Uvutaji sigara

Imepitiwa/Imerekebishwa Jun 2025 | Imebadilishwa Jul 2025
v34423137_sw

Kwa nini uvutaji tumbaku ni mbaya kwa afya yangu?

Watu waanavuta tumbaku kwenye sigara, biri na kiko. Uvutaji wa sigara una kemikali nyingi hatarishi zinazosababisha matatizo kwenye mwili wako wote, si mapafu yako tu.

Kuvuta moshi kutoka kwa mtu mwingine anayevuta sigara, kunaitwa uvutaji sigara mtumba, kunaweza kusababisha matatizo yaleyale sawa na kuvuta sigara mwenyewe.

Uvutaji sigara wakati wa ujauzito kunaweza kumdhuru mtoto ambaye hajazaliwa na kusababisha:

Vipi kuhusu sigara za kielektroniki?

Sigara za kielektroniki na sigara za mvuke zina kiowevu cha nikotini na kemikali za ladha, si tumbaku. Sigara ya kielektroniki au mvuke hupasha moto kiowevu na kuwa mvuke ambao unauvuta.

  • Unaweza kuwa mraibu wa sigara za kielektrobiki au mvuke ikiwa zina nikotini kwa sababu nikotini inafanya uwe mraibu

  • Kwa sababu hakuna kinachoungua kwenye sigara ya kielektroniki au mvuke, hupati matatizo yaleyale yanayosababishwa kwa kuvuta sigara

  • Dutu fulani kwenye mvuke, kama vile THC au vitamini E asetati, inaonekana kusababisha majaraha mabaya ya mapafu na wakati mwinginekifo

  • Sigara za kielektroniki na mvuke hazijakuwepo kwa muda mrefu madaktari kujua athari za muda mrefu

Je, nini kitatokea ikiwa mtoto atameza nikotini?

Mtoto ambaye amekula sigara au kitu chochote chenye nikotini (kama vile bigijii ya nikotini) anahitaji matibabu ya dharura. Madaktari watamtibu mtoto kuondoa sumu ya nikotini.

Athari za uvutaji sigara ni zipi?

Athari za haraka

Mara nyingi huwezi kuhisi kitu chochote kwa kuvuta sigara, lakini unaweza kuhisi:

  • Nguvu zaidi

  • Kumakinika vizuri zaidi

  • Kutohisi njaa sana

Ikiwa unajaribu uvutaji sigara na hujaizoea bado, unaweza kujihisi kichefuchefu tumboni mwako, ngozi kuwa nyekundu au yote mawili.

Athari za baada ya muda mrefu

Uvutaji wa sigara huua karibu kila ogani kwenye mwili wako. Matatizo makubwa yanayohusiana na uvutaji sigara ni:

Uvutaji sigara pia kunafanya uwe na uwezekano zaidi wa:

Uvutaji sigara pia husababisha:

  • Ngozi kavu na yenye mikunjo

  • Nywele kuwa nyembamba

  • Meno ya njano

  • Kupungua uzito

Dalili za kujiondoa

Ikiwa utaacha uvutaji sigara, huenda ukapitia hali ya kujiondoa. Kujiondoa ni wakati ambapo unahisi kuumwa baada ya kuacha kutumia dawa ya kulevya ambayo ulitumia kwa muda mrefu. Hali ya kujiondoa katika uvutaji sigara inaweza kusababisha:

  • Utake kuvuta sigara

  • Kujihisi mwenye hasira, wasiwasi, usingizi au huzuni

  • Kuumwa kichwa na kupata shida kumakinika

  • Kutetemeka(tikisiko)

  • Kuwa na maumivu ya tumbo na kuongezeka uzito

Je, ninapaswa kuzungumza na daktari wangu kuhusu uvutaji wangu wa sigara?

Ndiyo, unapaswa kuzungumza na daktari wako kuhusu uvutaji sigara na kiwango unachovuta.

Daktari wako anaweza: