Kuvimba Wakati wa Ujauzito Uliochelewa

NaEmily E. Bunce, MD, Wake Forest School of Medicine;
Robert P. Heine, MD, Wake Forest School of Medicine
Imekaguliwa naSusan L. Hendrix, DO, Michigan State University College of Osteopathic Medicine
Imepitiwa/Imerekebishwa Imebadilishwa Jul 2023
v1536155_sw

Kadri ujauzito unavyoendelea, maji yanaweza kujikusanya kwenye tishu, kwa kawaida kwenye miguu, vifundo vya miguu na sehemu ya chini ya miguu, na kuzifanya zivimbe na kuonekana kuwa nene. Mkusanyiko fulani wa maji wakati wa ujauzito ni wa kawaida, hasa wakati wa trimesta ya 3. Hali hii huitwa uvimbe (edema). Wakati mwingine, vidole pia huwa na uvimbe mdogo. Iwapo uvimbe ni mdogo zaidi mikononi au iwapo uso umevimba, mwanamke huyo anapaswa kutathminiwa na daktari.

Majimaji hujikusanya wakati wa ujauzito kwa sababu tezi za adrenali hutoa homoni nyingi zaidi zinazofanya mwili kuhifadhi majimaji(aldosteroni na kotisoli). Majimaji pia hujikusanya kwa kuwa uterasi inayoendelea kuwa kubwa hutatiza mtiririko wa damu kutoka miguuni hadi kwenye moyo. Kwa sababu hiyo, majimaji hurudi kwenye mishipa ya miguu na kuingia kwenye tishu zilizo karibu.

Sababu za Kuvimba Wakati wa Ujauzito Uliochelewa

Sababu za kawaida

Kwa kawaida wakati wa ujauzito, uvimbe ni

  • Kawaida, uvimbe unaohusishwa na ujauzito

Sababu zisizo za kawaida

Kwa nadra, uvimbe wakati wa ujauzito kutokana na tatizo hatari (tazama jedwali la ). Matatizo kama hayo yanaweza kuwa hatari. Yanajumuisha yafuatayo;

Katika preklampsia, ugonjwa ambao hutokea wakati wa ujauzito pekee, shinikizo la damu na viwango vya protini kwenye mkojo huongezeka. Majimaji yanaweza kujikusanya, na kusababisha uvimbe kwenye uso, mikononi, au miguuni na kuongeza uzito zaidi; wanawake wengi, lakini si wote, walio na preeclampsia huwa na uvimbe. Ikiwa imekithiri, preeclampsia inaweza kuharibu viungo, kama vile ubongo, figo, mapafu, au ini na kusababisha matatizo kwa mtoto.

Katika thrombosis ya mshipa wa ndani, vidonge vya damu huganda kwenye mishipa iliyo ndani kabisa ya sehemu ya mwili, mara nyingi kwenye miguu. Ujauzito huongeza hatari ya ugonjwa huu kwa njia kadhaa. Wakati wa ujauzito, mwili hutoa protini nyingi zaidi zinazosaidia kuganda kwa damu (vipengele vya kuganda), labda vinavyokusudiwa kuzuia kutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua. Pia, mabadiliko wakati wa ujauzito husababisha damu kurudi kwenye mishipa, na kuongeza uwezekano wa kuganda kwa damu. Iwapo mwanamke mjamzito hatembei sana, kuna uwezekano mkubwa zaidi wa damu kurudi kwenye mishipa ya miguu na kuganda. Vidonge vilivyoganda vinaweza kutatiza mtiririko wa damu. Iwapo damu iliyoganda itavunjika, inaweza kusafiri kupitia mfumo wa damu hadi kwenye mapafu, na kuzuia mtiririko wa damu pale. Kizuizi hiki (kinachoitwa embolism ya mapafu) ni hatari kwa maisha.

Ugonjwa wa moyo kabla au baada ya kujifungua ni hali adimu lakini mbaya inayosababisha upungufu wa pumzi na uchovu, pamoja na uvimbe.

Viashiria vya hatari

Hatari ya preeclampsia, thrombosis ya mishipa ya ndani, na ugonjwa wa moyo kabla au baada ya kujifungua huongezeka kutokana na hali mbalimbali (viashiria vya hatari).

Viashiria vikubwa vya hatari kwa preeclampsia vinajumuisha

Viashiria vya wastani vya hatari kwa preeclampsia ni pamoja na

  • Ujauzito wa kwanza

  • Unene kupita kiasi

  • Historia ya familia ya preeclampsia

  • Asili ya Kiafrika

  • Mapato ya chini

  • Umri wa miaka 35 au zaidi

  • Utungishaji mimba kwenye maabara

  • Vigezo vya historia ya kibinafsi (kwa mfano, watoto wachanga waliozaliwa wakiwa na uzito mdogo au wadogo kwa umri wa ujauzito, matokeo mabaya ya ujauzito uliopita, zaidi ya miaka 10 kati ya ujauzito mmoja na mwingine)

Kwa thrombosis ya mishipa ya ndani, viashiria vya hatari ni pamoja na vifuatavyo:

  • Kipindi cha awali cha thrombosis ya mishipa ya ndani

  • Matatizo ya kuganda kwa damu ya kurithiwa

  • Jeraha kwa mshipa wa mguu ambalo huzuia damu kutiririka kama kawaida

  • Ugonjwa ambao husababisha damu kuganda zaidi, kama vile saratani au matatizo ya figo au moyo

  • Uvutaji sigara

  • Kutoweza kusogea, kama inavyoweza kutokea baada ya ugonjwa au upasuaji

  • Unene kupita kiasi

Kwa ugonjwa wa moyo kabla au baada ya kujifungua, viashiria vya hatari ni pamoja na vifuatavyo:

Tathimini ya Kuvimba Wakati wa Ujauzito Uliochelewa

Lazima madaktari wahakikishe kuwa hakuna thrombosis ya mishipa ya ndani, preeclampsia, ugonjwa wa moyo, na sababu zingine zinazowezekana kabla ya kufanya utambuzi wa uvimbe wa kawaida wa kifisiolojia.

Ishara za onyo

Kwa wanawake wajawazito wenye miguu iliyovimba, dalili zifuatazo husababisha wasiwasi:

  • Uvimbe wa wastani au mkali kwenye mikono (mikono huonekana kuvimba sana na/au pete haiwezi kutolewa kwenye kidole)

  • Uvimbe ambao huongezeka ghafla katika sehemu yoyote ya mwili

  • Uvimbe katika mguu mmoja au sehemu ya nyuma ya mguu, hasa ikiwa eneo hilo lina joto, ni jekundu, na/au laini au mwanamke ana homa

  • Shinikizo la damu ambalo ni 140/90 mm Hg au zaidi

  • Maumivu makali ya kichwa yanayoendelea, mabadiliko ya uwezo wa kuona, kuchanganyikiwa, maumivu makali ya tumbo la juu, au ugumu wa kupumua—dalili ambazo huenda zimesababishwa na preeclampsia

  • Maumivu makali ya kifua au ugumu wa kupumua—thrombosis ya mishipa ya ndani

Wakati wa kuona daktari

Wanawake wanapaswa kwenda hospitalini mara moja ikiwa wana dalili zozote za onyo.

Wanawake wasio na dalili za onyo wanapaswa kumuona daktari, lakini kuchelewa kwa siku kadhaa kwa kawaida hakuna madhara.

Anachofanya daktari

Madaktari kwanza huuliza maswali kuhusu uvimbe na dalili zingine na kuhusu historia ya matibabu. Kisha madaktari hufanya uchunguzi wa kimwili. Kile ambacho wanapata wakati wa historia na uchunguzi wa kimwili mara nyingi huonyesha kisababishi cha uvimbe na uchunguzi unaopaswa kufanywa (tazama jedwali la ).

Madaktari huuliza yafuatayo:

  • Wakati ambapo uvimbe ulianza

  • Muda ambao uvimbe umekuwepo

  • Ikiwa shughuli yoyote (kama vile kulala upande wa kushoto)inaupunguza au kuuzidisha

Madaktari pia huuliza kuhusu hali zinazoongeza hatari ya kupata thrombosis ya mishipa ya ndani, preklampsia na ugonjwa wa moyo kabla au baada ya kujifungua.

Wanawake huulizwa kuhusu dalili zingine, ambazo zinaweza kuashiria chanzo. Wanaulizwa iwapo wamewahi kupata thrombosis ya mishipa ya ndani, embolism ya mapafu (pulmonary embolism), preklampsia, shinikio la juu la damu, au matatizo ya moyo, ikiwa ni pamoja na ugonjwa wa moyo na mishipa (cardiomyopathy).

Wakati wa uchunguzi wa kimwili, madaktari hutafuta ushahidi wa chanzo kikubwa cha uvimbe. Ili kuangalia dalili za preklampsia, madaktari hupima shinikizo la damu, husikiza moyo na mapafu, na wanaweza kuangalia hisia za mwanamke na kuangalia nyuma ya macho yake kwa kutumia ophthalmoskopu (kifaa kinachoshikiliwa kwa mkono ambacho hufanana na tochi ndogo). Madaktari pia hutafuta maeneo yenye uvimbe, hasa miguuni, mikononi, na kwenye uso. Sehemu yoyote iliyovimba huchunguzwa ili kuona kama ni nyekundu, yenye joto, au laini.

Jedwali
Jedwali

Kupima

Ikiwa preklampsia inashukiwa, kiwango cha protini hupimwa katika sampuli ya mkojo na hesabu kamili ya damu, elektroliti, na vipimo vya utendaji kazi wa figo na ini hufanywa. Shinikizo la juu la damu linaloanza pamoja na kiwango cha juu cha protini kwenye mkojo huashiria preklampsia. Ikiwa utambuzi hauko wazi, mwanamke huyo huombwa kuchukua mkojo wake kwa saa 24, na protini hupimwa katika kiwango hicho cha mkojo. Shinikizo la juu la damu pamoja na maumivu ya kichwa, mabadiliko ya uwezo wa kuona, maumivu ya tumbo, au matokeo yasiyo ya kawaida ya vipimo vya damu au mkojo yanaweza pia kuashiria preklampsia.

Iwapo inashukiwa kuwa kuna thrombosis ya mishipa ya kina, ultrasonografia ya Doppler ya mguu ambao umeathiriwa hufanywa. Kipimo hiki kinaweza kuonyesha usumbufu katika mtiririko wa damu unaosababishwa na kuganda kwa damu kwenye mishipa ya miguu.

Iwapo ugonjwa wa moyo kabla au baada ya kujifungua unashukiwa kuwepo, uchunguzi wa elektrokadi, eksirei ya kifua, uchunguzi wa echokadi, na vipimo vya damu ili kuangalia utendakazi wa moyo hufanywa.

Matibabu ya Kuvimba Wakati wa Ujauzito Uliochelewa

Uvimbe unapotokana na ugonjwa, ugonjwa huo hutibiwa.

Uvimbe unaotokea kwa kawaida wakati wa ujauzito unaweza kupunguzwa kwa kufanya mambo yafuatayo:

  • Kulala kwenye upande wa kushoto, ambao husogeza uterasi kutoka kwenye mshipa mkubwa unaorudisha damu moyoni (vena cava ya chini)

  • Kupumzika mara kwa mara huku miguu ikiwa imeinuliwa

  • Kuvaa soksi zenye mpira unaoshikilia

  • Kuvaa nguo zisizobana zisizozuia mtiririko wa damu, hasa miguuni (kwa mfano, kutovaa soksi au stokingi zenye mikanda iliyobana kuzunguka vifundo vya miguu au sehemu ya nyuma ya miguu)

Mambo Muhimu

  • Baadhi ya uvimbe kwenye miguu na vifundo vya miguu ni wa kawaida (kifiziolojia) wakati wa ujauzito na hutokea wakati wa trimesta ya 3.

  • Madaktari wanaweza kutambua sababu kuu za uvimbe kulingana na matokeo ya uchunguzi wa kimwili, kipimo cha shinikizo la damu, vipimo vya damu na mkojo, na wakati mwingine ultrasonografia.

  • Ikiwa mimba ndiyo chanzo, uvimbe unaweza kupunguzwa kwa kulala upande wa kushoto, kuinua miguu mara kwa mara, kuvaa soksi zinazosaidia na kuvaa nguo zisizozuia mtiririko wa damu.