Ugonjwa wa Osgood-Schlatter

(Ugonjwa wa Osgood-Schlatter)

NaNora E. Renthal, MD, PhD, Harvard Medical School
Imekaguliwa naMichael SD Agus, MD, Harvard Medical School
Imepitiwa/Imerekebishwa Imebadilishwa Sept 2025
v38720889_sw

Ugonjwa wa Osgood-Schlatter ni mwako wenye maumivu wa mfupa na gegedu juu ya muundi goko.

  • Ugonjwa huu unasababishwa na kutumia mguu kupita kiasi.

  • Dalili halisi zinajumuisha maumivu, kuvimba na udhaifu kwenye goti.

  • Utambuzi wa ugonjwa unajikita kwenye uchunguzi wa kimwili na wakati mwingine eksirei.

  • Tiba siku zote inajumuisha dawa za kupunguza maumivu na kupumzika.

Ugonjwa wa Osgood-Schlatter ni osteokondrosisi. Osteochondrosis ni tatizo la sahani za ukuaji za mifupa linalotokea mtoto anapokua haraka.

Ugonjwa wa Osgood-Schlatter unatokea kwa watoto wa umri kati ya miaka 10 na 15 na kwa kawaida huathiri mguu mmoja tu. Ugonjwa huu kwa kawaida unatokea sana miongoni mwa wavulana, lakini pengo la jinsia linapungua kwa kuwa wasichana wengi wanajihusisha kwenye programu za michezo.

Chanzo cha ugonjwa wa Osgood-Schlatter kinadhaniwa kuwa kuvuta sana na kwa kujirudia gegedu la kifuniko cha goti (patella) ambapo inajiambatisha juu ya muundi goko. Sehemu hii ya kujiambatisha inaitwa tibial tubercle. Watoto wengine wanapata uvimbe wa mfupa kwenye sehemu hii.

Dalili kuu za ugonjwa wa Osgood-Schlatter ni maumivu, uvimbe na ulaini kwenye tibial tubercle mbele ya goti chini tu ya kifuniko cha goti. Maumivu huzidi wakati waa kufanya shughuli na hupungua kwa kupumzika.

Utambuzi wa Ugonjwa wa Osgood-Schlatter

  • Tathmini ya daktari

  • Wakati mwingine eksirei

Madaktari wanakita utambuzi wa ugonjwa wa Osgood-Schlatter kwenye uchunguzi na dalili za mtoto.

Eksirei ya goti inaweza kuonyesha tibial tubercle imetanuka au imevunjika katika vipande. Hata hivyo, eksirei hazihitajiki isipokuwa mtoto huyo akiwa naa dalili zingine, kama vile maumivu na uvimbe ambao unasonge zaidi ya goti au maumivu yanayoambatana wekundu na ujoto. Dalili hizi zinaonyesha tatizo jingine, kama vile jeraha au kuvimba kwa kiungio.

Matibabu ya Ugonjwa wa Osgood-Schlatter

  • Mapumziko na hatua za kupunguza maumivu

  • Nadra kuzuia ujongevu, sindano za steroidi (pia huitwa glucocorticoids au corticosteroids) na upasuaji

Dalili za ugonjwa wa Osgood-Schlatter kwa kawaida huisha baada ya wiki au miezi kadhaa. Kuepuka mazoezi kupita kiasi na kukunja sana goti husaidia kupunguza maumivu. Hata hivyo, madaktari wanaruhusu watoto wenye ugonjwa huu kuendelea kushiriki kwenye michezo na mazoezi.

Matumizi ya dawa ya kupunguza uvimbe isiyo na asteroidi (NSAID), mazoezi ya kujinyosha na kutumia barafu kwenye goti lililoathiriwa kunaweza kusaidia kuondoa maumivu.

Mara chache, mguu unaweza kuhitaji kufanywa usijongee kwa kufungwa na plasta, steroid inaweza kuhitajika kudungwa chini ya ngozi kuzunguka tibial tubercle ili kupunguza mwako na mchakato wa upasuaji ambao unahusisha uondoaji wa vipande vya mfupa, kuchimba na kuchonga kunahitajika.