Sporotrichosis ni maambukizi yanayosababishwa na kuvu Sporothriksi.
Maambukizi haya hutokea wakati kuvu imeingia mwilini kupitia michubuko na mikwaruzo midogo kwenye ngozi au kupitia kuumwa au mikwaruzo kutoka kwa paka walioambukizwa.
Kwa kawaida, ngozi na nodi za limfu zilizo karibu huambukizwa, na kusababisha matuta na vidonda wazi kwenye ngozi na nodi za limfu ambazo zimevimba.
Ni nadra kwa mapafu, viungo au sehemu zingine za mwili kuambukizwa.
Utambuzi huhitaji ukuzaji na utambuzi wa kuvu katika sampuli ya tishu iliyoambukizwa.
Itraconazole hutumika kutibu maambukizi mengi, lakini amphotericin B huhitajika kwa maambukizi makali na yaliyoenea.
(Angalia pia Muhtasari wa Maambukizi ya Kuvu.)
Kuvu ya Sporothriksi kwa kawaida hukua kwenye vichaka vya waridi au barberry, kwenye kuvumwani ya sphagnum (sphagnum moss), kwenye nyasi kavu, na kwenye matandazo mengine. Tofauti na maambukizi mengine mengi ya kuvu, kuvu ya Sporothrix kwa kawaida hawavutwi puani bali huingia mwilini kupitia michubuko na mikwaruzo midogo kwenye ngozi. Mara nyingi, maambukizi hutokea kwa wakulima, wanaotunza bustani, na wafanyakazi wa mbao.
Wakati mwingine watu huambukizwa na paka, hasa watu wa Amerika Kusini. Paka walioambukizwa Sporothrix wanaweza kueneza kuvu kwa watu wanapowauma au kuwakwaruza. Watu wanaweza pia kuambukizwa ikiwa watagusana na vidonda vya ngozi vya paka ambao wameambukizwa. (Tazama pia Maambukizi ya Fangasi kwa Paka.)
Sporotrichosis huathiri zaidi ngozi na mishipa ya limfu iliyo karibu. Mara chache sana, maambukizi ya mapafu nimonia hutokea baada ya watu kuvuta vijimbegu vinavyozalishwa na kuvu.
Pia kwa nadra mifupa, viungo, sehemu za siri, ini, figo, wengu au ubongo huambukizwa, kwa kawaida kwa watu wenye mfumo dhaifu wa kinga, kama vile wale walio na maambukizi ya VVU yaliyoendelea (pia huitwa UKIMWI).
Dalili za Sporotrichosis
Katika sporotrichosis, maambukizi ya ngozi kwa kawaida huanza kwenye mkono lakini yanaweza kutokea popote mwilini. Kidonda kidogo kinaweza kuonekana kwenye ngozi, au kidonda kikubwa kinaweza kuonekana chini ya ngozi (kinundu). Kinundu chochote kinaweza kupanuka polepole na kusababaisha kidonda wazi (kidonda).
Sporotrichosis starts as a small bump that slowly enlarges and may form an open sore.
Katika siku au wiki kadhaa zinazofuata, maambukizi huenea kupitia mishipa ya limfu ya eneo ambalo limeambukizwa hadi kwenye nodi za limfu, na kuunda vinundu zaidi njiani. Bila matibabu, ngozi iliyo juu huwa nyekundu na inaweza kufa baadaye, wakati mwingine ikisababisha mifuko ya usaha (majipu) na vidonda vilivyo wazi kutokea. Usaha kutoka kwa nodi za limfu, mishipa ya limfu iliyovimba, au vyote viwili vinaweza kupasuka ndani ya ngozi, na kusababisha uwazi ambao nyenzo iliyoambukizwa hutoka. Sporotrichosis inaweza kuwa mbaya zaidi ikiwa watu watapatwa na maambukizi mengine yanayosababishwa na bakteria. Hata katika hatua hii, watu huwa na maumivu kidogo au kutokuwa nayo kabisa na kwa kawaida, huwa hawapati dalili zingine.
Sporotrichosis ni ugonjwa unaoua tu kwa watu ambao wanapata maambukizi ya bakteria yanayosababisha maambukizi makubwa katika damu (sepsisi).
If untreated, sporotrichosis may spread along the lymphatic vessels of a finger, hand, and arm, causing open sores on the skin along the way. In this photo, open sores have been infected by other bacteria, causing more widespread infection of the skin.
Mara chache, sporotrichosis haiambukizi ngozi au nodi za limfu bali huenea mwilini kote na kuambukiza viungo na wakati mwingine mifupa, sehemu za siri, ini, figo, wengu, au ubongo. Maambukizi ya viungo husababisha uvimbe na kufanya mwendo usababishe maumivu. Maambukizi kama hayo yanaweza kusababisha kifo na ni ya kawaida miongoni mwa watu walio na mfumo dhaifu wa kinga. Nimonia pia ni nadra. Watu huenda wakawa na maumivu kidogo ya kifua na kikohozi. Nimonia mara nyingi hutokea kwa watu walio na ugonjwa mwingine wa mapafu, kama vile emphysema.
Utambuzi wa Sporotrichosis
Uoteshaji wa sampuli za tishu zilizoambukizwa
Kipimo cha mmenyuko wa mnyororo wa polima (PCR)
Vinundu na vidonda vinavyoonekana vinaweza kumfanya daktari ashuku kuwepo kwa sporotrichosis, hasa kwa watu ambao huenda wameathiriwa na kuvu (kwa mfano, watunza bustani, watunza mandhari, na watunza misitu).
Utambuzi unathibitishwa kwa kukuza (kuotesha) na kutambua Sporothriksi katika sampuli za tishu zilizoambukizwa.
Kipimo cha kugundua nyenzo za kijenetiki katika kuvu (DNA yake), kama vile kipimo cha PCR, kinaweza kufanywa kwenye sampuli za tishu iliyoambikizwa. Kipimo cha PCR hutumika kutoa nakala nyingi za jeni kutoka kwenye kuvu, hivyo kufanya kuvu liwe rahisi zaidi kutambuliwa.
Matibabu ya Sporotrichosis
Dawa za kuua kuvu
Watu walio na maambukizi ya ngozi na nodi za limfu hutibiwa kwa itraconazole inayotolewa kwa njia ya mdomo.
Ikiwa maambukizi ni makubwa na yameenea, amphotericin B hutolewa kwa njia ya mishipa hadi dalili zianze kutoweka na kisha hubadilishwa kuwa itraconazole. Kwa ujumla, matibabu huchukua mwaka mmoja.
Baada ya maambukizi kudhibitiwa, watu wenye maambukizi ya VVU yaliyoendelea wanaweza kuhitaji kutumia itraconazole maisha yao yote. Itraconazole husaidia kuzuia sporotrichosis kujirudia wakati mfumo wa kinga ni dhaifu.