Uvimbe wa titi

(Maambukizi ya Titi)

NaJulie S. Moldenhauer, MD, Children's Hospital of Philadelphia
Imekaguliwa naOluwatosin Goje, MD, MSCR, Cleveland Clinic, Lerner College of Medicine of Case Western Reserve University
Imepitiwa/Imerekebishwa Imebadilishwa Aug 2024
v8531744_sw

Uvimbe wa titi ni uvimbe wenye maumivu kwenye matiti, kwa kawaida huambatana na maambukizi.

Uvimbe wa titi unaweza kutokea baada ya kujifungua, kwa kawaida wakati wa wiki 6 za kwanza na karibu kila wakati kwa wanawake wanaonyonyesha. Mara chache sana, maambukizi ya matiti hutokea baada ya jeraha au upasuaji. Kuwa na ugonjwa wa kisukari au kutumia dawa za corticosteroids huongeza hatari ya maambukizi ya matiti.

Ikiwa mtoto hajashikwa vizuri wakati wa kunyonyesha, mipasuko na maumivu yanaweza kutokea. Uvimbe wa titi ni tofauti na maumivu na kupasuka kwa chuchu ambazo mara nyingi hutokea siku za kwanza za kunyonyesha. Ikiwa ngozi ya chuchu au inayoizunguka itapasuka, bakteria kutoka kwenye ngozi wanaweza kuingia kwenye mifereji ya maziwa na kusababisha maambukizi.

Homa inayotokea wiki kadhaa baada ya kuanza kunyonyesha mara nyingi husababishwa na uvimbe wa titi.

Titi lililoambukizwa kwa kawaida huonekana jekundu na kuvimba na huhisi lenye joto na laini. Sehemu tu ya matiti inaweza kuwa jekundu na kuuma.

Mara chache, maambukizi ya matiti husababisha mfuko wa usaha (usaha wa titi). Eneo linalozunguka usaha huvimba, na usaha unaweza kutoka kwenye chuchu.

Madaktari hubaini utambuzi wa tatizo kulingana na matokeo ya uchunguzi wa kimwili.

Je, Ulijua...

  • Ikiwa maambukizi ya matiti yatatokea baada ya kujifungua, wanawake kwa kawaida wanapaswa kuendelea kunyonyesha.

Matibabu ya Uvimbe wa Titi

  • Kutoa maziwa kabisa kutoka kwenye titi

  • Dawa za kutuliza maumivu, kama vile acetaminophen au dawa zisizo za steroidi za kuzuia uvimbe (NSAID)

  • Wakati mwingine dawa za kuua bakteria

Maumivu na uvimbe hudhibitiwa kwa kubana kwa kitu baridi na dawa za kutuliza maumivu, kama vile acetaminophen au NSAID, ikiwa ni pamoja na ibuprofen. Titi linapaswa kutolewa maziwa kabisa wakati mifereji ya maziwa imejaa kwa kunyonyesha au kukamua. Ili kuondoa kabisa maziwa ya mama, kubana kwa kitu cha za joto kunaweza kutumika kwenye matiti kabla au wakati wa kunyonyesha au kukamua. Wanawake wanahimizwa wanywe maji wa kutosha (kuongeza unywaji wa majimaji). Hatua hizi zinatosha kutibu visa vingi vya uvimbe mdogo wa titi au wa wastani.

Ikiwa uvimbe wa titi unaonekana kuwa unatokana na maambukizi ya bakteria, huwa unatibiwa kwa viuavijasumu, kama vile dicloxacillin, cephalexin, clindamycin au wakati mwingine erythromycin.

Wanawake wanahimizwa wanywe maji mengi.

Ikiwa dalili za maambukizi hazipungui au dalili ni kali, wanawake wanapaswa kutafuta matibabu—kwa mfano, ikiwa matiti yanaonekana mekundu, uwekundu unaenea, au mwanamke ana homa na kibaridi.

Wanawake walio na maambukizi ya matiti na wanaonyonyesha wanapaswa kuendelea kunyonyesha kwa sababu kutoa maziwa yote kwenye matiti husaidia katika matibabu na hupunguza hatari ya kupata usaha kwenye matiti.

Usaha wa titi hutanbuliwa kwa kutumia picha ya mawimbi ya sauti. Usaha hutibiwa kwa viuavijasumu na kwa kawaida hutolewa kwa upasuaji. Utaratibu huu unaweza kufanywa kwa kutumia ganzi ya eneo mahususi lakini unaweza kuhitaji dawa za kitulizo zinazodungwa kwenye mshipa (ndani ya vena) au ganzi ya mwili wote.

Ikiwa kutumia viuavijasumu hakupunguzi maambukizi au hakuna maambukizi, madaktari hufanya tathmini ili kuchunguza sababu nyingine za uvimbe wa titi.