Maambukizi ya Virusi vya Cytomegalo (CMV) kwa Watoto Waliozaliwa Karibuni

(Maambukizi ya Kirusi vya Sitomegalo ya kuzaliwa; Maambukizi ya Virusi vya Sitomegalo ya Uzazi)

NaAnnabelle de St. Maurice, MD, MPH, UCLA, David Geffen School of Medicine
Imekaguliwa naBrenda L. Tesini, MD, University of Rochester School of Medicine and Dentistry
Imepitiwa/Imerekebishwa Imebadilishwa Apr 2025
v34436815_sw

Kirusi cha sitomegalo ni cha kawaida ambacho husababisha matatizo machache au hakisababishi matatizo kabisa lakini kinaweza kuwafanya watoto wachanga walioambukizwa kabla au wakati wa kuzaliwa waumwe sana.

  • Maambukizi haya husababishwa na virusi.

  • Watoto wengi hawana dalili, lakini wengine hupata matatizo kulingana na wakati walipoambukizwa.

  • Utambuzi hufanyika kwa kutambua virusi kwenye mkojo, mate, damu, au tishu.

  • CMV haina tiba ya kuiondoa kabisa, lakini dawa za kuzuia virusi zinaweza kupunguza ukali wa matatizo.

  • Watoto wanaweza kupata matatizo ya neva kama kupoteza uwezo wa kusikia.

  • Kunawa mikono husaidia kuzuia kuenea kwa virusi hivi.

(Tazama pia Muhtasari wa Maambukizi kwa Watoto Wachanga na Maambukizi ya CMV kwa watu wazima.)

Maambukizi kwa kirusi cha sitomegalo (CMV) inatokea sana. Watu wazima wengi wamewahi kupata CMV wakati Fulani. Virusi haviondoki kabisa na hubaki bila kufanya kazi (si amilifu) katika tishu mbalimbali kwa maisha. Wakati mwingine virusi hivi vinaweza kuanza kufanya kazi tena (reactivate).

Watu wengi wenye CMV, wakiwemo watoto wachanga, hawana dalili zozote.

Mtoto anapopata CMV akiwa tumboni, huitwa maambukizi ya kuzaliwa nayo (congenital CMV). Akipata maambukizi kabla, wakati, au muda mfupi baada ya kuzaliwa, huitwa maambukizi ya wakati wa kujifungua (perinatal CMV). CMV ndiyo maambukizi ya virusi yanayoongoza kwa watoto wanaozaliwa nayo.

Wajawazito ambao hawajawahi kupata CMV wanaweza kuambukizwa kupitia kugusana na watu wenye virusi, hasa watoto wadogo. Wakati mwingine, virusi vilivyolala mwilini mwa mjamzito huamka tena. Virusi vinaweza kuvuka kondo la nyuma (placenta) na kumwambukiza kijusi.

Watoto wanaweza pia kuambukizwa wakati wa kupita kwenye njia ya uzazi, kupitia maziwa ya mama, au kuongezewa damu yenye virusi.

Watoto njiti wako hatarini zaidi kupata dalili za CMV kwa sababu hawana kingamwili za kutosha kutoka kwa mama zao.

Dalili za Maambukizi ya CMV kwa Watoto Waliozaliwa Karibuni

Maambukizi ya CMV huleta matatizo tofauti kulingana na ikiwa mtoto aliambukizwa kabla au baada ya kuzaliwa.

Takribani asilimia 13 ya watoto walioambukizwa kabla ya kuzaliwa huonyesha dalili.

Dalili kwa watoto walioambukizwa kabla ya kuzaliwa ni pamoja na:

Dalili kwa watoto walioambukizwa wakati au baada ya kuzaliwa ni pamoja na

Baadhi ya watoto wachanga hupata dalili hizi zote.

Watoto walioambukizwa kupitia maziwa ya mama kawaida hupata maambukizi mepesi zaidi.

Utambuzi wa Maambukizi ya CMV kwa Watoto Waliozaliwa Karibuni

  • Kipimo cha PCR kwa kutumia mkojo, mate, damu, au tishu

  • Upimaji wa sampuli za mkojo, mate, au tishu

Ili kugundua CMV kabla ya kuzaliwa, madaktari hupima majimaji ya chupa ya uzazi (amniotic fluid).

Ili kugundua CMV baada ya kuzaliwa, madaktari hupima mkojo, mate, au tishu za mtoto mchanga. Sampuli hutumwa kwenye maabara ili kiumbe kinachosababisha maambukizi kiweze kutambuliwa.

Madaktari pia hufanya kipimo cha PCR kwenye sampuli za mtoto. Mbinu hii ya maabara inaweza kutambua virusi vya CMV kwa haraka kwa kuangalia vinasaba vyake.

Vipimo vingine kama vya damu, picha za kichwa na uchunguzi wa macho hufanywa kuona maambukizi na uvimbe na kuamua ukali wa ugonjwa. Madaktari pia hupima usikivu wa watoto wachanga. Upimaji huu ni wa kina zaidi kuliko vipimo vya kawaida vya usikivu kwa watoto wachanga.

Madaktari huangalia pia maambukizi mengine kama toksoplasmosisi, rubela, kaswende, na herpes simplex.

Matibabu ya Maambukizi ya CMV kwa Watoto Waliozaliwa Karibuni

  • Ganciclovir au valganciclovir kwa watoto wenye dalili.

CMV haina tiba ya kuiondoa kabisa mwilini.

Dawa za ganciclovir na valganciclovir ni dawa za kuzuia virusi zinazoweza kupunguza ukali wa dalili.

Watoto walioambukizwa wanapaswa kupimwa usikivu wao mara kwa mara katika mwaka wa kwanza.

Ubashiri wa Maambukizi ya CMV kwa Watoto Waliozaliwa Karibuni

CMV huua asilimia 5 hadi 10 ya watoto wenye dalili. Wengi wa manusura hupata ulemavu wa kusikia.

Hata watoto wasio na dalili wakati wa kuzaliwa, asilimia 5 hadi 15 kati yao hupata matatizo ya neva (hasa uziwi) baadaye. Kiwango fulani cha uziwi ndicho jambo linalotokea mara nyingi zaidi.

Uzuiaji wa Maambukizi ya CMV kwa Watoto Waliozaliwa Karibuni

Watu wajawazito wanapaswa kujaribu kupunguza uwezekano wa kuambukizwa virusi. Kwa mfano, kwa sababu maambukizi ya CMV ni ya kawaida miongoni mwa watoto wanaohudhuria vituo vya kulelea watoto mchana na huenea kwa urahisi, wajawazito wanapaswa kunawa mikono yao vizuri kila mara baada ya kupata mkojo na mate kutoka kwa watoto walio katika vituo vya kulelea watoto mchana.

Maziwa ya mama yaliyotolewa msaada yanaweza kuchemshwa (pasteurized) ili kuua virusi kabla ya kupewa watoto walio hatarini.