Baadhi ya Maambukizi ya Rockttsial na Maambukizi Yanayohusiana

Baadhi ya Maambukizi ya Rockttsial na Maambukizi Yanayohusiana

Maambukizi

Kiumbe Anayeambukiza

Mwenyeji

Maeneo Ambapo Maambukizi Hutokea

Maelezo

Homa kali iletwayo na chawa

Homa kali iletwayo na chawa ya mlipuko (homa kali inayoenezwa na chawa)

Ugonjwa wa Brill-Zinsser (kurudi tena kwa ugonjwa wa homa kali iletwayo na chawa ya mlipuko, wakati mwingine miaka kadhaa baada ya maambukizi ya kwanza)

Rickettsia prowazekii, huenezwa na chawa au kwa njia zisizojulikana wakati wenyeji ni vichakuro wanaoruka

Watu na vichakuro wanaoruka

Duniani kote (sio kawaida nchini Marekani, lakini wakati mwingine hutokea kwa watu ambao wamewahi kugusana na vichakuro wanaoruka)

Takriban siku 7 hadi 14 baada ya bakteria kuingia mwilini, dalili huanza ghafla, zikiwa ni homa, maumivu ya kichwa, na uchovu mkubwa sana (kulegea kabisa). Upele huonekana siku ya 4 hadi 6. Ikiwa haijatibiwa, maambukizi yanaweza kusababisha kifo, haswa kwa watu walio na umri wa zaidi ya miaka 50.

Murine typhus

Rickettsia typhi au Rickettsia felis, huambukizwa na viroboto

Paka, panya, na kifaurongo

Kote duniani

Takriban siku 8 hadi 16 baada ya bakteria kuingia mwilini, dalili huanza na zinafanana na zile za homa kali iletwayo na chawa ya mlipuko lakini si kali sana.

Homa kali iletwayo na chawa ya kichaka

Homa kali iletwayo na chawa ya kichaka

Orientia tsutsugamushi (hapo awali, Rickettsia tsutsugamushi), huenezwa na viluwiluwi vya utitiri (vijidudu)

Utitiri (utitiri ndio wanaoeneza maambukizi na pia ndio wenyeji)

Eneo la Asia-Pasifiki, linalozunguka Japani, Korea, Uchina, India, na kaskazini mwa Australia

Takriban siku 6 hadi 21 baada ya bakteria kuingia mwilini, dalili huanza ghafla, zikiwa na homa, baridi, maumivu ya kichwa, na uvimbe wa vinundu vya limfu. Kipele cheusi kinaweza kutokea mahali ambapo funza aling'ata. Upele huonekana siku ya 5 hadi 8.

Homa ya madoa

Homa ya Rock Mountain spotted

R. rickettsii, huenezwa na kupe

Wanyama wagugunaji

Nusu ya Magharibi ya Dunia, ikijumuisha sehemu kubwa ya Marekani (isipokuwa Maine, Hawaii, na Alaska) pamoja na Amerika ya Kati na Kusini.

Takriban siku 3 hadi 12 baada ya bakteria kuingia mwilini, dalili huanza.

Homa ya kupe wa Kiafrika

Rickettsia afrikae, huenezwa na kupe

Ng'ombe

Kusini mwa Jangwa la Sahara na West Indies

Takriban siku 4 hadi 10 baada ya bakteria kuingia mwilini, dalili huanza. Kwa kawaida Kipele cheusi hutokea mahali ambapo kupe aling'ata.

Homa ya madoa ya Mediterania (homa ya boutonneuse)

Rickettsia conorii, huenezwa na kupe wa mbwa

Mbwa

Afrika, India, kusini mwa Ulaya, na eneo la Mashariki ya Kati karibu na Bahari za Mediterania, Nyeusi na Kaspiani

Takriban siku 5 hadi 7 baada ya bakteria kuingia mwilini, dalili huanza. Kipele cheusi kinaweza kutokea mahali ambapo kupe aling'ata.

Riketiosis ya Kaskazini mwa Asia inayoenezwa na kupe

Rickettsia sibirica, huenezwa na kupe

Wanyama wagugunaji

Armenia, Asia ya kati, Siberia, Mongolia, na Uchina

Kipele cheusi kinaweza kutokea mahali ambapo kupe aling'ata.

Homa kali iletwayo na kupe ya Queensland

Rickettsia australis, huenezwa na kupe

Wanyama wagugunaji

Australia

Kipele cheusi kinaweza kutokea mahali ambapo kupe aling'ata.

Rickettsia parkeri rickettsiosis

Rickettsia parkeri, huenezwa na kupe

Wanyama wagugunaji

Kusini mwa Marekani na Amerika Kusini

Takriban siku 2 hadi 10 baada ya bakteria kuingia mwilini, dalili huanza. Kwa kawaida Kipele cheusi hutokea mahali ambapo kupe aling'ata.

Rickettsialpox

Rickettsia akari, huenezwa na utitiri

Panya wa nyumbani

Iligunduliwa mara ya kwanza katika Jiji la New York

Maeneo mengine ya Marekani na Urusi, Korea na Afrika

Kipele kidogo cheusi kinaonekana mahali pa kuumwa na utiriri. Hukua na kuwa kidonda kidogo kinachoacha kovu kinapopona. Karibu wiki 1 baadaye, homa, maumivu ya kichwa, maumivu ya misuli, na upele ulioenea hujitokeza.

Homa ya kupe ya Pwani ya Pasifiki

R. philipii (364D)

Kupe wa Pwani ya Pasifiki (Dermacentor occidentalis)

California

Kwa kawaida upele mweusi hutokea mahali ambapo kupe aliuma, ukifuatiwa na homa, uvimbe wa vinundu vya limfu, maumivu ya kichwa, maumivu ya misuli, na uchovu. Upele ni mdogo sana kuliko homa zingine za madoa.

Ehrlichiosis na anaplasmosis

Monocytic ehrlichiosis

Ehrlichia chaffeensis, huenezwa na kupe, hasa aina ya lone star

Kulungu mkia-mweupe na mamalia wengine

Kusini-mashariki na kusini-kati mwa Marekani

Takriban siku 12 baada ya kung'atwa na kupe, dalili kwa kawaida huanza. Hizi ni pamoja na homa, kibaridi, maumivu ya misuli, udhaifu, kichefuchefu na/au kutapika, kikohozi, maumivu ya kichwa, na hisia ya jumla ya ugonjwa. Upele unaweza kutokea kwenye kiwiliwili, mikono na miguu.

Granulocytic anaplasmosis

Anaplasma phagocytophilum, huenezwa na kupe

Haswa panya na panya wengine wadogo

Nchini Marekani, Kaskazini-mashariki, Atlantiki ya kati, Margaribi kati ya juu, na Pwani ya Magharibi

Ulaya

Takriban siku 12 baada ya kung'atwa na kupe, dalili kwa kawaida huanza. Dalili zake ni pamoja na homa, kibaridi, maumivu ya misuli, udhaifu, kichefuchefu na/au kutapika, kikohozi, maumivu ya kichwa, na hali ya kujisikia mgonjwa kwa ujumla (dhaifu/unyonge).

Homa ya Q

Homa ya Q

Coxiella burnetii, huenezwa kwa kuvuta matone ya hewa yaliyoambukizwa yenye bakteria au kwa kunywa maziwa mabichi yaliyochafuliwa

Kondoo, ng'ombe na mbuzi

Kote duniani

Takriban siku 9 hadi 28 baada ya bakteria kuingia mwilini, dalili huanza kwa ghafla. Dalili zake ni pamoja na homa, maumivu makali ya kichwa, kibaridi, udhaifu uliokithiri, maumivu ya misuli, kukosa hamu ya kula, kutokwa jasho, kikohozi kisicho na makohozi, maumivu ya kifua, na upungufu wa pumzi (unaosababishwa na nimonia), lakini hakuna upele.