Matumbwitumbwi

(Epidemic Parotitis)

NaBrenda L. Tesini, MD, University of Rochester School of Medicine and Dentistry
Imekaguliwa naBrenda L. Tesini, MD, University of Rochester School of Medicine and Dentistry
Imepitiwa/Imerekebishwa Jun 2023 | Imebadilishwa Nov 2025
v819146_sw

Matumbwitumbwi ni maambukizi ya virusi yanayoambukiza yanayosababisha uvimbe wenye uchungu kwenye tezi za mate. Maambukizi hayo pia yanaweza kuathiri korodani, ubongo, na kongosho, hasa kwa vijana na watu wazima.

  • Matumbwitumbwi husababishwa na virusi.

  • Dalili ni pamoja na baridi, maumivu ya kichwa, hamu duni ya kula, homa, na hisia ya ugonjwa, ikifuatiwa na uvimbe wa tezi za mate.

  • Utambuzi hutegemea dalili za kawaida.

  • Matibabu yanalenga kutuliza dalili.

  • Watoto wengi hupona bila matatizo yoyote, lakini maambukizi yanaweza kusababisha ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo au uvimbe wa ubongo.

  • Chanjo ya kawaida inaweza kuzuia maambukizi.

Watoto huambukizwa matumbwitumbwi kwa kuvuta matone madogo ya unyevunyevu yaliyokoholewa na mtu aliyeambukizwa au kwa kutangamana moja kwa moja na vitu vilivyochafuliwa na mate yaliyoambukizwa..

Maambukizi haya kwa kawaida hayatokei kwa watoto walio chini ya umri wa miaka 2, hasa wale walio chini ya mwaka 1.

Kuambukizwa mara moja virusi vya matumbwitumbwi kwa kawaida hutoa kinga ya maisha yote, ambayo inamaanisha kuwa mtu ambaye amewahi kuwa na matumbwitumbwi hapo awali hatapata tena.

Matumbwitumbwi hayaambukizi sana kuliko surua. Katika maeneo yaliyo na watu wengi, hutokea wakati wowote wa mwaka lakini hutokea mara nyingi mwishoni mwa majira ya baridi kali na mwanzoni mwa masika.

Milipuko hutokea hasa miongoni mwa watu ambao hawajapata chanjo na ambao hawajawahi kuwa na matumbwitumbwi hapo awali. Hata hivyo, milipuko imetokea miongoni mwa watu ambao walipata chanjo, labda kwa kuwa baadhi ya watu hawapati kinga baada ya chanjo na, katika baadhi ya wengine, kinga huenda ikapungua baada ya muda. Pia, huenda ikawa watu wengine hawakupokea idadi iliyopendekezwa ya dozi za chanjo. Kabla ya chanjo ya kawaida, matumbwitumbwi yalitokea sana miongoni mwa watoto wa umri wa kwenda shule. Hata hivyo, sasa maambukizi yamekuwa ya kawaida zaidi miongoni mwa vijana na watu wazima kwa sababu ya kupungua kwa kinga.

Chanjo imepunguza kwa kiasi kikubwa idadi ya visa vya matumbwitumbwi nchini Marekani. Hata hivyo, matumbwitumbwi bado hutokea kwa viwango vya chini. Mlipuko wa matumbwitumbwi wa mwaka wa 2006 nchini Marekani ulisababisha visa 6,584. Tangu wakati huo, milipuko ya hapa na pale, hasa katika vyuo vikuu na katika jamii zingine zinazoishi karibu, imechangia kubadilika kwa visa kutoka kiwango cha chini cha 229 katika mwaka wa 2012 hadi kiwango kingine cha juu cha 6,369 katika mwaka wa 2016. Milipuko hii imeangazia hitaji la kuendelea kutumia chanjo.

Sawa na surua, matumbwitumbwi yanaweza kuenezwa na watu ambao wanasafiri kutoka maeneo ambapo matumbwitumbwi ni mengi zaidi na kupata matumbwitumbwi wakiwa nje ya nchi kabla ya kurudi nchini Marekani. Wasafiri hawa walioambukizwa kisha husambaza maambukizi, hasa katika maeneo ambapo watu wengi hukusanyika pamoja (kama vile vyuo vikuu) au miongoni mwa watu katika jamii zenye uhusiano wa karibu zinazoishi katika mazingira yenye msongamano au wasiotangamana sana na wengine.

Kutambua Mahali Tezi Kuu za Mate zilipo

Dalili za Matumbwitumbwi

Dalili za matumbwitumbwi huanza siku 12 hadi 24 baada ya kuambukizwa. Watu wengi huhisi baridi, maumivu ya kichwa, hamu duni ya kula, hisia ya jumla ya ugonjwa (malaise), na homa ya chini hadi ya wastani. Dalili hizi hufuatwa ndani ya saa 12 hadi 24 na uvimbe wa tezi za mate (parotitis), ambao hutokea zaidi siku ya pili na hudumu kwa siku 5 hadi 7.

Watoto wengine huvimba tezi za mate bila dalili zingine. Uvimbe huo husababisha maumivu wakati wa kutafuna au kumeza, hasa wakati wa kumeza vinywaji vyenye asidi, kama vile juisi za matunda ya machungwa. Tezi huwa na maumivu zinapoguswa. Katika hatua hii, halijoto kwa kawaida huongezeka hadi 103 au 104°F (takriban 39.5 au 40°C) na hudumu kwa siku 1 hadi 3.

Takriban asilimia 25 hadi 30 ya watu huwa hawapati dalili.

Mabusha
Ficha Maelezo

Mumps is characterized by painful enlargement of the salivary glands.

Photo courtesy of Sylvan Stool, MD.

Matatizo ya Matumbwitumbwi

Matumbwitumbwi yanaweza kuathiri viungo vingine isipokuwa tezi za mate, ikiwa ni pamoja na

  • Korodani

  • Ubongo na tishu ambazo zimefunika ubongo

  • Kongosho

Baada ya kubalehe, takriban asilimia 30 ya wanaume ambao hawajapata chanjo na asilimia 6 ya wanaume walioambukizwa waliopata chanjo hupata uvimbe wa korodani moja au zote mbili (okitisi). Kuvimba kwa korodani husababisha uvimbe na maumivu makali. Mara tu baada ya kupona, korodani iliyoathiriwa inaweza kuwa ndogo, lakini uzalishaji wa testosterone na uwezo wa kuzaa kwa kawaida haziathiriwi.

Kwa wanawake, uvimbe wa ovari (oophoritis) hautambuliki sana, hauna maumivu mengi, na hauathiri uwezo wa kuzaa.

Matumbwitumbwi husababisha kuvimba kwa safu za tishu zinazofunika ubongo (homa ya uti wa mgongo) katika asilimia 1 hadi 10 ya watu walio na uvimbe wa tezi za mate. Homa ya uti wa mgongo husababisha maumivu ya kichwa, kutapika, na kukakamaa kwa shingo.

Matumbwitumbwi pia husababisha uvimbe wa ubongo (encephalitis) katika mtu 1 kati ya watu 1,000. Encephalitis husababisha kusinzia, kukosa fahamu, au kifafa. Watu wengi hupona kabisa, lakini wengine huwa na uharibifu wa kudumu wa neva au ubongo, kama vile uziwi au kupooza kwa misuli ya uso, kwa kawaida ikiathiri upande mmoja tu wa mwili. Matumbwitumbwi hudhaniwwa kuwa chanzo kikuu cha uziwi wa upande mmoja kwa watoto katika sehemu za dunia ambapo viwango vya chanjo ni vya chini.

Kuvimba kwa kongosho (ugonjwa wa kongosho) kunaweza kutokea mwishoni mwa wiki ya kwanza ya maambukizi. Ugonjwa huu husababisha maumivu ya tumbo, kichefuchefu kali, na kutapika. Dalili hizi hupotea ndani ya takriban wiki moja na mtu hupona kabisa.

Matatizo mengine, kama vile uvimbe wa ini, figo, au misuli ya moyo, hutokea lakini ni nadra sana. Matatizo hayapatikani sana kwa watu ambao tayari walipata chanjo.

Utambuzi wa Matumbwitumbwi

  • Tathmini ya daktari

  • Vipimo vya maabara

Madaktari hufanya utambuzi wa matumbwitumbwi kulingana na dalili za kawaida, hasa zinapotokea wakati wa mlipuko wa matumbwitumbwi.

Vipimo vya maabara vinaweza kufanywa ili kutambua virusi vya matumbwitumbwi na kingamwili zake. Vipimo hivyo vinaweza kutumika kuthibitisha utambuzi lakini kwa kawaida hufanywa ili kurekodi milipuko kwa ajili ya afya ya umma.

Kipimo cha majimaji ya uti wa mgongo (spinal tap) hufanywa kwa watu wenye dalili za ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo au encephalitis.

Matibabu ya Matumbwitumbwi

  • Acetaminophen au ibuprofen kwa ajili ya kutuliza maumivu

Hakuna matibabu maalum kwa matumbwitumbwi. Ili kupunguza maumivu, watoto wanapaswa kula lishe laini na kujiepusha na vyakula vinavyohitaji kutafunwa sana au vilivyo na asidi. Dawa za kutuliza maumivu, kama vile acetaminophen na ibuprofen, zinaweza kutumika kwa maumivu ya kichwa na usumbufu.

Wavulana au wanaume wenye uvimbe wa korodani huhitaji kupumzika kitandani. Korodani inaweza kutegemezwa kwa kutumia kifaa cha kutegemeza cha michezo au kwa kutumia mkanda unaonata ambao umeunganishwa kati ya mapaja. Pakiti za barafu zinaweza kutumika ili kupunguza maumivu.

Ikiwa kongosho husababisha kichefuchefu kali na kutapika, viowevu vinaweza kutolewa kwa njia ya vena (kupitia mishipa), na watu hawapaswi kula au kunywa chochote kwa siku chache.

Watoto wenye ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo au encephalitis wanaweza kuhitaji maji ya mishipa na acetaminophen au ibuprofen kwa homa au maumivu ya kichwa. Ikiwa kifafa kitatokea, dawa za kupambana na kifafa zinaweza kuhitajika.

Ubashiri wa Matumbwitumbwi

Karibu watu wote wenye matumbwitumbwi hupona kabisa bila matatizo, lakini katika hali nadra dalili zinaweza kuwa mbaya zaidi tena baada ya takriban wiki 2.

Kinga ya Matumbwitumbwi

  • Chanjo ya MMR

Hakuna tena chanjo tofauti kwa ajili ya matumbwitumbwi pekee. Chanjo ya surua-matumbwitumbwi-rubella (MMR) ni chanjo ya muunganisho ambayo ina surua hai lakini waliodhoofika, matumbwitumbwi ba vurusi vya rubela. Chanjo ya MMR ni mojawapo ya chanjo za kawaida za utotoni na hutolewa kwa watoto katika mataifa mengi ambayo yana mfumo imara wa huduma za afya. Chanjo ya MMR na chanjo ya varisela (tetekuwanga) zinapatikana pia kama chanjo iliyounganishwa (chanjo ya MMRV).

Dozi mbili za chanjo ya MMR hupendekezwa mara kwa mara. Dozi ya kwanza hutolewa kati ya umri wa miezi 12 na 15 lakini inaweza kutolewa kwa watoto wenye umri wa miezi 6 wakati wa mlipuko wa surua au kabla ya kusafiri kimataifa. Dozi ya pili hutolewa kati ya umri wa miaka 4 na 6.

Watoto ambao walikuwa chini ya umri wa mwaka 1 walipochanjwa bado wanahitaji dozi 2 zaidi baada ya siku yao ya kwanza ya kuzaliwa.

Kwa baadhi ya watoto, chanjo husababisha homa kidogo na upele, lakini watu hawaambukizi.

Chanjo ya MMR kwa kawaida hutoa kinga ya kudumu.

MMR ni chanjo hai na haitolewi wakati wa ujauzito.

Wakati wa mlipuko, watu ambao wamepata chanjo lakini wako katika hatari kubwa ya kupata matumbwitumbwi (kama vile wanafunzi wa vyuo vikuu au wengine wanaoishi katika maeneo ambayo kumekuwa na mlipuko wa matumbwitumbwi) wanaweza kupewa dozi ya tatu.

Kwa maelezo zaidi kuhusu nani anapaswa na nani asipewe chanjo ya MMR, tazama Utoaji wa Chanjo ya MMR. Tazama pia Madhara ya Chanjo ya MMR.