Babesiosisi

NaChelsea Marie, PhD, University of Virginia;
William A. Petri, Jr, MD, PhD, University of Virginia School of Medicine
Imekaguliwa naChristina A. Muzny, MD, MSPH, Division of Infectious Diseases, University of Alabama at Birmingham
Imepitiwa/Imerekebishwa Imebadilishwa Sept 2025
v786629_sw

Babesiosis ni maambukizi ya seli nyekundu za damu yanayosababishwa na protozoa Babesia.

  • Babesiosis husambazwa na kupe wa kulungu.

  • Babesiosis inaweza kusababisha homa, maumivu ya kichwa, uchungu mwilini, na uchovu.

  • Ili kugundua babesiosis, madaktari huchunguza sampuli ya damu chini ya hadubini na kutafuta protozoa katika seli nyekundu za damu au kufanya vipimo vingine vya damu.

  • Watu wengi wenye afya njema hawahitaji kutibiwa, lakini, dalili zikitokea, watu hupewa muchanganyiko wa dawa.

  • Kuzuia kuumwa na kupe husaidia kuzuia babesiosis.

Protozoa ni aina ya vimelea. Wanaunda kundi tofauti la viumbe vidogo, vyenye seli moja. Baadhi ya protozoa huhitaji mwenyeji binadamu au mnyama ili kuishi. Kuna aina nyingi za protozoa.

Babesia ni protozoa za nje ya utumbo, kumaanisha husababisha maambukizi katika maeneo yaliyo nje ya utumbo wa mtu pekee kama vile damu. Babesia protozoa huambukiza seli nyekundu za damu na hatimaye kuziharibu.

Babesiosis ni ugonjwa unaotokea sana miongoni mwa wanyama, hasa panya, lakini ni nadra sana miongoni mwa watu. Mnamo 2020, kulikuwa na visa 1,827 vya babesiosis vilivyoripotiwa nchini Marekani.

Babesia microti ni spishi ya protozoa ambayo kwa kawaida huwaambukiza watu nchini Marekani. Maambukizi kwa watu hutokea katika visiwa vya pwani au maeneo ya pwani ya Massachusetts, Rhode Island, pwani ya Connecticut, Long Island ya mashariki, Vermont, na New Jersey. Maambukizi pia hutokea Wisconsin na Minnesota. Spishi tofauti ya Babesia huambukiza watu huko Missouri, Washington, na California na katika maeneo mengine ya dunia.

Babesiosis husambazwa na kupe wale wale wanaosambaza Ugonjwa wa Lyme (Ixodes kupe au kupe wa kulungu). Kupe ni vekta, kumaanisha kwamba hubeba na kusambaza vimelea vinavyosababisha magonjwa kwa watu. Kupe wanaweza kuambukizwa baada ya kulisha wanyama walioambukizwa, kama wanyama wagugunaji. Maambukizi huenea wakati kupe aliyeambukizwa anapomuuma mwanadamu au mnyama. Ni nadra, babesiosis inaweza kuambukizwa kupitia kuongezwa damu au inaweza kupitishwa kutoka kwa mjamzito hadi kwa mtoto mchanga.

Kupe wanaweza kuambukizwa na zote mbili Babesia na Ixodes, ambayo inamaanisha mtu anaweza kuwa na ugonjwa wa Lyme na babesiosis kwa wakati mmoja. Kupe wanaweza kusababisha maambukizi mengine kama vile anaplasmosis, homa inayorejeana encephalitis.

(Angalia pia Muhtasari wa Maambukizi ya Vimelea.)

Dalili za ugonjwa wa Babesiosisi

Baadhi ya watu wenye babesiosis, hasa watu wenye afya njema walio chini ya umri wa miaka 40, hawana dalili zinazoonekana. Watoto waliozaliwa karibuni wanaweza kuwa na homa, idadi ndogo ya seli nyekundu za damu (anemia), na idadi ndogo ya chembe chembe za damu (thrombocytopenia).

Dalili za babesiosis kwa kawaida huanza takriban wiki 1 hadi 2 baada ya watu kung’atwa. Watu wanaweza kuwa na homa, maumivu ya kichwa, uchungu kwenye misuli na viungo, kuhisi baridi, na uchovu. Kwa watu wenye afya njema, dalili kwa kawaida hutoweka baada ya wiki. Kwa watu wengine, kuvunjika kwa seli nyekundu za damu (hemolisisi) kunaweza kusababisha anemia ya hemolitiki na ngozi na weupe wa macho kugeuka manjano (homa ya manjano). Ini na wengu mara nyingi huongezeka kwa ukubwa.

Hatari ya ugonjwa mkali na kifo ni kubwa zaidi kwa watu wazee, ambao wengu wao umeondolewa, au wanaotumia dawa au wana matatizo ambayo hudhoofisha mfumo wa kinga (hasa maambukizi ya VVU yaliyofika hatua za juu sana [pia huitwa UKIMWI]). Kwa watu hawa, dalili ni pamoja na homa kali, anemia, mkojo mweusi, homa ya manjano, na kushindwa kwa figo.

Utambuzi wa ugonjwa wa Babesiosisi

  • Uchunguzi wa sampuli ya damu chini ya hadubini

  • Vipimo vingine vya damu

Madaktari wanaweza kushuku kuwa babesiosis iko kwa watu wenye dalili za kawaida na anemia ya hemolitiki na wanaoishi au wamesafiri hadi eneo ambalo maambukizi hutokea sana. Mara nyingi, watu hawakumbuki tukio la kung’atwa na kupe.

Ili kugundua babesiosis, daktari kwa kawaida huchunguza sampuli ya damu chini ya hadubini ili kuichunguza. Babesia katika seli nyekundu za damu. Ili kusaidia kutambua protozoa, sampuli ya damu inaweza kupimwa ili kubaini kama ina nyenzo za kijenetiki za Babesia(DNA) au kingamwili za Babesia. (Kingamwili ni protini zinazozalishwa na mfumo wa kingamwili ili kusaidia kulinda mwili dhidi ya mashambulizi fulani, ikiwa ni pamoja na yale ya vimelea.)

Matibabu ya ugonjwa wa Babesiosisi

  • Wakati matibabu yanapohitajika, atovaquone pamoja na azithromycin au quinine pamoja na clindamycin hutumiwa

  • Kubadilishana damu

Watu wasio na dalili kwa kawaida hawahitaji matibabu kwa sababu babesiosis kwa kawaida huisha yenyewe.

Watu wote wenye babesiosis kwa kawaida hutibiwa na atovaquone (dawa ambayo kwa kawaida hutumika kutibu maambukizi ya protozoa) pamoja na azithromycin (kiuavijasumu). Atovaquone pamoja azithromaisini ni matibabu yanayopendelewa zaidi kwa sababu yana madhara machache na yanafaa kama kwinini (inayotumika kutibu malaria) pamoja na clindamycin (kiua vijasumu) kwa watu walio na babesiosis.

Watu wenye dalili kali wanaweza kutibiwa kwa njia mbadala ya kutumia quinine pamoja na klindamisini.

Kwa watu wagonjwa sana, ubadilishanaji wa damu (ambapo damu ya mtu hubadilishwa na damu ya anayepatiana) unaweza kufanywa ili kupunguza kiasi cha vimelea vinavyozunguka kwenye damu.

Uzuiaji wa Ugonjwa wa Babesiosisi

Katika maeneo ambapo kupe wa kulungu hupatikana sana, watu wanaweza kupunguza hatari ya kupata babesiosis kwa kuchukua tahadhari dhidi ya kupe.

Watu wanaweza kupunguza uwezekano wao wa kung'atwa na kupe kwa kufanya yafuatayo:

  • Kukaa kwenye njia na vijia wakati wa kutembea katika maeneo yenye miti

  • Kutembea katikati ya vijia ili kuepuka kukwaruzwa dhidi ya matawi na magugu

  • Si kukaa chini au juu ya kuta za mawe

  • Kuvalia mashati yenye mikono mirefu

  • Kuvaa suruali ndefu na kuziingiza kwenye buti au soksi

  • Kuvalia nguo zenye rangi nyepesi, jambo linalofanya kupe kuwa rahisi kuonekana

  • Kujipaka dawa ya kufukuza wadudu yenye diethyltoluamide (DEET) kwenye ngozi

  • Kupaka dawa ya kufukuza wadudu yenye permethrin kwenye nguo au kuvaa nguo zilizotibiwa hapo awali kibiashara kwa kutumia permethrin

  • Kutafuta mara nyingi watoto na maeneo yenye manyoya mwilini kwa ajili ya kuona kama kuna kupe

Ili kumwondoa kupe, watu wanapaswa kutumia kibano chenye ncha nyembamba ili kushika kupe kwenye sehemu za kichwa na mdomo pale tu inapoingia kwenye ngozi na wanapaswa kumtoa kupe polepole. Mwili wa kupe haupaswi kushikwa au kufinywa. Mara tu kupe anaondolewa, eneo la ngozi linapaswa kusuguliwa kutumia spiriti. Jeli ya mafuta, spiriti, viberiti vilivyowashwa, au vichocheo vingine vyovyote si njia bora za kumwondoa kupe na hazipaswi kutumika. (Angalia pia Matibabu ya Kuumwa na Kupe.)

Je, Ulijua...

  • Kwa mng’ato wa kupe, tumia kibano ili kushika kichwa na sehemu za mdomo na kuondoa polepole. Usishike mwili wa kupe na usijaribu kumwondoa kwa kutumia mafuta ya kujipaka kwenye ngozi, spiriti, au kiberiti kilichowashwa.

Watu ambao wamewahi kuwa na babesiosis wanaweza kuzuia usambazaji wa maambukizi kwa kutotoa damu au viungo hadi watakapokamilisha matibabu na vimelea haviwezi kupatikana katika damu yao. Nchini Marekani, wachangiaji wa damu na viungo huchunguzwa katika maeneo ambapo kiwango cha maambukizi ni kikubwa kwa kiasi.

Kupe

Taarifa Zaidi

Nyenzo zifuatazo za lugha ya Kiingereza zinaweza kuwa muhimu. Tafadhali kumbuka kuwa Mwongozo hauwajibiki kwa maudhui ya nyenzo hizi.

  1. Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC): Kuhusu Babesiosis