Kyclosporiasisi ni maambukizi ya utumbo mdogo yanayosababishwa na kimelea kinachoitwa Cyclospora cayetanensis. Dalili kuu ni kuhara kwa maji na mikakamao ya tumbo na kichefuchefu.
Watu wanaweza kuambukizwa na Cyclospora kwa kutumia vyakula au maji yaliyoingizwa kutoka nje ya nchi iliyo na vimelea hivyo.
Dalili za kyclosporiasis zinaweza kuwa mbaya sana kwa watu wenye mfumo wa kingamwili dhaifu, kama vile watu wenye virusi vya UKIMWI (VVU).
Dalili hutofautiana lakini ni pamoja na kuhara maji mengi, mikakamao ya tumbo, homa, na kupunguza uzito.
Madaktari wanatambua maambukizi kwa kubainisha Kyclospora kwenye sampuli ya kinyesi.
Trimethoprim/sulfamethoxazole (TMP/SMX) inatumika kutibu kyclosporiasis.
(Angalia pia Muhtasari wa Maambukizi ya Vimelea.)
Kyclosporiasis inapatikana sana kwenya mazingira ya joto ambapo hali ya usafi ni duni. Wakazi na wasafiri kwenye maeneo yenye maambukizi wapo hatarini.
Kyclosporiasis inazidi kurekodiwa nchini Marekani, Kanada na Ulaya. Nchini Marekani, mlipuko kwa kawaida unatokea wakati wa kiangazi na unahusishwa na kutumia vyakula vibichi kama vile, raspberi, blackberi, stroberi, bluberi, basil, cilantro, snow peas, snap peas, mboga za majani zilizoandaliwa, na mbogamboga zingine.
Cyclospora oocysts are not sporulated (ie, infective) when passed in stool. Thus, direct fecal-oral transmission does not occur.
1. Unsporulated oocysts are excreted from the infected host in stool.
2–3. The oocysts sporulate in the environment after 1 to 2 weeks at temperatures between 22 to 32° C.
4. The sporulated oocysts contaminate food or water. The mechanism for contamination has not been established.
5. The sporulated oocysts are ingested in contaminated food or water.
6. The oocysts excyst in the gastrointestinal tract, releasing the sporozoites, which invade the epithelial cells of the small intestine.
7. Inside the cells, they multiply asexually and develop sexually to mature into oocysts, which are shed in stool.
Image from the Centers for Disease Control and Prevention, Global Health, Division of Parasitic Diseases and Malaria.
Dalili za Kyclosporiasisi
Dalili ya kwanza ya kyclosporiasisi ni kuhara kwa ghafula kusiko na damu, kwa majimaji na kichefuchefu. Dalili nyingine hujumuisha homa, mikazo ya tumbo, kutapika, uchovu na kupungua uzani. Dalili kwa watu wenye mfumo wa kingamwili wa kawaida hudumu kuanzia siku chache hadi mwezi mzima au zaidi. Zinaweza kutokea tena.
Kwa watu wenye mfumo wa kingamwili uliodhoofika, ikiwa ni pamoja na watu wenye VVU yenye hatua ya mwisho, kyclosporiasis inaweza kusababisha kuharisha ambako kunaweza kudumu kwa muda mrefu.
Utambuzi wa Sistoisosporiasisi
Vipimo vya kinyesi
Ili kutambua ugonjwa wa kyclosporiasisi, sampuli ya kinyesi inachunguzwa kwa hadubini ili kuona mayai ya Cyclospora. Mbinu maalum zinaweza kutumika kuongeza nafasi za kutambua mayai. Mbinu za molekyula zinapatikana baadhi ya maabara za rejea ili kubainisha DNA ya kimelea.
Pale ambapo uchunguzi wa kinyesi hauonyeshi sababu ya kuhara kusikokoma, madaktari wanaweza kutumia neli jongevu ya kutazamia (endoscope) kuchunguza sehemu ya juu ya njia ya mmeng'enyo wa chakula na kuchukua sampuli ya tishu (kipande cha tishu) ili kuchunuwa kwa kutumia hadubini na kuchanganua DNA ya kimelea.
Matibabu ya Sistoisosporiasisi
Trimethoprim/sulfamethoxazole (TMP/SMX)
Vinginevyo, ciprofloxacin
Watu wengi wenye afya wanapona bila matibabu. Isipotibiwa, ugonjwa unaweza kudumu kwa siku kadhaa hadi mwezi mmoja au zaidi na unaweza kutokea tena.
Uchaguzi wa matibabu ya kyclosporiasis ni nguvu mara mbili TMP/SMX ikimezwa kwa mdumu siku 7 hadi 10.
Watu wenye VVU, ni muhimu sana kutibu maambukizi ya VVU kwa ufanisi kadiri iwezekanavyo kwa dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI. Matibabu kama hayo yanaweza kuimarisha mfumo dhaifu wa kingamwili, ambao kwa kawaida husaidia kudhibiti kuhara na dalili nyingine. Watu wenye VVU ya hatua ya mwisho wanaweza kunufaika na dozi ya juu ya TMP/SMX na matibabu ya muda mrefu.
Ciprofloxacin na wakati mwingine nitazoxanide ni mbadala wa TMP/SMX kutibu kyclosporiasis.
Uzuiaji wa Sistoisosporiasisi
Kuepuka chakula au maji ambayo yana vimelea ni njia bora ya kuzuia kyclosporiasisi.
Wasafiri kwenda kwenye maeneo yenye kyclosporiasis (kama vile maeneo ya joto au nusujoto) wanapaswa kuwa na tahadhari kwamba kutibu maji au chakula kwa kemikali ya kuua vijidudu au mbinu za utakasaji hakuwezi kuua Cyclospora. (Angalia Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa [CDC]: Vimelea - Cyclosporiasis: Kuzuia na kudhibiti). Mapendekezo ya kina kwa wasafiri wa kimataifa yanapatikana kwenye Kitabu cha Njano cha CDC: Tahadhari za Chakula na Maji.
Katika maeneo yenye maambukizi, maji ya kuywa yanapaswa kuchemshwa, matunda yasiyomenywa yanapaswa kuepukwa na mboga za majani zipikwe sana.
Taarifa Zaidi
Nyenzo zifuatazo za lugha ya Kiingereza zinaweza kuwa muhimu. Tafadhali kumbuka kuwa MWONGOZO hauwajibiki kwa maudhui ya nyenzo hizi.