Tishu unganishi ni tishu ngumu, mara nyingi yenye nyuzinyuzi ambayo huunganisha miundo ya mwili pamoja na kushikilia na kutoa unyumbufu. Mifupa ya, misuli, gegedu, ligamentina kano hujengwa zaidi kwa tishu unganishi. Tishu unganishi pia zipo katika sehemu zingine za mwili, kama vile ngozi na viungo vya ndani. Sifa za tishu unganishi na aina za seli zilizomo hutofautiana, kulingana na mahali zinapatikana mwilini. Tishu unganishi za kawaida zina nguvu ya kutosha kuhimili uzito na ukakamavu unaohitajika na sehemu husika.
Kuna magonjwa zaidi ya 200 yanayohusiana na tishu unganishi. Magonjwa maalum yaliyojadiliwa hapa ni pamoja na yafuatayo:
Baadhi ya matatizo haya hayana chanzo dhahiri, mengine yanarithiwa na mengine hujitokeza baada ya muda kutokana na uharibifu wa tishu. Matatizo fulani ya kurithi husababisha tishu unganishi mwilini kujiwasilisha isivyo kawaida. Mara nyingi kasoro zinazosababishwa na matatizo ya tishu zinazounganisha viungo, iwe ya kurithi au la, hujitokeza wakati wa utoto au ujana na hudumu katika maisha yote.
Matatizo mengi ya tishu unganishi hugunduliwa kulingana na dalili na matokeo ambayo madaktari huyaona wakati wa uchunguzi wa kimwili. Eksirei inaweza kufichua kasoro za mifupa ambazo zinaweza kuhusishwa na ugonjwa wa tishu unganishi. Biopsy (kuondolewa kwa sampuli ya tishu kwa ajili ya uchunguzi chini ya darubini) pia inaweza kusaidia. Tishu kwa kawaida huondolewa kwa kutumia nusukaputi kwenye sehemu husika, ambayo hufisha ganzi sehemu hiyo. Uchambuzi wa jeni, kutoka kwa sampuli ya damu au seli zingine, unaweza kuwasaidia madaktari kugundua baadhi ya magonjwa ya kurithi.