Bakteria wadogo wanaoishi ndani ya seli nyingine za viumbe hai

(Vesicular Rickettsiosis)

NaWilliam A. Petri, Jr, MD, PhD, University of Virginia School of Medicine
Imekaguliwa naBrenda L. Tesini, MD, University of Rochester School of Medicine and Dentistry
Imepitiwa/Imerekebishwa Imebadilishwa Jan 2024
v27409862_sw

Rickettsialpox ni ugonjwa wa rickettsial unaosababishwa na Rickettsia akari na kuenezwa na viwavi wa utiriri au utitiri wazima.

  • Dalili za rickettsialpox, ambazo ni nyepesi, ni pamoja na homa yenye kibaridi na kutokwa na jasho, maumivu ya kichwa, unyeti kwa mwanga, maumivu ya misuli na upele.

  • Ili kutambua maambukizi, madaktari wanapima sampuli ya upele na wakati mwingine kufanya vipimo.

  • Rickettsialpox hutibiwa kwa dawa ya kiuavijasumu.

Rickettsiae ni aina ya bakteria ambayo inaweza kuishi tu ndani ya seli za viumbe vingine. Rickettsiae inayosababisha rickettsiosis kwa kawaida huishi katika panya wa nyumbani (mwenyeji).

Rickettsialpox hutokea katika maeneo mengi ya Marekani na Urusi, Korea na Afrika. Rickettsiae huenezwa kwa binadamu wanapoumwa na viwavi wa utitiri au utitiri wazima. Utiriri huu unaweza pia kusambaza bakteria kwa panya wa nyumbani.

Dalili za Rickettsialpox

Dalili za rickettsialpox ni nyepesi. Kidonda kidogo kama kifungo kilichofunikwa na upele mweusi (ukurutu) huonekana mahali pa kuumwa. Hukua na kuwa kidonda kidogo kinachoacha kovu kinapopona.

Karibu wiki moja baadaye, dalili zingine hujitokeza. Hizi ni pamoja na homa yenye kibaridi na kutokwa na jasho, maumivu ya kichwa, usumbufu machoni kutokana na mwanga, maumivu ya misuli na upele ulioenea. Vinundu vya limfu vilivyo karibu vinaweza kuvimba.

Utambuzi wa Rickettsialpox

  • Tathmini ya daktari

  • Bayopsi na upimaji wa upele

  • Vipimo vya damu

Utambuzi wa rickettsialpox huashiriwa na dalili.

Ili kuthibitisha utambuzi, madaktari wanaweza kufanya kipimo cha kuakisi mwanga kwenye kingamwili, ambacho hutumia sampuli kutoka kwa upele. Au wanaweza kutumia mbinu ya mmenyuko wa mnyororo wa polima (PCR) ili kuwawezesha kugundua bakteria haraka zaidi.

Madaktari wanaweza kufanya vipimo vya damu ili kugundua kingamwili kwa bakteria. Hata hivyo, kufanya kipimo mara moja hakutoshi. Ni lazima kipimo kirudiwe wiki 1 hadi 3 baadaye ili kuangalia kama kuna ongezeko katika kiwango cha kingamwili. Hivyo, vipimo vya kingamwili haviwasaidii madaktari kugundua maambukizi mara tu baada ya mtu kuugua lakini vinaweza kusaidia kuthibitisha utambuzi baadaye.

Matibabu ya Rickettsialpox

  • Dawa za kuua bakteria

Rickettsialpox haihitaji matibabu; hata hivyo, matibabu ya kiuavijasumu cha dawa ya doxycycline inayomezwa kwa siku 5 hupunguza muda wa baadhi ya dalili.

Kinga ya Rickettsialpox

Kuzuia rickettsialpox kunahusisha kudhibiti idadi ya panya na kutumia dawa za kuua wadudu.

Kufanya mazingira yasivutie panya sana kunaweza kusaidia. Kwa mfano, watu wanaweza kuondoa marundo ya mbao, taka za majani, na takataka na kukata nyasi ndefu na vichaka kuzunguka nyumba. Panya wanaweza kujificha na kuweka viota katika maeneo kama hayo. Mashimo na nafasi zingine ambazo panya wanaweza kuingia ndani ya nyumba zinapaswa kuzibwa. Chakula chote kinapaswa kuhifadhiwa kwenye vyombo visivyoweza kuliwa na panya.