Histoplasmosis ni maambukizi yanayosababishwa na kuvu Histoplasma capsulatum. Hutokea hasa kwenye mapafu lakini wakati mwingine yanaweza kuenea mwilini kote.
Kwa kawaida maambukizi husababishwa na kuvuta pumzi ya spore ya kuvu.
Watu wengi hawana dalili, lakini wengine hujihisi wagonjwa na huwa na homa na kikohozi, wakati mwingine pamoja na ugumu wa kupumua.
Wakati mwingine maambukizi huenea, na kusababisha ini, wengu, na tezi za limfu kuwa kubwa na kuharibu viungo vingine.
Utambuzi huo hutegemea ukuzaji vimelea na vipimo vya sampuli za tishu, damu na viowevu na vipimo vya upigaji picha wa mapafu.
Uamuzi wa iwapo matibabu ya dawa za kuzuia fangasi yatahitajika hutegemea ukali wa maambukizi.
(Angalia pia Muhtasari wa Maambukizi ya Kuvu.)
Histoplasmosis kwa kawaida hutokea wakati watu wamevuta vijimbegu vya kuvu. Histoplasma capsulatum hukua vizuri zaidi kwenye udongo na vumbi iliyochafuliwa na kinyesi cha ndege au popo. Wakulima wanaofuga kuku, wafanyakazi wa mjengo, wanaopenda kuingia kwenye mapango (watu wanaopenda kuchunguza mapango) na wengine ambao wanafanya kazi kwa kutumia udongo wana uwezekano mkuu wa kuvuta vijimbegu vinavyotokana na kuvu. Hatari ya maambukizi ni kubwa zaidi wakati shughuli zinazalisha vijimbegu vinavyopeperushwa hewani (kwa mfano, kuondoa miti au jengo katika maeneo ya ujenzi kwenye maeneo ambayo ndege au popo huishi) au wakati wa kuchunguza mapango.
Histoplasmosis hupatikana sana katika mashariki na magharibi mwa Marekani, hasa kando ya mabonde ya Mto Ohio na Mississippi. Huenda ikatokea katika majimbo ya kusini na kusini-mashariki. Histoplasmosis pia hutokea katika sehemu za Amerika ya Kati na Kusini, Afrika, Asia, na Australia. Milipuko inayohusiana na mapango ya popo imetokea duniani kote, ikiwa ni pamoja na Amerika Kusini, Afrika na sehemu za Asia, na nchini Marekani imeripotiwa huko Florida, Texas, na Puerto Rico.
Histoplasmosis kwa kawaida huathiri mapafu. Maambukizi kwa kawaida hubaki kwenye mapafu, lakini yanaweza kuenea hadi sehemu nyingine za mwili. Ugonjwa mkali unaweza kutokea wakati idadi kubwa ya vijimbegu imevutwa.
Watu fulani huwa katika hatari kubwa ya kupata maambukizi makali ya histoplasmosis. Maambukizi makali yanayotokea hasa kwa watu wenye mfumo dhaifu wa kinga mwilini huitwa maambukizi nyemelezi. Histoplasmosis inayoenea kwenye sehemu nyingine za mwili ni maambukizi nyemelezi kwa watu wanaoishi na maambukizi ya VVU yaliyoendelea (pia huitwa UKIMWI).
Viashiria vingine vya hatari kwa maambukizi makali ya histoplasmosis ni pamoja na yafuatayo:
Kuathiriwa sana na vijimbegu kwa muda mrefu
Umri wa miaka 55 au zaidi
Umri wa mwaka 1 au mdogo
Matumizi ya dawa zinazokandamiza mfumo wa kinga, kama steroidi (pia wakati mwingine huitwa glucocorticoids or corticosteroids) au vizuizi vya visababishi vya tumor necrosis (zinazotumiwa kutibu baridi yabisi (rheumatic arthritis) na magonjwa yanayohusiana)
Miundo ya Histoplasmosis
Kuna aina tatu kuu za histoplasmosis:
Histoplasmosis kali ya mapafu: Aina hii ndiyo aina ya awali ya maambukizi. Hutokea kwenye mapafu na kwa kawaida hubaki hapo.
Histoplasmosis iliyosambazwa inayoendelea: Ikiwa mfumo wa kinga umedhoofika au haujakomaa, huenda maambukizi yakaenea (kusambaa) kutoka kwenye mapafu kupitia damu hadi sehemu zingine za mwili, kama vile ubongo, uti wa mgongo, ini, wengu, tezi za limfu, tezi za adrenali, mfumo wa usagaji chakula, au uboho. Aina hii ni nadra kutokea kwa watu wazima wenye afya njema. Kwa kawaida hutokea kwa watoto wachanga au wadogo sana wenye utapiamlo au kwa watu wenye mfumo dhaifu wa kinga, kama vile wale walio na maambukizi ya VVU, waliopandikizwa viungo, au wanaotumia dawa zinazokandamiza mfumo wa kinga, ikiwa ni pamoja na steroidi.
Histoplasmosis sugu ya vijishimo Katika aina hii, nafasi moja au zaidi (vijishimo) hutokea polepole kwenye mapafu kwa wiki kadhaa. Maambukizi haya kwa kawaida hayaenei kutoka kwenye mapafu hadi kwenye sehemu zingine za mwili.
Dalili za Histoplasmosis
Watu wengi walioambukizwa Histoplasma hawapati dalili zozote au hupata dalili ndogo sana, hasa watu wenye mfumo wenye afya wa kinga mwilini.
Dalili zinapojitokeza, hutofautiana kulingana na aina ya histoplasmosis.
Histoplasmosis ya mapafu kali
Dalili kwa kawaida huonekana siku 3 hadi 17 baada ya watu kuvuta vijimbegu. Watu wanaweza kujihisi wagonjwa, kuwa na homa na kikohozi, na kuhisi kama kwamba wana mafua. Dalili kwa kawaida hupotea bila matibabu ndani ya wiki 2 na ni nadra kudumu kwa zaidi ya wiki 6.
Watu wanaovuta vijimbegu vingi huenda wakapata nimonia. Wanaweza kuishiwa sana na pumzi na kuwa wagonjwa kwa miezi kadhaa.
Histoplasmosis kali ya mapafu ni nadra sana lakini inaweza kuwa kali kwa watu walio na mfumo dhaifu wa kinga (kama vile wale walio na maambukizi ya VVU yaliyoendelea).
Histoplasmosis iliyosambazwa inayoendelea
Dalili huwa si wazi mwanzoni. Watu wanaweza kupunguza uzito na kuhisi uchovu, udhaifu na kwa ujumla wawe wagonjwa. Dalili zinaweza kuzidi polepole sana au haraka sana.
Nimonia inaweza kutokea lakini ni nadra kuwa kali, isipokuwa kwa watu walio na maambukizi ya VVU yaliyoendelea. Mara chache, homa ya uti wa mgongo (kuvimba kwa tishu zinazofunika ubongo na uti wa mgongo) inaweza kutokea, na kusababisha maumivu ya kichwa na shingo iliyokakamaa. Wakati mwingine ini, wengu, na tezi za limfu zinaweza kuwa kubwa. Mara chache sana, maambukizi husababisha majeraha (vidonda) kinywani na kwenye matumbo. Mara chache sana, tezi za adrenali huharibika, na kusababisha Ugonjwa wa Addison.
Hata kwa matibabu, histoplasmosis inaweza kusababisha kifo haraka kwa watu walio na maambukizi ya VVU yaliyoendelea.
In people with a weakened immune system, histoplasmosis can cause sores (ulcers) to form in the mouth.
Chronic cavitary histoplasmosis
Aina hii hukua polepole kwa wiki kadhaa, na kusababisha kikohozi na ugumu wa kupumua ambao huzidi kuwa mbaya. Dalili ni pamoja na kupunguza uzito, kutokwa na jasho usiku, homa kidogo na hisia ya jumla ya ugonjwa (malaise).
Watu wengi hupona bila matibabu. Hata hivyo, matatizo ya kupumua huenda yakaendelea kuwa mabaya zaidi na baadhi ya watu hukohoa damu, wakati mwingine kwa kiasi kikubwa.
Aina zingine za histoplasmosis
Katika baadhi ya visa sugu, tishu za mapafu huharibiwa na tishu za kovu huundwa. Uharibifu wa mapafu au uvamizi wa bakteria kwenye mapafu hatimaye unaweza kusababisha kifo.
Aina zingine za histoplasmosis zinaweza kuathiri macho na ngozi. Histoplasmosis ya macho ni maambukizi ya macho yasababishwayo na maambukizi ya awali ya Histoplasma. Inaweza kusababisha madoa yasiyoonekana na kuona kusio kwa kawaida kutokana na makovu na kuvuja kwa mishipa ya damu kwenye sehemu ya nyuma ya jicho. Kwa watu walio na mfumo dhaifu wa kinga, histoplasmosis inaweza pia kusababisha aina mbalimbali za uvimbe wa ngozi (ikiwa ni pamoja na vinundu), mabaka, au vidonda, ambavyo vyote vinaweza kutofautiana katika mwonekano wake kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine. Wakati mwingine maambukizi yanaweza pia kuharibu tishu laini zilizo chini ya ngozi.
Utambuzi wa Histoplasmosis
Ukuzaji na uchunguzi wa sampuli za tishu au majimaji
Wakati mwingine vipimo vya damu na mkojo
Eksirei au uchunguzi wa kifua kwa kutumia tomografia iliyokadiriwa (CT)
Upimaji mwingine
Ili kugundua histoplasmosis, madaktari huchukua sampuli za makohozi, mkojo, na damu. Madaktari wanaweza kutumia bomba la kutazama (bronkoskopu) kuchukua sampuli kutoka kwenye mapafu. Au wanaweza kufanya biopsi ili kuchukua sampuli kutoka kwa ini, uboho, au nodi za limfu. Sampuli hizi hutumwa kwenye maabara kwa ajili ya ukuzaji na kuchunguzwa.
Madaktari huenda pia wakafanya kipimo cha mkojo na damu ili kutafuta protini (antijeni) zinazotolewa na kuvu. Kipimo cha kugundua nyenzo za kijenetiki katika kuvu (DNA yake) huenda kikafanyika.
Madaktari pia hufanya eksirei au kufanya uchanganuzi wa CT ya kifua ili kutafuta ushahidi wa maambukizi ya mapafu.
Matibabu ya Histoplasmosis
Dawa za kuua kuvu
Histoplasmosis kali ya mapafu au watu wenye afya njema (yaani, watu wasio na dalili) ni nadra kuhitaji dawa. Hata hivyo, ikiwa watu hawatapata nafuu baada ya mwezi 1 au ikiwa wana mfumo dhaifu wa kinga, itraconazole, inayotolewa kwa mdomo, mara nyingi huagizwa. Madaktari huenda pia wakaagiza posaconazole au isavuconazonium.
Ikiwa nimonia kali itatokea, watu hupewa amphotericin B kwa njia ya mishipa.
Maambukizi makali ya mapafu yaliyoenea hutibiwa kwa amphotericin B, ikitolewa kwa njia ya mishipa, ikifuatwa na itraconazole, inayotolewa kwa njia ya mdomo.
Watu walio na maambukizi ya VVU yaliyoendelea hupewa itraconazole hadiIdadi yao ya CD4 (idadi ya aina moja ya seli nyeupe za damu inayopungua wakati maambukizi ya VVU yameendelea bila kudhibitiwa) iongezeke hadi seli 150 au zaidi kwa kila mikrolita ya damu na pia wawe wanapokea tiba ya kupunguza makali ya virusi vya ukimwi (ART).
Katika histoplasmosis sugu ya vijishimo, itraconazole au, kwa maambukizi makubwa zaidi, amphotericin B inaweza kuondoa kuvu. Hata hivyo, matibabu hayawezi kupindua uharibifu katika mapafu uliosababishwa na maambukizi. Hivyo, watu wengi huendelea kuwa na matatizo ya kupumua, sawa na yale ambayo husababishwa na ugonjwa sugu unaoziba mapafu. Kwa hivyo, matibabu yanapaswa kuanza haraka iwezekanavyo ili kupunguza uharibifu wa mapafu.
Ubashiri wa Histoplasmosis
Histoplasmosis kali ya msingi karibu kila mara huisha bila matibabu. Hata hivyo, mara chache sana, aina hii inaweza kusababisha kifo kwa watu walio na maambukizi makali na yaliyoenea.
Histoplasmosis sugu ya vijishimo inaweza kusababisha kifo kwa watu ambao wana ugumu wa kupumua unaozidi kuwa mbaya.
Histoplasmosis iliyosambazwa inayoendelea ambayo haijatibiwa inaweza kusababisha kifo kiwa watu wengi.