Ubotuli wa Watoto Wachanga

NaLarry M. Bush, MD, FACP, Charles E. Schmidt College of Medicine, Florida Atlantic University;
Maria T. Vazquez-Pertejo, MD, FACP, Wellington Regional Medical Center
Imekaguliwa naBrenda L. Tesini, MD, University of Rochester School of Medicine and Dentistry
Imepitiwa/Imerekebishwa Jun 2023 | Imebadilishwa Apr 2025
v39247275_sw

Ubotuli wa watoto wachanga ni maambukizi yanayoweza kutishia maisha na husababisha udhaifu wa misuli. Hukua kwa watoto wachanga wanaokula chakula chenye viiniyoga vya bakteria wa Clostridium botulinum.

(Angalia pia Muhtasari wa Maambukizi ya Clostridia na Ubotuli wa watu wazima.)

Clostridium botulinum hazihitaji oksijeni ili kuishi. Yaani, hivyo ni anaerobi.

Bakteria wa clostridia huzalisha viiniyoga. Viiniyga huwa katika hali isiyo hai (bwete) ya bakteria. Vijibofu huwezesha bakteria kuishi wakati hali ya mazingira ni ngumu. Hali zinapokuwa nzuri, viiniyoga hukua na kuwa bakteria. Viiniyoga vya clostridia hukua zinapokuwa na unyevu na virutubisho na oksijeni inapokosekana, hali ambayo ipo kwenye utumbo. Hivyo, watoto wachanga wakila chakula chenye viiniyoga vya clostridia, viiniyoga hivyo hukua na kuwa bakteria ndani ya utumbo na kuanza kuzalisha sumu.

Ubotuli wa watoto wachanga hutokea mara nyingi zaidi kwa watoto walio chini ya miezi 6, na unaweza kutokea hadi takriban umri wa miezi 12. Kwa watoto wenye umri wa miezi 12 na zaidi na kwa watu wazima, aina hii ya ubotuli ambayo sumu huzalishwa kutokana na viiniyoga kwenye utumbo huitwa ubotuli wa smu ya utumbo kwa watu wazima.

Chanzo cha viiniyoga katika visa vingi vya ubotuli wa watoto wachanga kwa kawaida hakijulikani, lakini baadhi ya visa vimehusishwa na kumeza asali, ambayo inaweza kuwa na viiniyoga. Hivyo, madaktari wanapendekeza kwamba watoto walio chini ya miezi 12 hawapaswi kulishwa asali.

Je, Ulijua...

  • Watoto walio chini ya miezi 12 hawapaswi kulishwa asali kwa sababu inaweza kuwa na viiniyoga vya bakteria wa Clostridium botulinum.

Dalili za Ubotuli wa Watoto Wachanga

Kuvibiwa ni dalili ya kwanza kwa watoto wengi wachanga wenye ubotuli wa watoto wachanga. Kisha misuli hudhoofika, kuanzia kwenye uso na kichwa na hatimaye kufikia mikono, miguu, na misuli inayohusika na kupumua. Kope huinama, kulia huhisi dhaifu, na utoaji wa mate unaweza kuongezeka. Watoto wachanga hawawezi kunyonya vizuri, na uso wao hupoteza ishara zake.

Matatizo huanzia uchovu na kula polepole hadi kupoteza kiasi kikubwa cha misuli na kuwa na ugumu wa kupumua. Watoto wachanga wanapopoteza mkazo wa misuli, wanaweza kuhisi kama wamechoka sana (udhaifu wa misuli ya mtoto).

Utambuzi wa Ubotuli wa Watoto Wachanga

  • Vipimo vya kinyesi

Madaktari hushuku ubotuli wa watoto wachanga kulingana na dalili.

Kugundua bakteria au sumu katika sampuli ya kinyesi cha mtoto huthibitisha utambuzi wa ubotuli wa watoto wachanga.

Matibabu ya Ubotuli wa Watoto Wachanga

  • Globulini ya kinga dhidi ya ubotuli

Matibabu huanza mara tu ubotuli wa watoto wachanga unaposhukiwa, bila kusubiri matokeo ya vipimo.

Watoto wachanga hulazwa hospitalini, na madaktari huchukua hatua za kuwatuliza (kuzuia hali yao isizidi kuwa mbaya), kama vile kutumia mashine ya kupumulia kusaidia kupumua.

Ubotuli wa watoto wachanga hutibiwa kwa kutumia globulini ya kinga dhidi ya ugonjwa wa ubotuli, ambayo hutolewa taratibu kupitia mshipa wa damu. Globulini hii ya kinga hupatikana kutoka kwa wachangiaji wa binadamu wenye viwango vya juu vya kingamwili dhidi ya sumu ya ubotuli. (Kingamwili ni protini zinazozalishwa na mfumo wa kinga ili kusaidia kulinda mwili dhidi ya kishambuzi fulani, kama vile sumu ya ubotuli.)

Viuavijasumu havisaidii kwa sababu tatizo kuu ni sumu ambayo tayari imeshazalishwa na bakteria.

Taarifa Zaidi

Nyenzo zifuatazo za lugha ya Kiingereza zinaweza kuwa muhimu. Tafadhali kumbuka kuwa Mwongozo hauwajibiki kwa maudhui ya nyenzo hizi.

  1. Mpango wa Matibabu na Kinga ya Ubotuli wa Watoto Wachanga: Tovuti au piga simu 510-231-7600: Hutoa taarifa kuhusu matibabu, kinga, na makundi ya usaidizi