipimo cha ugonjwa wa zinaa (STI) hufanywa kwa kutumia aina tofauti za vipimo, kulingana na maambukizi.

Ugonjwa wa zinaa (STI) unaopimwa kwa kutumia sampuli za uke, mlango wa kizazi au mkojo ni

Kwa ugonjwa huu mwingi wa zinaa (STI), daktari hutumia sifongo ili kutoa sampuli ndogo kutoka kwenye mlango wa kizazi. Sampuli hutumwa kwenye maabara ili ichunguzwe. Kipimo cha kisonono na klamidia unaweza pia kufanywa kwa kutumia sampuli ya mkojo au sampuli kutoka ukeni (ambayo inaweza kuchukuliwa na daktari au na mwanamke mwenyewe).

Ugonjwa wa zinaa (STI) unaopimwa kwa kutumia vipimo vya damu ni:

Kipimo cha ugonjwa wa zinaa (STI) ni sehemu muhimu ya utunzaji wa kinga, kwa sababu ugonjwa wa zinaa usiotibiwa unaweza kusababisha matatizo makubwa (kama vile, utasa, ugonjwa mkali wa ini, mfumo wa neva au mfumo wa kingamaradhi au kansa).

Ingawa HPV ni ugonjwa wa zinaa (STI), kwa kawaida kipimo cha HPV hufanywa kama sehemu ya uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi, peke yake au pamoja na kipimo cha Pap, si kama kipimo cha ugonjwa wa zinaa (STI). HPV inaweza kusababisha chunjua za sehemu za siri na kuongeza hatari ya saratani ya mlango wa kizazi. Chunjua za sehemu za siri hutambuliwa na madaktari wakati wa uchunguzi wa fupanyonga, kulingana na mwonekano wake. Wakati mwingine, ikiwa utambuzi hauna uhakika, bayopsi inahitajika.

Upimaji wa Saratani ya Mlango wa Kizazi

Uchunguzi wa Saratani ya Mlango wa Kizazi

Vipimo vinavyotumika kuchunguza saratani ya mlango wa kizazi vinajumuisha vifuatayvo:

  • Kipimo cha Papanicolaou (Pap): Seli kutoka kwenye mlango wa kizazi huchunguzwa kwa kutumia hadubini ili kubaini ikiwa kuna seli zozote za kansa au zisizo za kawaida na zinaweza, bila matibabu, kuwa kansa (seli zinazotangulia kansa).

  • Kipimo cha Virusi vya Papiloma vya Binadamu (HPV): Sampuli kutoka kwenye mlango wa kizazi hupimwa ili kubaini ikiwa kuna HPV. HPV inaweza kusababisha saratani ya mlango wa kizazi.

Katika kipimo cha Pap na cha HPV, madaktari hutoa sampuli kutoka kwenye mlango wa kizazi. Madaktari hukusanya sampuli kwa kuingiza spekulamu (kifaa cha chuma au plastiki) kwenye uke ili kufungua kuta za uke. Kisha hutumia brashi ya plastiki kuondoa baadhi ya seli kutoka kwenye sehemu ya mbele ya mlango wa kizazi na kutoka katika njia inayopitia kwenye mlango wa kizazi (mfereji wa mlango wa kizazi). Sampuli hutumwa kwenye maabara, ambapo huchunguzwa kwa kutumia hadubini ili kutafuta seli zisizo za kawaida. Seli zisizo za kawaida zinaweza kuonyesha mabadiliko ya kabla ya kansa au mara chache, saratani ya mlango wa kizazi.

Kipimo cha Maabara

Kwa kawaida, kufanyiwa kipimo cha Pap huhisi kama kuna mikwaruzo au maumivu, lakini si chungu na huchukua sekunde chache tu.

Vipimo vya Pap hutambua saratani nyingi za mlango wa kizazi, hata saratani ya hatua za mwanzo kabisa. Pia wanaweza kugundua mabadiliko ya kabla ya kansa katika seli za mlango wa kizazi. Mabadiliko haya, yanayoitwa neoplasia ya ndani ya epitheliali ya mlango wa kizazi (CIN), yanaweza kutibiwa, hivyo kusaidia kuzuia kansa kuendelea na kuenea.

Vipimo vya Pap ni sahihi zaidi ikiwa mwanamke hataoga au kutumia malai za ukeni au bidhaa nyingine kwa angalau saa 24 kabla ya kipimo.

Wataalamu wanapendekeza kwamba kipimo cha kwanza cha Pap kifanyike kwa wanawake wengi baada ya umri wa miaka 21.

Mara ambazo kipimo kinahitajika inategemea zaidi umri wa mwanamke na matokeo ya vipimo vya awali vya Pap:

  • Chini ya umri wa miaka 21: Uchunguzi hauhitajiki

  • Kuanzia umri wa miaka 21 hadi 29: Kwa kawaida kipimo hufanywa kila baada ya miaka 3 kwa kutumia kipimo cha Pap pekee (vinginevyo, wagonjwa wa kawaida walio na umri wa miaka 25 au zaidi na walio katika hatari ya kupata HPV pekee wanaweza kuanza uchunguzi kwa kutumia kipimo cha awali cha HPV pekee kila baada ya miaka 5)

  • Kuanzia umri wa miaka 30 hadi 65: Kipimo hufanywa kila baada ya miaka 3 ikiwa kipimo cha Pap pekee kinafanywa, au kila baada ya miaka 5 ikiwa kipimo cha HPV pekee kinafanywa, au kila baada ya miaka 5 ikiwa kipimo cha Pap na kipimo cha HPV kinafanywa.

  • Baada ya umri wa miaka 65: Wanawake wengi hawahitaji tena kupimwa ikiwa hawajapata matokeo yasiyo ya kawaida ya kipimo katika miaka 10 iliyopita.

Wanawake walio na hatari kubwa ya kupata saratani ya mlango wa kizazi wanahitaji kupimwa mara kwa mara. Wanawake hao ni pamoja na wenye maambukizi ya VVU, ambao wana mfumo dhaifu wa kingamaradhi (ambao unaweza kusababishwa na kutumia dawa au kuwa na tatizo linalokandamiza mfumo wa kingamaradhi), au ambao wamepata matokeo yasiyo ya kawaida ya kipimo cha Pap.

Vipimo vya Pap kwa wanawake wazee vinaweza kuendelea ikiwa mwanamke ana mwenzi mpya wa ngono au ikiwa ana wenzi kadhaa wa ngono.

Wanawake ambao wameondolewa kabisa uterasi (histerektomia yote) na ambao hawajapata matokeo yasiyo ya kawaida ya kipimo cha Pap hawahitaji kuchunguzwa saratani ya mlango wa kizazi. Hata hivyo, ikiwa histerektomia haujafanywa (yaani, mlango wa kizazi haujaondolewa), uchunguzi unahitajika. (Mlango wa kizazi ni sehemu ya chini ya uterasi inayofunguka ndani ya uke.)

Matokeo yasiyo ya kawaida ya vipimo vya uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi yanahitaji tathmini zaidi.

Taratibu za uchunguzi na matibabu ya mlango wa kizazi

Kolposkopi

Kwa kolposkopi, spekalamu hutumiwa kushikilia kuta za uke na lenzi ya kukuza ya darubini (sawa na ile ya hadubini) hutumiwa kukagua mlango wa kizazi ikiwa kuna dalili za kansa. Mara nyingi, sampuli ya tishu huondolewa ili ichunguzwe kwa kutumia hadubini (bayopsi).

Kolposkopi mara nyingi hufanywa wakati

  • Vidonda kwenye mlango wa kizazi, uke au kuma vinahitaji kutathminiwa.

  • Matokeo ya kipimo cha Papanicolaou (Pap) si ya kawaida, ikiwa na au bila kipimo cha HPV.

  • Mwanamke amekamilisha matibabu ya saratani ya mlango wa kizazi.

Wanawake kwa kawaida huhisi usumbufu fulani wakati spekulamu inapoingizwa, lakini kolposcopia pekee (bila bayopsi) haina maumivu na hivyo haihitaji ganzi. Utaratibu wa bayopsi kwa kawaida huelezewa kama kusababisha hisia ya kuwasha au kufinya kwa kasi na pia hauhitaji ganzi. Kwa kawaida utaratibu huchukua dakika 10 hadi 15. Madoa machache ni ya kawaida baada ya utaratibu.

Kutoa sampuli za tishu za ndani za mlango wa kizazi

Utaratibu wa kutumia chombo cha madaktari cha kuchunia au kukwangulia kwenye utando wa mlango wa kizazi unahusisha kuingiza kifaa kidogo, chenye ncha kali, chenye umbo la kijiko (kisunzi) kwenye mlango wa kizazi (mfereji wa mlango wa kizazi) ili kutoa tishu. Kisunzi hutumika kukwaruza kiasi kidogo cha tishu kutoka juu ndani ya mfereji wa kizazi. Bayopsi ya mlango wa kizazi (kuondoa kipande kidogo cha tishu kutoka kwenye sehemu ya nje ya mlango wa kizazi) kwa kawaida hufanywa kwa wakati mmoja. Sampuli za tishu huchunguzwa na mwanapatholojia kwa kutumia hadubini.

Upasuaji wa ndani ya mlango wa kizazi hufanywa wakati

  • Saratani ya endometriamu au ya mlango wa kizazi inashukiwa au inahitaji kuondolewa.

Kwa kawaida, hufanywa wakati wa kolposkopi na haihitaji ganzi.

Utaratibu wa kuondoa tishu kwa kutumia umeme

Katika utaratibu wa kukata kwa kututmia umeme (LEEP), kitanzi chembamba cha waya kinachopitisha umeme hutumika kuondoa kipande cha tishu. Kwa kawaida, kipande hiki cha tishu ni kikubwa kuliko kile kinachopatikana katika bayopsi ya mlango wa kizazi.

Utaratibu huu unaweza kufanywa baada ya matokeo yasiyo ya kawaida ya kipimo cha Pap

  • Ili kutathmini hali isiyo ya kawaida kwa usahihi zaidi

  • Ili kuondoa tishu isiyo ya kawaida (na hivyo kutibu saratani ya mlango wa kizazikatika hatua za mwanzo)

LEEP inahitaji ganzi (mara nyingi ya ndani), huchukua takribani dakika 5 hadi 10, na inaweza kufanywa katika ofisi ya daktari. Baadaye, wanawake wanaweza kuhisi usumbufu mdogo hadi wa wastani na kutokwa na damu kiasi. Kutumia NSAID, kama vile ibuprofen, dakika 20 kabla ya upasuaji kunaweza kusaidia kutuliza kutohisi vizuri wakati wa upasuaji.

Biopsi za Magonjwa ya Uzazi ya Wanawake

Bayopsi inajumuisha kuondoa sampuli ndogo ya tishu ili ichunguzwe kwa kutumia hadubini. Biopsi ya kuma, uke, mlango wa kizazi au utando wa uterasi inaweza kufanywa.

Shingo ya kizazi au uke

Bayopsi ya mlango wa kizazi hufanywa wakati

  • Matokeo ya kipimo cha Pap yalionyesha hali ambayo inaweza kusababisha kansa (hali ya kabla ya kansa) au kansa inashukiwa.

  • Daktari huona jambo lisilo la kawaida wakati wa uchunguzi wa fupanyonga.

Biopsi ya mlango wa kizazi au uke kwa kawaida hufanywa wakati wa kolposkopia. Wakati wa kolposkopi, madaktari wanaweza kutambua eneo linaloonekana kuwa lisilo la kawaida na kuchukua sampuli za tishu hapo.

Kwa kawaida, bayopsi ya mlango wa kizazi au uke haihitaji ganzi (dawa ya ganzi), ingawa utaratibu huu kwa kawaida huhisi kama kubanwa au kuuma kwa misuli. Kutumia dawa ya kuzuia uvimbe isiyo ya steroidi (NSAID), kama vile ibuprofen, dakika 20 kabla ya utaratibu kunaweza kusaidia kupunguza usumbufu wowote wakati wa utaratibu.

Vulva

Biopsi ya kuma (eneo linalozunguka mlango wa uke) hufanywa wakati

  • Utambuzi hauwezi kufanywa kulingana na dalili za mwanamke na matokeo ya uchunguzi wa kimwili.

  • Kansa ya uke inashukiwa.

Bayopsi ya kuma kwa kawaida inaweza kufanywa katika ofisi ya daktari na inahitaji matumizi ya ganzi ya ndani. Ikiwa kansa au matatizo ya kabla ya kansa inayosababishwa na HPV inashukiwa, wakati mwingine kolposkopu hutumika kuangalia eneo lisilo la kawaida na kuongoza bayopsi.

Uterasi

Biopsi ya utando wa uterasi (bayopsi ya endometriamu) kwa kawaida hufanywa ili

Pia, wataalamu wa utasa hutumia utaratibu huu kubaini ikiwa kutaga mayai kunatokea kwa njia ya kawaida na iwapo uterasi iko tayari kupandikizwa viinitete kama sehemu ya utungisho wa ndani ya vitro.

Kwa bayopsi ya endometriamu (mpumuo wa endometriamu), spekulamu hutumika kushikilia kuta za uke, na, baada ya kusafisha mlango wa kizazi kwa kioevu cha antiseptiki, neli ndogo ya plastiki (upana wa milimita 3) huingizwa kupitia mlango wa kizazi hadi kwenye uterasi. Neli hutumika kutoa tishu kwenye utando wa uterasi.

Bayopsi ya endometriamu inaweza kufanywa katika ofisi ya daktari na kwa kawaida haihitaji ganzi. Kwa kawaida, huhisi kama maumivu makali ya hedhi. Kutumia NSAID, kama vile ibuprofen, dakika 20 kabla ya upasuaji kunaweza kusaidia kutuliza kutohisi vizuri wakati wa upasuaji.

Uchunguzi wa Picha za Magonjwa ya Uzazi ya Wanawake

Atrasonografia

Altrasonografia (sonografia) hutumia mawimbi ya kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti, yanayotolewa kwa masafa ya juu hivyo haisikiki. Mawimbi ya kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti hutolewa na kifaa cha mkononi kinachowekwa kwenye fumbatio (kinachoitwa atrasonografia ya fumbatio) au ndani ya uke (kinachoitwa atrasonografia ya ukeni). Mawimbi huakisi kwenye nyenzo za ndani, na muundo unaotokana na kuakisi unaweza kuonyeshwa kwenye skrini.

Mara kwa mara altrasonografia kwenye uke hufanywa ili kugundua yafuatayo:

  • Ujauzito wa nje ya kizazi

  • Uvimbe wa kawaida, uvimbe uliojaa maji na kasoro nyingine katika viungo vya ndani vya uzazi (ovari, mirija ya ova, uterasi na uke)

Kipimo cha picha kwa kutumia mawimbi ya sauti ndani ya uke kinaweza pia kutumika kumwongoza daktari wakati wa taratibu fulani (kupanua na kupooza, kuweka kifaa ndani ya uterasi).

Altrasonografia kwenye fumbatio na kwenye uke inaweza kufanywa wakati wa ujauzito kwa sababu zifuatazo:

Altrasonografia haina maumivu na haina hatari zinazojulikana kwa mama au kijusi.

Upigaji picha kwa mwangwi wa sumaku (MRI) au Tomografia ya kompyuta (uchanganuzi wa CT)

Ikiwa tathmini kwa kutumia altrasonografia haitoshi, MRI (ambayo ni nzuri sana katika kugundua matatizo kwenye fupanyonga lakini ni ghali) inaweza kutumika. CT kwa kawaida haipendezi sana kwa sababu si sahihi sana kwa tatizo la wanawake, inahusisha mfiduo mkubwa wa mionzi, na mara nyingi huhitaji sindano majimaji yenye kutofautisha. CT hutumika zaidi wakati wa kutathmini kansa ya wanawake ambayo imeenea.

Sonografia ya Myeyusho wa Chumvi na Maji

Kwa sonografia ya myeyusho wa chumvi na maji (sonohysterography), kiowevu huwekwa kwenye uterasi kupitia neli nyembamba (catheter) ambayo huingizwa kupitia uke na kisha mlango wa kizazi. Kisha altrasonografia inafanywa. Kiowevu hujaza na kunyoosha uterasi ili kasoro ndani ya uterasi, kama vile polipu au fibroidi, ziweze kugunduliwa kwa urahisi zaidi.

Utaratibu huu hufanywa katika ofisi ya daktari na unaweza kuhitaji ganzi ya ndani. Kutumia NSAID, kama vile ibuprofen, dakika 20 kabla ya upasuaji kunaweza kusaidia kutuliza kutohisi vizuri.

Histerosalpingografia

Kwa hysterosalpingography, eksirei huchukuliwa baada ya majimaji yenye kutofautisha, ambao yanaweza kuonekana kwenye eksirei, kudungwa kupitia mlango wa kizazi ili kuonyesha sehemu ya ndani ya uterasi na mirija ya ova.

Mara nyingi histerosalpingografia hutumiwa kufanya yafuatayo

  • Ili kusaidia kubaini chanzo cha utasa

  • Ili kuthibitisha kwamba utaratibu wa kusafisha vijidudu ili kuziba neli umefanikiwa

Utaratibu huu hufanywa sehemu ambako eksirei zinaweza kuchukuliwa, kama vile hospitalini au chumba cha radiolojia cha ofisi ya daktari.

Kwa kawaida histerosalpingografia husababisha usumbufu, kama vile maumivu tumboni. Kutumia NSAID, kama vile ibuprofen, dakika 20 kabla ya upasuaji kunaweza kusaidia kutuliza kutohisi vizuri.

Taratibu za Uchunguzi

Wakati mwingine, taratibu za uchunguzi zaidi zinahitajika.

Kupanua na kuponya

Kwa kupanua na kuponya (D na C), kwa kawaida dawa ya kupoteza fahamu au ganzi ya mwili mzima hutumika. (Kwa kutumia dawa ya kutuliza fahamu, watu wanaweza kuitikia maelekezo lakini hawahisi maumivu.) Kisha, spekulamu hutumika kutawanya kuta za uke, na mlango wa kizazi hupanuliwa kwa kutumia vijiti vyembamba vya ukubwa unaoongezeka. Wakati mwingine dawa hutumika kusaidia kupanua mlango wa kizazi. Kisha kifaa kidogo, chenye ncha kali, chenye umbo la kijiko (kisunzi) kinaweza kuingizwa ili kuondoa tishu kutoka kwenye utando wa uterasi. Wakati mwingine neli ya plastiki iliyounganishwa na mashine ya kufyonza (kisunzi cha kufyonza) au vifaa vingine hutumiwa, ikiwa tishu zinahitaji kuondolewa baada ya kuharibika mimba au tatizo jingine linalohusiana na ujauzito.

D na C

Baada ya spekulamu kuwekwa panapofaa, chuma iliyopinda (vipanuzi—haijaonyeshwa) hutumika kupanua mlango wa kizazi ili kisunzi kiweze kuingizwa kwenye uterasi. Kisunzi hutumika kuondoa tishu kutoka kwenye utando wa uterasi.

D na C zinaweza kutumika kutibu wanawake wanaotokwa na damu kwenye uterasi kwa hali isiyo ya kawaida au kuharibika mimbaambako hakujakamilika au vipengee vingine vya mimba vilivyosalia baada ya ujauzito. Mara nyingi hufanywa wakati wa utaratibu sawa na histeroskopia ili daktari aweze kuona ndani ya uterasi.

D na C mara nyingi hufanywa katika chumba cha upasuaji hospitalini. Hata hivyo, wanawake wengi hawalazimiki kusalia hospitalini usiku kucha.

Histeroskopia

Ili kuona sehemu ya ndani ya uterasi, madaktari wanaweza kuingiza neli nyembamba wa kutazama (hysteroscope) kupitia uke na mlango wa kizazi ndani ya uterasi. Neli ina kipenyo cha milimita 4 au 5 (karibu inchi 1/4) na ina nyaya zinazopitisha mwanga. Vifaa vinavyotumika kwa bayopsi, utabibu wa umeme (joto) au upasuaji vinaweza kupitishwa kupitia neli. Sehemu kunakotokwa na damu kwa hali isiyo ya kawaida au kasoro nyingine kwa kawaida linaweza kuonekana na linaweza kuchunguzwa kupitia bayopsi, kufungwa kwa kutumia joto au kuondolewa.

Histeroskopia inaweza kutumika kwa tathmini au matibabu ya njia inayopitia mlango wa kizazi (inayoitwa endocervix au mfereji wa mlango wa kizazi) au kijishimo cha uterasi ili kufanya yafuatayo:

  • Tambua matatizo kwenye uterasi, kama vile polipu, tumbawe, hyperplasia ya endometriamu (ukuaji mkubwa wa utando wa uterasi), kansa ya uterasi, tishu za kovu au kasoro nyinginezo.

  • Ili kutibu kasoro kwenye uterasi, kama vile kuondola polipu, fibroidi, kifaa cha kuingizwa kwenye uterasi kilichopotea au matatizo mengine yasiyo ya kawaida au kuondoa endometriamu (utaratibu wa kutibu kuvija damu nyingi kwenye kizazi kwa kutumia joto au aina nyingine za nishati ili kupunguza utando wa uterasi).

Wakati mwingine histeroskopia ya utambuzi (na aina fulani za matibabu) hufanywa katika ofisi ya daktari. Mara nyingi zaidi, hufanywa hospitalini kwa ganzi ya mwili mzima.

Laparoskopia

Ili kuchunguza moja kwa moja uterasi, mirija ya ova au ovari, madaktari hutumia neli ya kutazama inayoitwa laparoskopi. Laparoskopi imeunganishwa kwenye kebo nyembamba yenye vijiti vya plastiki au kioo vinavyonyumbulika vinavyosambaza mwanga.

Laparoskopi huingizwa ndani ya utobo wa tumbo kupitia chale ndogo chini ya kitovu. Kipima kidonda huingizwa kupitia uke hadi kwenye uterasi. Kipima kidonda hicho huwawezesha madaktari kudhibiti viungo ili vionekane vyema zaidi. Dioksidi ya kaboni husukumwa kupitia laparoskopi ili kupanua fumbatio, ili viungo vilivyo kwenye fumbatio na fupanyonga viweze kuonekana vyema.

Mara nyingi, laparoskopia hutumiwa kufanya yafuatayo:

  • Kubaini chanzo cha maumivu ya fupanyonga, utasa na ugonjwa mwingine wa wanawake

  • Ili kufanya taratibu za upasuaji, kama vile biopsy, kusafisha neli, kuondoa uvimbe wa ovari uliojaa maji, kuondoa ovari na mirija ya uzazi, kuondoa ujauzito wa nje ya kizazi kwenye mirija ya ova, histerektomia au upasuaji wa kuchomoza kwa kiungo cha fupanyonga.

Laparoskopia inaweza kugundua kasoro za kimuundo ndogo sana kuweza kugunduliwa kwa kutumia picha, pamoja na kasoro kwenye sehemu za viungo, kama vile (tishu za endometriamu nje ya uterasi), uvimbe na makovu.

Chale za ziada zinaweza kuhitajika ikiwa taratibu za upasuaji wa kina, kama vile kuondoa uvimbe wa ovari uliojaa maji au uterasi (histerektomia), zinahitajika.

Laparoskopia hufanyika hospitalini na inahitaji ganzi, kwa kawaida ganzi ya mwili mzima. Kwa kawaida kulazwa hospitalini usiku kucha hakuhitajiki. Laparoscopia inaweza kusababisha maumivu kwenye fumbatio, lakini shughuli za kawaida zinaweza kurejelewa ndani ya siku 3 hadi 5, kulingana na kiwango cha utaratibu uliofanywa kupitia laparoskopia.