Maambukizi wa Intraamniotic

(Chorioamnionitis)

NaJulie S. Moldenhauer, MD, Children's Hospital of Philadelphia
Imekaguliwa naSusan L. Hendrix, DO, Michigan State University College of Osteopathic Medicine
Imepitiwa/Imerekebishwa Jan 2024 | Imebadilishwa Sept 2024
v8949778_sw

Maambukizo kwenye chupa ya uzazi ni maambukizo na uvimbe unaotokana na tishu zinazozunguka kijusi, kama vile kiowevu kinachozunguka kijusi (maji ya uzazi), kondo la nyuma, utando unaozunguka kijusi, kijusi chenyewe au mchanganyiko wa hivi.

  • Maambukizo ndani ya chupa ya uzazi huongeza hatari ya matatizo kwa mwanamke mjamzito na kwa kijusi.

  • Wanawake kwa kawaida hupata homa na mara nyingi huwa na maumivu ya fupanyonga na kutokwa na uchafu ukeni.

  • Kwa kawaida, madaktari wanaweza kugundua maambukizo kwa kufanya uchunguzi wa mwili, lakini wakati mwingine ni lazima kiowevu cha uzazi kifanyiwe uchunguzi.

  • Wanawake hupewa viua kijasumu na dawa za kupunguza joto mwilini na mpango wa kujifungua kuwekwa haraka iwezekanavyo.

Viashiria vya hatari vya maambukizi ya intraamniotic

Maambukizo ndani ya chupa ya uzazi kwa kawaida hutokea wakati bakteria kutoka kwenye uke zinapoingia kwenye uterasi na kuambukiza tishu zinazozunguka kijusi. Kwa kawaida, aina nyingi za bakteria huishi kwenye uke. Kwa kawaida, huwa hazisababishi maambukizo ukeni, lakini zikisambaa hadi kwenye uterasi, zinaweza kusababisha maambukizo kwenye uterasi. Kwa kawaida, makamasi yalioko kwenye mlango wa kizazi, utando unaozunguka kijusi, na kondo la nyuma huzuia bakteria kusababisha maambukizo. Hata hivyo, hali fulani zinaweza kufanya iwe rahisi kwa bakteria kupenya kinga hizi.

Maambukizo ndani ya chupa ya uzazi pia yana uwezekano mkubwa wa kutokea ikiwa

  • Utando unaozunguka kijusi umepasuka mapema mno (huitwa kupasuka kwa utando kabla ya uchungu).

  • Kuna ucheleweshaji mrefu kati ya kupasuka kwa utando na kuzaliwa kwa mtoto. Kadiri ucheleweshaji unavyokuwa mrefu, ndivyo uwezekano wa maambukizo ndani ya chupa ya uzazi unavyoongezeka.

  • Uchungu unaanza mapema (uchungu wa uzazi kabla ya wakati).

  • Maji ya amnioti yana meconium (choo cha rangi ya kijani kibichi kinachotolewa na kijusi kabla ya kuzaliwa na ambacho kwa kawaida hutolewa baada ya kuzaliwa).

  • Bakteria zinazoweza kusababisha maambukizo zipo kwenye njia ya uzazi. Wanawake wanaweza kukosa kufahamu kuwa kuna bakteria hizi, hasa ikiwa hawajapata huduma ya kawaida ya kliniki ya wajawazito, ambapo vipimo vya bakteria hizi vingekuwa vimefanywa.

  • Madaktari au wakunga hufanya uchunguzi mwingi wa fupanyonga kwa wanawake ambao utando wao umepasuka. Uchunguzi wa aina hiyo unaweza kuingiza bakteria kwenye uke na uterasi.

  • Uchungu unachukua muda mrefu.

Mara chache, maambukizo hutokea wakati ufuatiliaji wa sehemu za ndani za kijusi unafanywa. Kwa utaratibu huu, madaktari hukifuatilia kijusi kwa kuingiza elektrodi (sensa ndogo ya mviringo iliyounganishwa kwenye waya) kupitia uke wa mwanamke na kuibandika kwenye ngozi ya kichwa cha kijusi.

Matatizo ya maambukizi ya intraamniotic

Maambukizo ndani ya chupa ya uzazi yanaweza kuongeza hatari ya matatizo yafuatayo kwa kijusi au mtoto mchanga:

Maambukioi ndani ya chupa ya uzazi yanaweza kusababisha, na pia yanaweza kutokana na, kujifungua kabla ya wakati au kupasuka kwa utando kabla ya uchungu na kabla ya wakati.

Maambukizo ndani ya chupa ya uzazi yanaweza kuongeza hatari ya matatizo yafuatayo kwa mwanamke:

Mara chache, ikiwa maambukizo ndani ya chupa ya uzazi hayatatibiwa, wanawake wanaweza kupata matatizo yanayotokana na sumu katika damu (shinikizo la damu kushuka kiasi cha kuhatarisha maisha kutokana na maambukizo makali kwenye mwili mzima), ugonjwa wa kuganda kwa damu uliokithiri (tatizo la kuganda kwa damu linalosababisha madonge ya damu na kutokwa na damu) na ugonjwa mbaya wa shida ya kupumua.

Dalili za maambukizi ya intraamniotic

Maambukizo ndani ya chupa ya uzazi kwa kawaida husababisha homa na mara nyingi husababisha maumivu ya fumbatio na kutoa uchafu ukeni ambao unaweza kuwa na harufu mbaya. Mama na kijusi wanaweza kuwa na mapigo ya moyo ya juu sana. Hata hivyo, baadhi ya wanawake huwa hawana dalili za kawaida.

Utambuzi wa maambukizi ya intraamniotic

  • Tathmini ya daktari

  • Idadi kamili ya damu

  • Wakati mwingine amniosentesisi

Madaktari hufanya uchunguzi wa mwili na kipimo kamili cha damu (ambacho kinajumuisha idadi ya seli nyeupe za damu).

Maambukizo ya ndani ya uterasi hushukiwa wakati mwanamke ana homa na angalau dalili nyingine moja ya kawaida, kama vile mapigo ya moyo ya haraka kwa kijusi, au utokaji wa uchafu wenye harufu mbaya, au idadi kubwa isiyo ya kawaida ya seli nyeupe za damu kwa mwanamke. Ikiwa utambuzi bado haueleweki vizuri, madaktari wanaweza kuchukua sampuli ya kiowevu cha uterasi na kuipima (amniosentesisi).

Ikiwa uchungu wa uzazi kabla ya wakati au kupasuka kwa utando kabla ya uchungu kuanza kutatokea, madaktari hufikiria uwezekano wa kuwepo kwa maambukizo hata kama mwanamke hana dalili za kawaida.

Matibabu ya Maambukizi ya Intraamniotic

  • Dawa za kuua bakteria

  • Dawa za kushusha halijoto mwilini.

  • Kuzaa

Wanawake wenye maambukizo ya ndani ya uterasi hupewa viua vijasumu kupitia mshipa wa damu. Pia hupewa dawa za kushusha halijoto mwilini (ikiwezekana acetaminophen kabla ya kujifungua).

Kujifungua hakupaswi kucheleweshwa mara tu utambuzi unapofanyika.

Ikiwa uchungu haujaanza, uchungu unaweza kuanzishwa kwa kutumia dawa (kuanzisha uchungu).

Kujifungua kwa njia ya upasuaji kwa dharura mara nyingi si lazima ikiwa mama na kijusi wako katika hali nzuri na ikiwa viua vijasumu vinatolewa wakati uchungu unaanzishwa.

Kinga ya Maambukizi ya Intraamniotic

Ikiwa utando wa mwanamke utapasuka kabla ya wakati na kabla ya uchungu kuanza, madaktari hufanya uchunguzi wa fupanyonga pale tu inapohitajika.

Kwa kawaida, madaktari pia humpa mwanamke viua vijasumu kupitia mshipa wa damu na kwa kunywa ili kusaidia ujauzito udumu kwa muda mrefu zaidi na kupunguza hatari ya matatizo kwa kijusi.

Madaktari huwafanyia uchunguzi wagonjwa wajawazito ili kubaini uwepo wa streptococcus ya aina ya B katika wiki ya 35 hadi 37 ya ujauzito. Watu ambao matokeo yao yanaonyesha uwepo wa bakteria hizo hupewa viua vijasumu wakati wa uchungu wa uzazi.