Uvimbe wa ovari usio na kansa unajumuisha uvimbe uliojaa maji (hasa unaotokana na mzunguko wa hedhi) na uvimbe wa nyama, ukiwemo uvimbe usio na kansa.
Mara nyingi uvimbe uliojaa maji na uvimbe wa kawaida usio na kansa hausababishi dalili zozote, lakini baadhi husababisha maumivu au shinikizo katika eneo la fupanyonga.
Madaktari wanaweza kugundua uvimbe wakati wa uchunguzi wa fupanyonga, kisha kutumia kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti kuthibitisha utambuzi huo.
Baadhi ya uvimbe uliojaa maji hutoweka wenyewe.
Uvimbe uliojaa maji au uvimbe wa kawaida unaweza kuondolewa kupitia chale moja au zaidi ndogo, au chale moja kubwa kwenye fumbatio, na wakati mwingine ni lazima ovari iliyoathirika iondolewe pia.
This illustration shows a cyst on the ovary (circled).
VERONIKA ZAKHAROVA/SCIENCE PHOTO LIBRARY
Uvimbe wa ovari uliojaa maji ni vifuko vilivyojaa kiowevu ambavyo hutokea ndani au juu ya ovari. Uvimbe wa aina hii ni wa kawaida kiasi. Mwingi hauna kansa na hutoweka wenyewe. Kansa ya ovari ina uwezekano mkubwa wa kutokea kwa wanawake wenye umri wa zaidi ya miaka 50.
Uvimbe wa Ovari Uliojaa Maji Unaotenda
Uvimbe uliojaa maji unaotokana na mzunguko wa hedhi hutokana na vijishimo vyenye majimaji (kinyweleo) katika ovari. Kila kinyweleo huwa na yai moja. Kwa kawaida, wakati wa kila mzunguko wa hedhi, kinyeleo hutoa yai moja, na kinyweleo hicho hutoweka baada ya yai kutolewa. Hata hivyo, yai lisipotolewa, ukubwa wa kinyweleo hicho unaweza kuendelea kuongezeka hicyo kuunda uvimbe mkubwa zaidi.
Takriban theluthi moja ya wanawake walio katika hali ya kabla ya kukoma hedhi hupata uvimbe uliojaa maji. Uvimbe uliojaa maji unaotokana na mzunguko wa hedhi mara chache hutokea baada ya ukomo wa hedhi.
Kuna aina mbili za uvimbe uliojaa maji unaotokana na mzunguko wa hedhi:
Uvimbe wa kinyweleo uliojaa maji: Uvimbe huu huundwa wakati yai linapokua kwenye kinyweleo.
Uvimbe uliojaa maji wa luteamu ya kopasi: Uvimbe huu hukua kutokana na nyenzo inayoundwa baada ya kinyweleo kupasuka na kutoa yai lake. Nyenzo hiyo inaitwa luteamu ya kopasi. Uvimbe uliojaa maji wa luteamu ya kopasi unaweza kutokwa na damu na kusababisha ovari kuvimba au unaweza kupasuka. Uvimbe uliojaa maji ukipasuka, kiowevu huingia kwenye fumbatio (utobo wa tumbo) na inaweza kusababisha maumivu makali sana.
Uvimbe mwingi uliojaa maji unaotokana na mzunguko wa hedhi huwa na kipenyo cha chini ya inchi 2/3 (sentimita 1.5). Chache ni inchi 2 (sentimita 5) au zaidi.
Uvimbe uliojaa maji unaotokana na mzunguko wa hedhi kwa kawaida hutoweka wenyewe baada ya siku au wiki chache.
Uvimbe wa ovari tulivu
Kwa kawaida uvimbe wa ovari usio na kansa hukua polepole na mara chache huwa yenye kansa. Unaotokea mara kwa mara ni pamoja na ufuatao:
Teratoma zisizo na kansa (uvimbe kwenye ngozi): Uvimbe huu wa kawaida mara nyingi hutokea kutokana na kwa safu zote tatu za tishu kwenye kiinitete (zinazoitwa safu za seli zazi). Viungo vyote huundwa kutoka kwenye tishu hizi. Kwa hivyo, teratoma zinaweza kuwa na tishu kutoka kwa nyenzo nyingine, kama vile neva, tezi na ngozi.
Uvimbe wa nyuzi: Uvimbe huu wa kawaida ni uvimbe wa nyama ulioundwa na tishu zinazounganisha (tishu zinazoshikilia nyenzo pamoja). Uvimbe wa nyuzi hukua polepole na kwa kawaida huwa na kipenyo cha chini ya inchi 3 (takribani sentimita 7). Kwa kawaida hutokea upande mmoja tu.
Saitadenoma: Uvimbe huu uliojaa kiowevu hutokea kwenye sehemu ya nje ya ovari na huwa na baadhi ya tishu kutoka kwenye tezi zilizo ndani ya ovari.
Dalili
Uvimbe mwingi uliojaa maji unaotokana na mzunguko wa hedhi na uvimbe wa ovari usio na kansa hausababishi dalili zozote. Lakini baadhi husababisha maumivu ya fupanyonga makali ya kwenda na kurudi au ya muda mfupi. Wakati mwingine husababisha matatizo ya hedhi. Wanawake wachache huhisi maumivu ndani kabisa ya fumbatio wakati wa tendo la ndoa.
Baadhi ya uvimbe uliojaa maji hutoa homoni zinazoathiri hedhi. Kwa hivyo, hedhi inaweza kuwa isiyo ya kawaida au nzito kuliko kawaida. Madoa yanaweza kutokea wakati wa hedhi. Kwa wanawake waliokoma hedhi, uvimbe kama huo unaweza kusababisha kuvuja damu ukeni.
Ikiwa uvimbe uliojaa maji wa luteamu ya kopasi utatokwa na damu, hali hii inaweza kusababisha maumivu au uchungu katika eneo la fupanyonga.
Mara kwa mara, maumivu makali ya ghafla ya fumbatio hutokea kwa sababu uvimbe mkubwa uliojaa maji au uvimbe wa nyama husababisha ovari kusongoa (tatizo linaloitwa msokoto wa adnexal).
Mara chache, kiowevu hujikusanya kwenye fumbatio (ugonjwa wa tumbo kuvimba kwa kujaa maji) au kwenye mapafu (kuvimba kwa pleura) kwa wanawake wenye uvimbe wa nyuzi au kansa ya ovari. Ugonjwa wa tumbo kujaa maji unaweza kusababisha hisia ya shinikizo au uzito kwenye fumbatio.
Utambuzi wa Ugonjwa
Uchunguzi wa Fupanyonga
Kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti kwenye fupanyonga
Wakati mwingine vipimo vya damu
Wakati uvimbe wa kawaida au uvimbe wa ovari uliojaa maji hausababishi dalili, madaktari wakati mwingine hugundua dalili hizo wakati wa uchunguzi wa kawaida wa kifua cha fupanyonga. Mara nyingi, hugunduliwa wakati kipimo cha picha (kama vile kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti) kinapofanywa kwa sababu nyingine. Ikiwa mwanamke ana dalili, madaktari wanaweza kufanya uchunguzi wa fupanyonga au kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti ili kutathmini uvimbe wa ovari.
Kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti ili kutathmini ovari kwa kawaida hufanywa kwa kutumia kifaa cha kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti kinachoingizwa kwenye uke (upigaji picha kwa mawimbi ya sauti ndani ya uke). Wakati mwingine MRI hufanywa ikiwa matokeo ya kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti hakitoi utambuzi.
Kipimo cha ujauzito hufanywa ili kuondoa fikira ya kuwa ni mimba, ikiwa ni pamoja na ujauzito ulio nje ya uterasi (ujauzito wa nje ya kizazi).
Ikiwa picha inaonyesha kwamba uvimbe huo unaweza kuwa wa kansa au ikiwa kuna ugonjwa wa tumbo kuvimba kwa kujaa maji, madaktari huondoa uvimbe huo na kuuchunguza kwa hadubini. Laparoskopi, inayoingizwa kupitia chale dogo chini ya kitovu, inaweza kutumika kuchunguza ovari na kuondoa uvimbe.
Ikiwa madaktari wanashuku kansa ya ovari, huwa wanafanya vipimo vya damu ili kuangalia dutu zinazoitwa alama za uvimbe, ambavyo vinaweza kuonekana kwenye damu au vinaweza kuongezeka wakati kuna baadhi ya kansa. Hata hivyo, vipimo hivi havitegemewi kwa utambuzi. Ni muhimu zaidi kwa kufuatilia jinsi wanawake wenye kansa ya ovari wanavyoitikia matibabu
Matibabu
Kwa baadhi ya uvimbe uliojaa maji, ufuatiliaji wa mara kwa mara kwa kutumia kipimo cha Kipimo cha picha kwa kutumia mawimbi ya sauti ndani ya uke
Wakati mwingine upasuaji
Uvimbe wa ovari uliojaa maji
Uvimbe wa ovari uliojaa maji ambao ni kifuko kilichojaa kiowevu kilichozungukwa na tishu nyembamba na laini huitwa uvimbe wa kawaida uliojaa maji. Aina hii ya uvimbe wa ovari uliojaa maji haielekei kuwa ya kansa.
Baadhi ya uvimbe wa ovari uliojaa maji una sifa nyingine kwenye kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti, kama vile kifuko ambacho kimegawanywa katika sehemu 2. Aina nyingi haina kansa. Kwa kawaida Kipimo cha picha kwa kutumia mawimbi ya sauti ndani ya uke kwenye uke hurudiwa mara kwa mara ili kubaini ikiwa uvimbe uliojaa maji umebadilika ukubwa au umetoweka.
Uvimbe wa ovari
Uvimbe usio na kansa, kama vile uvimbe wa nyuzi na saitadenomasi, unahitaji matibabu.
Ikiwa uvimbe una vipengele kwenye kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti vinavyoongeza wasiwasi wa kansa ya ovari kwenye kipimo cha picha kinachotumia mawimbi ya sauti (kama vile uvimbe wa nyama ambao ni mgumu kabisa au kiasi), upasuaji hufanywa ili kutathmini uvimbe na, ikiwezekana, kuuondoa. Mojawapo ya taratibu zifuatazo hufanywa:
Laparoskopia
Laparotomia
Laparoskopia inahitaji chale ndogo moja au zaidi kwenye fumbatio. Inafanywa hospitalini na kwa kawaida huhitaji ganzi ya mwili mzima. Hata hivyo, huenda wanawake wasilazimike kusalia usiku kucha.
Laparotomia ni sawa lakini inahitaji chale kubwa na kusalia hospitalini usiku kucha.
Utaratibu unaotumika hutegemea ukubwa wa uvimbe na ikiwa viungo vingine vimeathiriwa.
Ikiwezekana kitaalamu, madaktari wanalenga kuokoa ovari kwa kuondoa uvimbe uliojaa maji pekee (cystectomy).
Kuondolewa kwa ovari iliyoathiriwa (oophorectomy) ni muhimu kwa yafuatayo:
Uvimbe wa nyuzi au uvimbe mwingine mgumu ikiwa uvimbe huo hauwezi kuondolewa kwa cystectomy
Sistadenoma
Teratoma za uvimbe uliojaa maji ambazo ni kubwa kuliko inchi 4
Uvimbe uliojaa maji ambao hauwezi kutenganishwa na ovari kupitia upasuaji
Uvimbe mwingi uliojaa maji unaotokea kwa wanawake waliokoma hedhi na ambao ni mkubwa kuliko inchi 2