Ugonjwa wa kutungiwa na mtu mwingine ni kughushi au kutoa dalili za ugonjwa wa kimwili au kisaikolojia kwa mtu mwingine. Kwa kawaida hufanywa na walezi (kawaida wazazi) kwa mtu wanayemlea.
(Tazama pia Muhtasari wa Wasiwasi wa Mwili na Matatizo Yanayohusiana.)
Ugonjwa huu ulikuwa ukiitwa ugonjwa wa kutunga kwa uwakala au ugonjwa wa Munchausen kwa uwakala.
Ugonjwa wa kutungiwa na mtu mwingine ni sawa na ugonjwa kujitungia binafsi, isipokuwa kwamba watu (kawaida walezi, kwa kawaida mzazi) kwa makusudi hudanganya au kutoa dalili za kimwili au kisaikolojia kwa mtu wanayemlea (kawaida mtoto ambaye hawezi kupinga uwongo wa mlezi au kusema jinsi mlezi alivyosababisha jeraha).
Mlezi hudanganya historia—kwa mfano, kwa kusema kwamba watoto wamekuwa wakipata homa au kutapika nyumbani wakati kiuhalisia walikuwa wazima. Baadhi ya walezi wanaweza hata kumdhuru mtoto kwa dawa au dawa haramu au viambato vingine au kuongeza uchafu wa damu au bakteria kwenye sampuli za mkojo ili kuigiza ugonjwa. Mlezi hutafuta huduma ya matibabu kwa ajili ya mtoto na anaonekana kuwa na wasiwasi mkubwa na mwenye kumlinda. Mtoto kwa kawaida huwa na historia ya kulazwa hospitalini mara kwa mara, kwa kawaida kwa dalili mbalimbali zisizo bayana, lakini hakuna utambuzi thabiti uliofanywa. Watoto kama hao wanaweza kuwa wagonjwa sana na wakati mwingine kufa kwa sababu ya majaribio ya mlezi kuigiza ugonjwa.
Kama ilivyo kwa ugonjwa wa kujitungia binafsi, mlezi kwa kawaida hana sababu dhahiri za nje kwa tabia hiyo. Kwa mfano, mlezi si kwamba najaribu kuficha dalili za unyanyasaji wa watoto.