Mimba inachukuliwa kuwa ya hatari ya juu wakati mama na/au kijuzi wana matatizo ya kimatibabu au matatizo mengine ya kiafya ambayo huongeza hatari ya kuugua kabla, wakati, au baada ya kujifungua.
Mimba zenye hatari ya juu ni pamoja na zile ambazo kuna hatari inayowezekana kwa afya ya mama na/au kijusi au mtoto. Hatari zinaweza kusababishwa na mambo mbalimbali kama vile ugonjwa sugu, kuwa na kijusi zaidi ya kimoja (mimba nyingi), matatizo ya awali ya ujauzito, au matatizo yanayohusiana au yasiyohusiana na ujauzito yanayotokea wakati wa ujauzito.
Hali au sifa fulani, zinazoitwa mambo ya hatari, hufanya ujauzito kuwa wa hatari wa juu. Kama sehemu ya utaratibu utunzaji wakati wa ujauzito, madaktari huchunguza mambo haya ili kubaini kiwango cha hatari kwa mwanamke fulani na mtoto na hivyo kutoa huduma bora ya kimatibabu. Kwa baadhi ya wazazi watarajiwa, tathmini ya kijenetiki inashauriwa. Inahusisha kutathmini historia ya familia zao na, ikihitajika, kuchambua sampuli za damu au tishu (kama vile seli kutoka ndani ya shavu). Tathmini hii inafanywa ili kubaini kama kuna hatari iliyoongezeka ya kupata mtoto mwenye ugonjwa wa kijenetiki unaorithiwa.
Mambo yanayoweza kuathiri hatari kwa wanawake ni pamoja na
Sifa za kimwili (kama vile umri na uzani)
Matatizo yanayotokea wakati wa uchungu wa kujifungua na kujifungua
Matatizo yaliyokuwepo kabla ya ujauzito, kama vile shinikizo la juu sana la damu (shinikizo la juu la damu), kisukari, maambukizi ya zinaa, au maambukizi ya figo
Matatizo yanayotokea wakati wa ujauzito, kama vile kisukari cha ujauzito au preklampsia
Mimba zenye hatari ya juu lazima zifuatiliwe kwa karibu na zihusishe huduma maalum, mara nyingi ikiwa ni pamoja na madaktari wa uzazi na hospitali iliyobobea katika mimba zenye hatari ya juu.