kandidiasisi ni nini?
Kandidiasi ni maambukizi yanayosababishwa na chachu ya Kandida, ambayo ni aina ya kuvu.
Kandidiasi inaweza kutokea:
Kwenye tabaka la juu la mwili wako, mara nyingi huwa ni ya kawaida
Kusambaa sehemu kubwa ndani ya mwili wako (huitwa kandidiasi inayosambaa), ambayo ni yenye kutishia maisha
Kandidiasi kwenye tabaka la juu la mwili wako inaweza kumuathiri mtu yeyote. Kwa kawaida hutokea kwenye sehemu zenye hali ya joto na unyevunyevu kama vile:
Mdomo
Kwapa
Eneo la msamba
Ngozi iliyo katikati ya vidole vya miguu yako au chini ya matiti yako
Kwa kawaida kandidiasi inayosambaa hutokea kwa watu ambao wana mfumo dhaifu wa kingamwili au waliolazwa hospitalini kwa sababu ya ugonjwa mbaya. Inaweza kusafiri kupitia mtiririko wa damu na kuathiri viungo vingi, ikiwemo:
Vali zako za moyo
Ubongo
Macho
Figo
bandama
Kwa aina zote za kandidiasi, madaktari watakupatia dawa ya kuvu.
Je, nini husababisha kandidiasi?
Kandida kwa kawaida hupatikana kwenye ngozi yako, ndani ya utumbo wako, na ikiwa wewe ni mwanamke, katika sehemu za siri. Kwa kawaida, haisababishi matatizo.
Maambukizi ya Kandida juu ya mwili wako yana uwezekano mkubwa zaidi ikiwa:
Una kisukari, saratani au VVU katika hatua ya mwisho
Una mimba
Unatumia dawa za kuua bakteria
Kandidiasi inayosambaa sehemu kubwa kimsingi hutokea ikiwa:
Uko hospitalini kwa tatizo kubwa kama vile upasuaji mkubwa au matatizo ya hatua ya mwisho ya VVU
Una mabomba mwilini mwako (kwa mfano, ya kukulisha chakula)
Unaingiza dawa fulani za kuua bakteria kupitia mishipa
Je, dalili za kandidiasi ni zipi?
Dalili zinategemea aina ya kandidiasi uliyonayo.
In candidiasis of the mouth, white, painful patches form in the mouth—for example, under dentures (top photo) or on the tongue (bottom photo).
In candidiasis of the mouth, white, painful patches form in the mouth—for example, under dentures (top photo) or on the
Images courtesy of Jonathan Ship, MD.
In candidiasis of the mouth, white, painful patches may form on the inside of the lips.
In candidiasis of the mouth, white, painful patches may form on the inside of the lips.
© Springer Science+Business Media
In candidiasis of the mouth, white, painful patches may form on the tongue.
In candidiasis of the mouth, white, painful patches may form on the tongue.
© Springer Science+Business Media
This photo shows whitish patches caused by Candida.
This photo shows whitish patches caused by Candida.
Image provided by Kristle Lynch, MD.
Kwa kandidiasi ya ngozi unaweza kuwa na upele mwekundu wenye kuwasha ambao unaweza kufanana magamba. Aina nyingine za upele wa pepi husababishwa na Kandida.
Kwa kandidiasi ya mdomo wako, dalili ni pamoja na:
Madoa yenye rangi yeupe ya malai mdomoni mwako
Kupasuka kwenye pembe za mdomo
Kwa kandidiasi ya uke, dalili ni pamoja na:
Kutokwa na uchafu mwingi, mweupe au wa manjano (majimaji) kutoka kwenye uke wako
Madoa meupe ndani au nje ya uke
Mwako na kuwashwa kwenye sehemu za ndani au nje ya uke
Kwa kandidiasi inayoasambaa kwa hatua, dalili zako hutegemea na sehemu ya mwili wako ambayo imeathiriwa. Inaweza kuwa vigumu kwa madaktari kujua ni dalili gani zinasababishwa na kandidiasi na zipi zinasababishwa na matatizo mengine ya kiafya unayoweza kuwa nayo.
Je, madaktari wanawezaje kujua ikiwa nina kandidiasi?
Kwa kawaida madaktari hutambua kandidiasi kwenye eneo la nje la mwili wako kwa kuiangalia. Wanaweza kukwangua sampuli ya ngozi ili kuichunguza kwenye hadubini.
Kwa kandidiasi inayosambaa ndani, kwa kawaida madaktari hupima sampuli ya damu yako au tishu kuangalia kama kuna kuvu.
Je, madaktari hutibu vipi kandidiasi?
Madaktari hutibu kandidiasi kwa kutumia dawa ya kuvu. Kulingana na aina ya maambukizi uliyo nayo, unaweza kutumia dawa hizi kama krimu, kidonge, au unaweza kupewa kupitia mshipa (IV).