Paracoccidioidomycosis ni maambukizi ambayo husababishwa na kuvu Paracoccidioides brasiliensis.
Maambukizi haya kwa kawaida hutokea baada ya vijimbegu vinavyozalishwa na ukungu kuvutwa.
Watu wengi hawawi na dalili, lakini dalili, zikitokea, kwa kawaida hutokea miaka mingi baada ya watu kuvuta hewa yenye kuvu.
Paracoccidioidomycosis kwa kawaida husababisha kikohozi, homa, upungufu wa pumzi, na ugumu wa kupumua, lakini inaweza kusababisha vidonda vya ngozi na mdomo, uvimbe wa tezi za limfu na wakati mwingine maumivu ya tumbo.
Madaktari hutambua maambukizi kwa kutambua kuvu katika sampuli za tishu.
Madaktari kwa kawaida hutibu paracoccidioidomycosis kwa kutumia dawa ya kuzuia kuvu itraconazole na wakati mwingine pamoja na dawa zingine.
(Angalia pia Muhtasari wa Maambukizi ya Kuvu.)
Paracoccidioidomycosis husababishwa na kuvuta pumzi yenye vijimbegu. Vijimbegu vimepatikana kwenye udongo katika sehemu za Amerika Kusini na Kati pekee. Paracoccidioidomycosis hutokea mara nyingi zaidi kwa wanaume wenye umri wa miaka 40 hadi 50, hasa wafanyakazi wa kilimo katika maeneo ya vijijini ya Brazili.
Paracoccidioidomycosis kwa kawaida huathiri mapafu, ngozi, mdomo, koo na nodi za limfu na wakati mwingine huathiri ini au wengu.
Paracoccidioidomycosis inaweza kutokea kwa watu ambao wana mfumo wa kinga wenye afya. Hata hivyo, wakati mwingine hutokea kwa watu wenye mfumo wa kinga ulio dhaifu kwa sababu ya tatizo lingine au kwa kuwa wanatumia dawa zinazokandamiza mfumo wa kinga, kama vile steroidi (pia wakati mwingine huitwa glucocorticoids au corticosteroids).
Dalili za Paracoccidioidomycosis
Watu wengi wanaovuta hewa yenye vijimbegu hupata maambukizi ambayo hayasababishi dalili zozote.
Dalili, zikitokea, kwa kawaida hujitokeza miezi hadi miaka kadhaa baada ya kuambukizwa kwa mara ya kwanza. Wakati mwingine dalili hudumu kwa muda mrefu, lakini ni nadra kwa maambukizi kuwa hatari.
Dalili zinafanana na zile za nimonia. Watu huwa na kikohozi, homa, upungufu wa pumzi na ugumu wa kupumua. Dalili hizi zinaweza kutoweka zenyewe.
Maambukizi haya yanaweza kuenea kutoka kwenye mapafu hadi kwenye sehemu zingine za mwili.
Majeraha yenye maumivu (vidonda) yanaweza kutokea mdomoni na kwenye ngozi, mara nyingi usoni, hasa karibu na pua na mdomo, ikiwa ni pamoja na ulimi, koo, na fizi.
In this photo, paracoccidioidomycosis has caused 2 rough, gray plaques and other areas of inflammation (including redness and swelling).
Image courtesy of Karen McKoy, MD.
Nodi za limfu ambazo zimeambukizwa huvimba na usaha unaweza kutoka humo, na kupenya kwenye ngozi lakini ukisababisha maumivu kidogo. Nodi za limfu ambazo huambukizwa sana ni zile zilizo shingoni na chini ya mikono.
In paracoccidioidomycosis, infected lymph nodes in the neck become swollen, and pus may drain from them, breaking through the skin.
Image courtesy of www.doctorfungus.org © 2005.
Ini na wengu vinaweza kupanuka na tezi za limfu tumboni zinaweza kupanuka na wakati mwingine kusababisha maumivu ya tumbo.
Baadhi ya watu wenye paracoccidioidomycosis hupata ugonjwa sugu wa mapafu, ambao husababisha makovu (fibrosis), malengelenge, na uharibifu mkubwa katika mapafu (emphysema).
Paracoccidioidomycosis inapotokea kwa watu walio chini ya umri wa miaka 30 au kwa watu ambao wana maambukizi ya VVU au maambukizi ya VVU yaliyoendelea (pia huitwa UKIMWI), huwa kali zaidi. Huenea sana, ikiwa ni pamoja na kwenye uboho na viungo vingine. Watu huwa na homa na hupunguza uzito. Nodi za limfu, ini, na wengu huwa kubwa.
Utambuzi wa Paracoccidioidomycosis
Uchunguzi na ukuzaji wa sampuli za tishu zilizoambukizwa
Vipimo vya damu
Madaktari hushuku paracoccidioidomycosis kulingana na dalili za mtu na matokeo ya uchunguzi wa kimwili.
Ili kugundua paracoccidioidomycosis, daktari huchukua sampuli za tishu kwa ajili ya uchunguzi kwa kutumia darubini na kwa ajili ya ukuzaji.
Madaktari huenda pia wakafanya vipimo vya damu ili kugundua paracoccidioidomycosis.
Matibabu ya Paracoccidioidomycosis
Itraconazole
Dawa ya kuzuia kuvu ya itraconazole, inayotumiwa kwa njia ya mdomo, ndiyo tiba bora ya paracoccidioidomycosis.
Amphotericin B, dawa nyingine ya kuzuia kuvu, pia hufaa na mara nyingi hutumika kwa visa vikali sana.
Sulfamethoxazole/trimethoprim ni dawa ya kuua bakteria. Inaweza kuzuia Parakoksidioidi (Paracoccidioides) kukua na kusaidia kuponya baadhi ya vidonda. Dawa hii inaweza kuhitaji kutumiwa kwa muda mrefu.