Homa ya ini sugu ni nini?
Homa ya ini sugu ni uvimbe (kuvimba) wa ini ambao unadumu kwa miezi 6 au zaidi. Homa ya ini sugu kwa kawaida inatokana na homa kali ya ini lakini huenda usijue ulipata homa ya ini kali.
Kwa kawaida, homa ya ini sugu inasababishwa na virusi vya homa ya ini B au C au dawa fulani
Watu wengi hawaoneshi dalili lakini baadhi ya watu wanaweza kujihisi kuumwa kidogo, kuchoka au hawahisi njaa
Wakati mwingine, homa ya ini sugu inaweza kusababisha matatizo kali baada ya muda, kama vile sirosisi , ambayo husababisha makovu na kuharibika kwa ini, wakati mwingine kusababisha kufeli kwa ini
Homa ya ini sugu inaweza kudumu kwa miaka kadhaa
Madaktari wakati mwingine hutibu homa ya ini sugu kwa dawa
Je, nini kinasababisha homa ya ini sugu?
Homa ya ini sugu kwa kawaida inasababishwa na maoja wapo kati ya virusi vya homa ya ini, hasa homa ya ini B na C.
Homa ya ini sugu inaweza pia kusababishwa na:
Aina fulani za dawa, hasa ikiwa utazitumia kwa muda mrefu
Magonjwa fulani, kama vile ugonjwa wa ini unaohusiana na pombe, ugonjwa wa ini lenye mafuta, na mengine
Mmenyuko wa mfumo wa kingamwili kwenda kinyume na mwili (wakati mfumo wa kingamwili hushambulia ini kimakosa)
Madaktari hawajui hasi kile kinachosababisha homa ya ini sugu kwa baadhi ya watu.
Je, dalili za homa ya ini sugu ni zipi?
Karibu watu 2 kati ya 3 wenye homa ya ini sugu wanakuwa nayo taratibu na wanakuwa hawaonyeshi dalili hadi wanapokuwa na sirosisi (ini kuwa na makovu).
Unaweza kuwa na dalili kama vile:
Kujisikia kuumwa kidogo, na kutokuhisi njaa sana
Wakati mwingine, homa na maumivu kiasi kwenye eneo la juu la tumbo lako
Uvimbe kutokana na majimaji kujitengeneza kwenye eneo la tumbo lako (ugonjwa wa tumbo kujaa maji)
Mishipa misogo ya damu kama buibui kwenye ngozi yako (angioma ya buibui)
Viganja vyekundu
Kutofikiria vyema
Kutokwa damu kwa urahisi
Mwasho
Kinyesi chenye rangi angavu, kinachokaa grisi, kinachonukia vibaya
Dalili za mfumo wa kingamwili kwenda kinyume na mwili kama vile maumivu ya viungo na kwa wanawake kukosa hedhi
Ikiwa una homa ya ini B sugu au homa ya ini C pamoja na sirosisi, unaweza kuwa na saratani ya ini.
Madaktari wanawezaje kujua kuwa nina homa ya ini sugu?
Madaktari watafanya:
Fanya vipimo vya damu
Watachukua sampuli ndogo ya ini lako ili kuichunguza kwenye hadubini (uondoaji wa kipande cha tishu kwa uchunguzi)
Je, madaktari hutibu vipi homa ya ini sugu?
Daktari wako atatibu homa ya ini sugu kwa njia tofauti kulingana na kisababishi:
Ikiwa dawa fulani ndiyo chanzo, daktari wako atakuambia uache kutumia dawa hiyo.
Ikiwa homa ya ini B, C au E ndiyo kisababishaji, daktari wako kwa kawaida atakupatia dawa ili kutibu virusi
Ikiwa unapata athari ya mfumo wa kingamwili kwenda kinyume na mwili, daktari wako atakupa kotikosteroidi kupunguza mwako kwenye ini
Ikiwa ini limeshindwa kufanya kazi, huenda ukahitaji kuwekewa ini jingine
Madaktari pia watatibu matatizo yoyote ambayo yamesababishwa na homa ya ini sugu.