Unene Kupita Kiasi Wakati wa Balehe

NaSarah M. Bagley, MD, MSc, Boston University Chobanian & Avedisian School of Medicine
Imekaguliwa naAlicia R. Pekarsky, MD, State University of New York Upstate Medical University, Upstate Golisano Children's Hospital
Imepitiwa/Imerekebishwa Imebadilishwa Nov 2024
v817892_sw

Unene kupita kiasi ni tatizo sugu, linaloojirudia na gumu lenye sifa za kuwa na uzito wa mwili kupita kiasi.

  • Ingawa vinasaba na baadhi ya matatizo husababisha unene kupita kiasi, unene mwingi wa vijana hutokana na ukosefu wa shughuli za kimwili na kula kalori zaidi kuliko inavyohitajika kwa kiwango cha shughuli.

  • Kielezo cha uzito wa mwili (BMI) kilicho au zaidi ya asilimia 95 kwa umri na jinsia ni kifaa mojawapo kinachotumika kugundua unene uliopitiliza.

  • Kula lishe bora na kuongeza mazoezi husaidia kutibu unene kupita kiasi, na baadhi ya watoto wanaweza kupewa dawa za kupunguza uzito au kufanyiwa upasuaji wa kupunguza uzito.

Unene kupita kiasi umekuwa wa kawaida zaidi miongoni mwa vijana, na takribani kijana 1 kati ya 5 nchini Marekani ana unene kupita kiasi. Ingawa matatizo mengi ya unene kupita kiasi hutokea katika utu uzima, vijana wenye unene kupita kiasi wana uwezekano mkubwa wa kuwa na shinikizo la damu na kisukari aina ya 2. Vijana wengi wenye unene kupita kiasi huwa watu wazima wenye unene kupita kiasi.

Kwa sababu ya unyanyapaa wa jamii dhidi ya unene kupita kiasi, vijana wengi wenye unene kupita kiasi hudhihakiwa au kuonewa, hali inayoweza kuwafanya waendelee kukaa kimya na kutengwa kijamii.

(Tazama pia Utangulizi wa Masuala ya Huduma za Afya kwa Vijana na Unene kupita kiasi kwa watu wazima.)

Sababu za Unene Kupita Kiasi Wakati wa Balehe

Mambo mengi ya kimazingira huchangia unene kupita kiasi kwa vijana. Kwa mfano, vijana wanaweza kuwa wanakula sana vyakula visivyo na virutubisho bora na hawapati wa vyakula vya kutosha vyenye virutubisho, wanaweza kuwa na tatizo la kukosa usingizi, au wanaweza kujenga tabia za kukaa chini kutokana na matumizi ya simu za mkononi kupita kiasi, michezo ya kompyuta na vifaa vingine vya kielektroniki.

Matatizo ya homoni, kama vile tezi isiyofanya kazi vizuri (hypothyroidism) au tezi za adrenali zinazofanya kazi kupita kiasi, zinaweza kusababisha unene kupita kiasi lakini mara chache huwa chanzo chake. Vijana walio na ongezeko la uzito linalosababishwa na tatizo la homoni kwa kawaida huwa na dalili nyingine za tatizo hilo.

Vinasaba huonekana sehemu kubwa, kumaanisha kwamba baadhi ya watu wako katika hatari kubwa ya unene kupita kiasi kuliko wengine, na unene kupita kiasi unaweza kuwa wa kawaida zaidi miongoni mwa wanafamilia moja.

Utambuzi wa Unene wa Kupita Kiasi kwa Balehe

  • Kielelezo cha uzito wa mwili

  • Wakati mwingine hupima matatizo mengine

Kielezo cha uzito wa mwili (BMI) ni moja ya zana zinazotumika kugundua unene kupita kiasi. Vijana ambao BMI yao iko katika 5% ya juu kulingana na umri na jinsia yao wanachukuliwa kuwa na unene uliopitiliza. Kuwa katika 5% ya juu kunamaanisha BMI yao ni kubwa kuliko 95% ya wenzao (kwa au zaidi ya asilimia 95). Hata hivyo, BMI ina mapungufu kwa sababu haizingatii uzito wa misuli, msongamano wa mifupa, muundo wa mwili kwa ujumla, na tofauti za rangi na jinsia.

Kijana yeyote mwenye unene uliopitiliza ambaye ni mfupi na ana shinikizo la damu anaweza kupimwa tatizo la homoni Ugonjwa wa Cushing. Vipimo vingine hufanywa ikiwa madaktari wanatilia shaka kwamba kijana ana tatizo jingine au tatizo jingine limegunduliwa, kama vile kisukari, shinikizo la damu, viwango vya juu vya mafuta katika damu na matatizo ya afya ya akili.

Matibabu ya Unene Kupita Kiasi Wakati wa Balehe

  • Tabia za kula na kufanya mazoezi yanayofaa

  • Kwa vijana wa miaka 12 na zaidi wenye BMI katika au zaidi ya asilimia 95, dawa za kupunguza uzito

  • Kwa vijana wenye umri wa miaka 13 na zaidi walio na BMI kwa kiasi kikubwa zaidi ya asilimia 95, tathmini ya upasuaji wa kupunguza uzito

Watoto na vijana wote wenye unene kupita kiasi hupewa mikakati thabiti ya kuwasaidia kukuza tabia za kula na kufanya mazoezi yenye afya na kufanya mabadiliko katika tabia zao za kiafya.

Kupunguza ulaji wa kalori na kuchoma kalori ni njia mbili za kufikia malengo haya.

Ulaji wa kalori hupunguzwa kwa

  • Kuanzisha lishe bora ya vyakula vya kawaida

  • Kufanya mabadiliko ya kudumu katika tabia za kula

Kuchoma kalori huongezeka kwa

  • Kuongeza shughuli za kimwili

Vijana wenye umri wa miaka 12 na zaidi walio na unene kupita kiasi (BMI ikiwa au zaidi ya asilimia 95 kwa umri na jinsia) wanaweza kutolewa dawa za kupunguza uzito.

Vijana wenye umri wa miaka 13 na zaidi walio na unene kupita kiasi (BMI iliyo juu zaidi ya asilimia 95 kwa umri na jinsia) wanaweza kupelekwa kwa daktari bingwa wa upasuaji ambaye ni mtaalamu katika eneo hili kwa ajili ya tathmini kamili ya upasuaji wa kupunguza uzito (upasuaji wa bariatric).

Ushauri nasaha ili kuwasaidia vijana kukabiliana na matatizo ya kijamii unaweza kuwa msaada.