Homa ya mafua (Mafua)

NaSophie Katz, MD, MPH, Vanderbilt University Medical Center
Imekaguliwa naBrenda L. Tesini, MD, University of Rochester School of Medicine and Dentistry
Imepitiwa/Imerekebishwa May 2024 | Imebadilishwa Apr 2025
v788616_sw

Homa ya mafua (mafua) ni maambukizi ya virusi kwenye mapafu na njia za hewa kupitia mojawapo ya virusi wanaosababisha mafua. Inasababisha homa, kamasi, kikohozi, kukohoa, maumivu ya kichwa, maumivu ya misuli (homa ya misuli), na homa kwa ujumla (uchovu).

  • Virusi vinavyosambazwa kwa kuvuta matone yaliyotoka katika mwili wa aliyeambukizwa kwa kupiga chafya au kukohoa au kugusa moja kwa moja majimaji ya puani ya mtu aliyeathiriwa.

  • Mara nyingi mafua huanza kwa kuhisi baridi, ikifuatiwa na homa, maumivu ya misuli, maumivu ya kichwa, kikohozi, kukohoa, kamasi na kuhisi homa kwa ujumla.

  • Kwa kawaida mafua hutambuliwa kulingana na dalili.

  • Kupumzika, kunywa maji mengi na kuepuka kufanya kazi ngumu kunaweza kusaidia watu kupona, vilevile kutumia vituliza maumivu, dawa za kuzibua njia za pua na wakati mwingine dawa za kuzuia virusi.

  • Chanjo ya mafua ya kila mwaka ni njia bora ya kuzuia mafua.

Mafua ni tofauti kabisa na mafua ya kawaida. Husababishwa na virusi tofauti na huonyesha dalili ambazo ni kali zaidi. Pia, mafua huathiri zaidi seli za ndani kwenye njia ya upumuaji.

Uenezaji wa influenza

Virusi vya mafua husambazwa kwa

  • Kuvuta matone yaliyotoka katika mwili wa aliyeambukizwa kwa kupiga chafya au kukohoa

  • Kugusa moja kwa moja majimaji ya puani ya mtu aliyeathiriwa

  • Kushika vifaa vya nyumbani ambavyo vimeguswa mtu aliyeambukizwa au majimaji ya mtu aliyeathiriwa

Aina za mafua na mikazo

Kuna aina 3 za virusi vya mafua:

  • Aina A

  • Aina B

  • Aina C

Kuna aina tofauti kwenye aina kuu virusi vya mafua za A na B lakini vyote viwili vinasababisha homa sawa. Aina tofauti zinasababisha mlipuko wa kawaida wa msimu wa mafua. Aina ya C haisababishi homa ya kawaida homa ya mafua.

Aina A husababisha hali za mafua (kwa kawaida zaidi ya asilimia 70 kwenye msimu wa kawaida) na nyinginezo husababishwa na aina B. Mafua ya aina C hutolea mara chache, hasa kwa watoto.

Aina ya virusi vya mafua vinavyosababisha mlipuko hubadilika taratibu, kwa hivyo kila mwaka virusi vya mafua huwa tofauti kidogo na mwaka uliotangulia. Mara kwa mara hubadilika sana na kusababisha chanjo yenye ufanisi ya awali isifanye kazi tena.

Aina ya mafua ya aina ya A hupewa jina kulingana na aina husika ya safu mbili za protini zilizo kwenye mwili wa virusi. Protini ni H (ikiashiria hemaglutini) na N (ikiwakilisha neuraminidase). Kuna aina 18 tofauti za protini H na aina 11 za protini N. Kwa hivyo, aina husika inaweza kuitwa Mafua A, H1N1. Aina ya H1N1 ndiyo ilisababisha aina ya janga lililoitwa mafua ya nguruwe mwaka 2009 hadi 2010. (Janga hili ni mlipuko mkubwa ulimwenguni.) Hivi majuzi, aina ya H3N2 imekuwa ikisababisha mojawapo ya maambukizi nchini Marekani.

Jina la aina mara nyingi linaakisi aina yake ndogo, mahali ilikotokea kwa mara ya kwanza (kwa mfano, mafua ya Hong Kong) au mnyama (kwa mfano mafua ya nguruwe) na mwaka yalipotambuliwa.

Magonjwa ya mafua na magonjwa ya milipuko

Katika mlipuko wa mafua, watu wengi wanaumwa ndani ya kipindi kifupi. Kila mwaka, duniani kote milipuko inayosambaa sehemu nyingi ya mafua hutokea mwishoni majira ya kupukutika au mwanzoni mwa majira ya baridi katika hali ya hewa ya baridi kiasi (huitwa milipuko ya kimsimu). Milipuko ya mafua inaweza kutokea katika mawimbi mawili:

  • Kwanza, kwa wanafunzi wadogo na watu wanaoishi nao

  • Pili, kwa wanaokaa nyumbani kwa kuda mrefu au ambao wanaishi katika nyumba za utunzaji wa muda mrefu, hasa wazee.

Katika kila mlipuko, mara nyingi aina moja ya virusi vya mafua ndiyo husababisha ugonjwa.

Janga la mafua ni mlipuko unaosambaa katika eneo kubwa, hasa katika mabara na wakati mwingine ulimwenguni kote. Kumekuwa na majanga makubwa 6 tu ya mafua tangu 1889. Janga la mafua linaleta wasiwasi kwa sababu mara nyingi linatokea wakati kumekuwa na mabadiliko makubwa kuliko kawaida katika aina ya virusi vya mafua. Mabadiliko hayo yanapotokea, aina hiyo ya mafua inaweza kuathiri watu wengi zaidi na kusababisha ugonjwa mkali zaidi. Hatari ya kifo ni kubwa zaidi. Igawa hakuna anayejua kwa hakika, wanasayansi wanafikiri kuwa janga la mafua la mwaka 1918 limesababisha vifo milioni 30 hadi 50 ulimwenguni kote, ikiwa ni pamoja na vifo 675,000 nchini Marekani.

Mwaka 2009 hadi 2010, kulikuwa na mlipuko wa aina ya H1N1 ya mafua (angalia Aina kuu na ndogo za mafua), ambao ulisambaa sehemu kubwa na ulichukuliwa kuwa janga. Aina hii ilikuwa na muunganiko wa jeni za nguruwe (nguruwe), ndege na virusi vya mafua ya binadamu. Kwa sababu ripoti za kwanza zimezingatia jeni za nguruwe, umma uliita "mafua ya nguruwe," ingawa hayakupatikana moja kwa moja kutoka kwa nguruwe. Watu walipata maambukizi haya ya virusi vya mafua kutoka kwa watu walioambukizwa (kusambaza kati ya mtu na mtu) kama vile mafua ya kawaida.

Dalili za Mafua

Dalili za Mafua huanza siku 1 hadi 4 baada ya maambukizi na yanaweza kuanza ghafla. Kuhisi baridi mara nyingi ni dalili ya kwanza. Kwa kawaida homa hutokea katika siku kadhaa za kwanza, wakati mwingine hufika Farenihaiti 102 hadi 103° (takribani Sentigredi 39°). Watu wengi huhisi homa sana, udhaifu na kuchoka na husalia kitandani kwa siku kadhaa. Huhisi maumivu mwili mzima, hasa mgongoni na miguuni. Maumivu ya kichwa huwa makali, pamoja na kuuma sehemu zinazozunguka na nyuma ya macho. Mwangaza angavu unaweza kuongeza maumivu ya kichwa.

Mwanzoni, dalili katika njia ya upumuaji zinaweza kuwa kiasi. Zinaweza kujumuisha kikohozi, maumivu sehemu ya kifua, kikohozi kikavu na kamasi. Baadaye, kukohoa kunaweza kuzidi na kusababisha kikohozi (kohozi).

Ngozi inaweza kuwa na joto na iliyovutika, hasa usoni. Koo na mdomo unaweza kuwa mwekundu, macho yanaweza kuwa na dalili ya machozi na rangi nyeupe machoni inaweza kuwa kama alama za damu. Watu, hasa watoto wanaweza kupata kichefuchefu na kutapika. Watu kadhaa hupoteza hisia ya kunusa kwa siku au wiki kadhaa. Mara chache, inaweza kupotea kabisa.

Dalili nyingi huonekana zaidi baada ya siku 2 au 3. Hata hivyo, wakati mwingine homa hudumu hadi siku 5. Kukohoa, udhaifu, kutokwa na jasho na uchovu vinaweza kuendelea kwa siku kadhaa au mara chache wiki kadhaa. Muwasho kiasi katika njia ya hewa, ambao unaweza kusababisha kupungua kwa muda au nguvu ambazo mtu anaweza kuzitumia katika mazoezi au kupumua kwa shida huchukua wiki 6 hadi 8 hadi kuisha kabisa.

Matatizo

Maradhi yanayotokea mara kwa mara ya mafua ni

Kwa nimonia ya virusi, virusi vya mafua vinasambaa vyenyewe kwenye mapafu. Baadhi ya watu wenye nimonia ya virusi pia huambukizwa na bakteria na huweza kupata nimonia ya bakteria; hii inaweza kutokea bakteria (kama vile pneumococci au staphylococci) hushambulia kingamwili dhoofu za mtu. Watu wanaweza kuwa na kikohozi kilichokithiri, kupumua kwa shida, homa za mara jwa mara na wakati mwingine kikohozi huwa na damu au usaha.

Watu walio katika hatari kubwa ya kupata maradhi na kifo kutokana na mafua ni pamoja na

  • Watoto walio chini ya umri wa miaka 5; hasa watoto walio na umri wa chini ya miaka 2 wapo katika hatari kubwa

  • Watu wazima walio na umri wa zaidi ya miaka 65

  • Watu walio na magonjwa sugu ya kimatibabu (hasa ugonjwa wa kisukari na matatizo yanayoathiri moyo, mapafu, figo, maini au mfumo wa kingamwili)

  • Watu walio na uzito uliokithiri (kielezo cha uzito wa mwili (BMI) ya 40 au zaidi)

  • Wanawake walio katika awamu ya pili au ya tatu ya ujauzito na hadi walio na wiki 2 baada ya kujifungua

  • Watu wenye magonjwa yanayoongeza uwezekano wao wa kupaliwa na majimaji ya kinywani, kama vile kiharusi au magonjwa mengine yanayohusu neva ambayo yanasababisha udhaifu na magonjwa ya mshtuko

Utambuzi wa Mafua

  • Tathmini ya daktari

  • Wakati mwingine vipimo vya sampuli ya damu au majimaji ya njia ya upumuaji

  • Wakati mwingine eksirei ya kifua na kipimo cha kiwango cha oksijeni kwenye damu

Kwa sababu watu wengi wanafahamu dalili za mafua na kwa kuwa mafua hutokea kama mlipuko, mara nyingi hutambuliwa kwa usahihi na mtu aliye nayo au na mwanafamilia. Ukali wa dalili na uwepo wa homa kali pamoja na maumivu mwilini husaidia kutofautisha mafua na mafua ya kawaida, hasa homa inapotokea wakati wa mlipuko wa mafua. Ni vigumu sana kutambua kwa usahihi mafua kwa dalili pekee wakati hakuna mlipuko unaotokea.

Vipimo vya sampuli za majimaji ya njia ya upumuaji vinaweza kutumika kutambua virusi vya mafua. Vipimo vya damu vinaweza kusaidia kubaini kiwango cha homa aliyonayo mtu baada ya kuambukizwa. Vipimo hivyo hufanyika hasa watu wanaoonekana wanaumwa sana au daktari anapohisi chanzo kingine cha dalili. Baadhi ya vipimo vinaweza kufanyika katika ofisi ya daktari.

Ikiwa madaktari wanashuku kuwa mtu amepata nimonia, watapima eksirei na viwango vya oksijeni kwenye damu kwa kutumia kitambuzi kinachowekwa kwenye kidole (kipimo cha oksijeni katika damu).

Matibabu ya Mafua

  • Pumzika na utumie vimiminika vya kutosha.

Tiba kuu ya mafua ni kupumzika vya kutosha, kunywa vimiminika kwa kiasi kingi na kuepuka kufanya kazi ngumu. Shughuli za kawaida zinaweza kuendelea saa 24 hadi 48 baada ya joto la mwili kurejea katika hali ya kawaida, lakini kwa watu wengi huchukua siku kadhaa kurejea.

Watu wanaweza kutibu homa na maumivu kwa kutumia acetaminophen au dawa za kupunguza kuvimba zisizo na steroidi (NSAID), kama vile aspirini au ibuprofeni. Kwa sababu ya hatari ya Ugonjwa wa Reye, watoto na vijana wadogo (wenye umri wa miaka 18 au chini yake) hawapaswi kutumia aspirini. Acetaminophen na ibuprofeni zinaweza kutumika kutibu watoto ikihitajika. Hatua nyingine kama zilivyoorodheshwa kwenye kutibu mafua ya kawaida, kama vile dawa za kuzibua njia za puani zilizoziba zinaweza kusaidia kupunguza dalili.

Dawa za kupambana na virusi (oseltamivir, zanamivir, baloxavir marboxil na peramivir) hufaa kutibu watu wenye mafua. Hata hivyo, dawa hizi hufanya kazi tu zikitumiwa katika siku ya kwanza au ya pili baada ya dalili kuanza. Dawa za kupambana na virusi hupunguza ukali wa dalili na kufupisha muda wa homa pamoja na muda wa kurejea katika shughuli za kawaida, lakini ni kwa takribani siku moja. Hata hivyo, dawa hizi zinafaa zaidi kwa baadhi ya watu.

Aina ya dawa zitakazotumika hutokana na aina husika ya virusi vya mafua vinavyosababisha maambukizi. Oseltamivir na baloxavir marboxil, humezwa kupitia mdomo pamoja na zanamivir, ambayo huvutwa, hufaa dhidi ya mafua ya virusi vya aina A na B. Oseltamivir zinaweza kutumiwa kwa watoto wenye umri wa mwaka 1. Zanamivir zinaweza kutumiwa na watu wazima na watoto walio na umri wa miaka 7 na zaidi baloxavir zinaweza kutumiwa na watoto wenye umri wa miaka 12 na zaidi. Peramivir inatolewa kupitia sindano kwenye mishipa ya damu (kwa njia ya mishipa) kama dozi ya mara moja na inaweza kutumiwa na watu wazima na watoto wenye umri wa miaka 2 na zaidi ambao hawawezi kuvumilia dawa zinazomezwa kupitia mdomo au kivuta pumzi.

Iwapo kutakuwa na maambukizi ya bakteria, madaktari watakuandikia viua vijasumu.

Uzuiaji wa Mafua

Kuzuia ni pamoja na

  • Chanjo kila mwaka kwa kila mtoto mwenye umri wa miezi 6 au zaidi (kwa kufuata baadhi ya kanuni)

  • Wakati mwingine kutumia dawa za kupambana na virusi

Kuzuia ni muhimu kwa watu wote, lakini hasa kwa watoa huduma za afya na wale walio katika hatari kubwa ya kupata maradhi ya mafua.

Je, Ulijua...

  • Watu wote wenye umri wa miezi 6 au zaidi, kwa kufuata baadhi ya kanuni, wanapaswa kupata chanjo kila mwaka.

Chanjo za mafua

Chanjo za kila mwaka ni njia bora za kuepuka kupata mafua.

Ili upate maelezo zaidi kuhusu majadiliano ya chanjo za mafua, angalia Chanjo ya Homa ya Mafua. Chanjo inapangwa kutolewa kwa watu wengi lakini ni muhimu hasa kwa watu walio katika hatari zaidi na wataalamu wa afya.

Chanjo za mafua mara nyingi hukinga dhidi ya aina 3 au 4 tofauti za virusi vya homa ya mafua. Aina za virusi zinazosababisha milipuko ya mafua hubadilika kila mwaka. Kwa hivyo, chanjo tofauti hutengenezwa kila mwaka ili kukabiliana na mabadiliko ya virusi. Wataalamu wanajaribu kutabiri aina ya virusi ambavyo vitashambulia kila mwaka kulingana na aina ya virusi ambavyo vilikuwepo wakati wa msimu wa mafua uliopita na aina inayosababishwa ugonjwa katika sehemu nyingine ulimwenguni. Protini za H na N zinapolingana na aina zile zilizopo kwenye aina ya mafua yanayosababisha mlipuko wa sasa, chanjo itapunguza kiwango cha maambukizi kwa asilimia 70 hadi 90 kwa watu wazima wenye afya.

Kwa watu wazima wengine wanaoishi katika nyumba za utunzaji wa muda mrefu wana uwezekano mdogo sana wa kuzuia mafua, lakini inapunguza uwezekano wa kupata nimonia na kufa. Kwa sababu mfumo wa kingamwili unakuwa dhaifu zaidi kadiri watu wanapozeeka, chanjo ya dozi kubwa ya homa ya mafua imetengenezwa mahususi kwa watu wenye umri wa miaka 65 na zaidi. Chanjo hii yenye dozi kubwa inaweza kusababisha jibu thabiti zaidi la kingamaradhi kwa wazee.

Ingawa chanjo ya homa ya mafua inaweza kutolewa wakati mmoja sawa na chanjo ya COVID-19.

Dawa za kupambana na virusi

Ingawa chanjo ni njia inayopendelewa ya kuzuia maambukizo, dawa kadhaa za kupambana na virusi zinaweza kutumiwa na watu fulani ili kuzuia maambukizo ya virusi vya mafua.

Wakati wa mlipuko wa mafua, dawa za kupambana na virusi hutolewa kwa watu ambao wamepewa chanjo ndani ya kipindi cha wiki 2 zilizopita (kwa sababu huchukua wiki 2 hadi chanjo ianze kufanya kazi). Husitishwa wiki 2 baada ya watu kupewa chanjo. Dawa hizi pia hutolewa kwa watoto walio na matatizo ambayo hufanya chanjo isifae au iwe hatari.