Adenomyosis ya Uterasi

NaCharles Kilpatrick, MD, MEd, Baylor College of Medicine
Imekaguliwa naOluwatosin Goje, MD, MSCR, Cleveland Clinic, Lerner College of Medicine of Case Western Reserve University
Imepitiwa/Imerekebishwa Imebadilishwa Oct 2025
v1666466_sw

Katika adenomayosisi, tishu kutoka kwenye tezi za utando wa uterasi (endometriamu) hukua ndani ya ukuta wa misuli wa uterasi. Uterasi huwa mkubwa kuliko kawaida, wakati mwingine ukubwa wake huongezeka mara mbili au tatu.

  • Adenomayosisi inaweza kusababisha vipindi vya hedhi nzito na yenye maumivu pamoja na fupanyonga.

  • Madaktari hushuku kuwepo kwa adenomayosisi wanapofanya uchunguzi wa fupanyonga, na mara nyingi hufanya kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti au picha ya mwangwi wa sumaku ili kusaidia utambuzi wa ugongwa.

  • Kifaa cha ndani ya uterasi kinachotoa homoni ya kike ya kutengenezwa inayoitwa levonorgestrel kinaweza kusaidia kupunguza dalili, lakini histerektomia ndiyo yenye ufanisi zaidi.

Idadi ya wanawake wenye adenomayosisi haijulikani, kwa kiasi fulani kwa sababu ni vigumu kuitambua.

Baadhi ya wanawake wenye adenomayosisi pia huwa na endometrayosisi au tumbawe.

Chanzo cha adenomayosisi hakijulikani.

Dalili za Adenomyosis ya Uterasi

Dalili za adenomayosisi ni pamoja na hedhi nzito na yenye maumivu (dysmenorrhea), maumivu yasiyo dhahiri katika eneo la fupanyonga, na hisia ya mgandamizo kwenye kibofu na rektamu. Kutokwa na damu sana kunaweza kusababisha anemia. Wakati mwingine tendo la ndoa huwa na maumivu.

Kwa kawaida, dalili hutoweka au kupungua baada ya kukatika hedhi.

Utambuzi wa Adenomyosis ya Uterasi

  • Uchunguzi wa Fupanyonga

  • Kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti au picha ya mwangwi wa sumaku (MRI)

Madaktari wanaweza kushuku kuwepo kwa adenomayosisi wanapofanya uchunguzi wa fupanyonga na kugundua kuwa uterasi umekuwa mkubwa, wa duara, na laini kuliko kawaida.

Mara nyingi madaktari hutambua adenomayosisi kulingana na matokeo ya kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti au picha ya mwangwi wa sumaku (MRI) ya fupanyonga. Mara nyingi kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti hufanywa kwa kutumia kifaa cha ultrasound kinachoshikiliwa mkononi na kuingizwa ukeni (inayoitwa Kipimo cha picha kwa kutumia mawimbi ya sauti ndani ya uke).

Hata hivyo, ili kupata utambuzi wa hakika wa adenomayosisi, ni sharti madaktari wachunguze tishu zilizotolewa kwenye uterasi. Njia pekee ya kupata tishu hizi ni kuondoa uterasi (histerektomia).

Matibabu ya Adenomyosis ya Uterasi

  • Kifaa cha ndani ya uterasi cha levonorgestrel

  • Dawa za kuzuia mimba

  • Kwa dalili kali, histerektomia

Kutumia kifaa cha ndani ya uterasi (IUD) kinachotoa homoni ya kike ya kutengenezwa inayoitwa levonorgestrel kunaweza kusaidia kudhibiti kuvuja damu na vipindi vya hedhi yenye maumivu. Madaktari wanaweza kupendekeza kutumia tembe za kuzuia mimba (tembe za kupanga uzazi), lakini huenda tembe hizo zisiwe na ufanisi.

Dawa za kutuliza maumivu (analgesics) zinaweza kutumiwa ili kutuliza maumivu.

Ikiwa dalili ni kali, histerektomia hufanywa. Histerektomia huondoa dalili kabisa.