Historia ya uzazi na ugonjwa wa wanawake mara nyingi huchukuliwa kama sehemu tofauti ya historia ya matibabu. Historia hii inajumuisha historia ya matibabu ya zamani inayohusiana na afya ya uzazi na jumla ya wanawake, ikiwa ni pamoja na mimba, hedhi, matatizo ya afya ya ngono, udhibiti wa uzazi na kukatika hedhi.
Kwa huduma ya ugonjwa wa wanawake, mwanamke anapaswa kuchagua mtaalamu wa afya ambaye anaweza kujadili naye kwa urahisi mada nyeti, kama vile matatizo ya utendaji wa ngono, udhibiti wa uzazi, ujauzito na kukatika hedhi. Daktari anaweza kuwa daktari, ikiwa ni pamoja na daktari wa ugonjwa wa wanawake, daktari wa huduma ya msingi, mkunga, muuguzi mtaalamu au msaidizi wa daktari. Tathmini ya jinakolojia kwa watoto na wasichana balehe ikiwa inahitajika, kwa kawaida inaweza kufanywa na daktari wa watoto wa mtoto.
Tathmini ya ugonjwa wa wanawake inajumuisha historia ya uzazi na ugonjwa wa wanawake na, kwa kawaida, uchunguzi wa fupanyonga.
Kwa historia ya ugonjwa wa wanawake, madaktari huuliza kuhusu vipindi vya hedhi vya zamani na vya sasa, mimba za zamani, shughuli za ngono na dalili za ugonjwa wa wanawake, matatizo na matibabu ambayo mwanamke amewahi kupata hapo awali au anayopokea.
Maswali kuhusu hedhi ni pamoja na yafuatayo:
Umri wa mwanamke wakati hedhi ilianza
Hedhi hutokea mara ngapi, kawaida vipi na kwa muda upi
Jinsi hedhi ambapo damu hutoka nyingi huwa
Hedhi ya mwisho ilipoanza na kuisha
Ikiwa mwanamke ana dalili (kama vile maumivu, mkakamao wa hedhi, maumivu ya kichwa au kinyesi kinacholegea) wakati wa hedhi
Ikiwa mwanamke amewahi au amekuwa na hali ambapo anatokwa na damu kwa hali isiyo ya kawaida—kutokwa na damu nyingi sana, kidogo sana au kati ya hedhi
Maswali kuhusu mimba za awali ni pamoja na yafuatayo:
Mwanamke amepata mimba ngapi
Tarehe za mimba hizo zilikuwa zipi
Jinsi mimba hizo zilivyoisha (kama vile wakati wa kujifungua mtoto akiwa hai au kuharibika mimba) na katika kipindi kipi cha kuchukua mimba
Ikiwa matatizo (kama vile kutokwa na damu nyingi wakati wa ujauzito au baada yake, shinikizo la damu, kisukari) yalitokea
Dalili za ugonjwa wa wanawake zinazojadiliwa daktari anapochukua historia ni pamoja na zifuatazo:
Kutojizuia kuenda haja ndogo au kubwa
Kwa kawaida daktari huuliza kuhusu shughuli za ngono ili kutathmini hatari ya maambukizi ya zinaa, upangaji wa uzazi, ujauzito na matatizo ya afya ya ngono. Mwanamke huulizwa iwapo anatumia au anataka kutumia njia za upangaji wa uzazi na ikiwa ana nia ya kupata ushauri nasaha kuhusu upangaji wa uzazi, kujiandaa kwa ujauzito au taarifa nyingine.
Daktari huuliza ikiwa mwanamke huhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa, katikati ya mzunguko wa hedhi (ambayo inaweza kuonyesha kwamba maumivu hayo yanaambatana na kutaga mayai) au katika hali nyingine. Ikiwa ana maumivu, huwa anaulizwa kuhusu sehemu, yalipoanza, ikiwa yalianza polepole au ghafla, muda, ukali, dalili zinazohusiana na mambo ya kupunguza au kuzidisha maumivu.
Daktari pia huuliza kuhusu matatizo ya matiti, kama vile maumivu, uvimbe, maeneo yenye uchungu au wekundu na kutoka kwa dutu kwenye chuchu. Mwanamke huulizwa iwapo anahitaji taarifa yoyote kuhusu mbinu ya kujichunguza matiti.
Daktari huuliza kuhusu historia ya jumla ya matibabu na upasuaji ya mwanamke.
Daktari hupitia dawa zote ambazo mwanamke anatumia, ikiwa ni pamoja na dawa za kuagizwa na daktari na zisizoagizwa na daktari, tumbaku na pombe, kwa sababu nyingi huathiri utendaji kazi wa wanawake.
Mwanamke huulizwa kuhusu unyanyasajiwa kiakili, kimwili au kingono—iwapo ananyanyaswa au amenyanyaswa hapo awali.